Powder
JF-Expert Member
- Jan 6, 2016
- 5,280
- 7,149
Sahihi Mkuu, kanuni ya Mafanikio ya ki Mungu ni Moja tu, very simple....!Nice one mkuu, umeongea kitu kikubwa sana sema watu kuona hili ndo mtihani.
Mungu humpatia mazuri yule atendae mambo yenye msaada kwa wengine. With a pure heart you can manifest all desires of your heart, ila ukikimbilia ego na kujikweza utaishia kuwa mfiasi wa negative energy bila kujua
UNATAKA MUNGU ABADIRISHE MAISHA YAKO, JARIBU, JITAHIDI UBADIRISHE MAISHA YA WENGINE..... Automatically Mungu atabadirisha Maisha Yako, usitumie Nguvu nyingi kuomba Mungu akupe Utajiri, usipoteze Muda wako kufunga ili Mungu akupe Utajiri ama akupe Maisha ya juu, Wewe badirisha tu Maisha ya wengine Mungu ataanza kuachilia Neema hizo hutoamini.
Kwa Nini ni rahisi Mungu kukubariki pale unapobadirisha Maisha ya wengine, Sisi wote hapa ni Watoto wa Mungu, wapo Walemavu, Yatima, Wajane, labda wote Hawa Hawawezi kumudu Maisha Yao ya Kila siku, lakini Mungu kama Roho aliumba hii Dunia ambapo yeye kama yeye hawezi kuja kwenye hii Dunia ya Nyama, na Kuna Watu wanahutaji msaada wake, na hawezi kuwadondoshea Mabegi ya pesa Wahitaji, Wala kudondosha Mana Tena.
So Mungu anatamani apate Binadamu ambaye ataingia naye deal, na yenyewe, atapandikiza ideas za Biashara kichwani mwako, utaona wewe ndiyo unaweza, kumbe yeye amepandikiza hizo Business idea, atakuunganisha na Watu kimaajabu, ili ukipiga pesa, Sasa urudi kuwasaidia Masikini, na kadri unavyosaidia Masikini, ndivyo anavyoshusha Neema zake kwenye Maisha Yako.
SI inatokea Neema kidogo, unaanza kushinda Bar, unaingeza na Mke wa pili, unatembea na wake wa marafiki zako, nakuhakikishia Utakuja hapa Kwa hasira nyingi, kutupigia kelele kwamba Mungu ana Upendeleo.