JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Mastory ya bey​

My people,​



Kama ukipewa nafasi ya kuwa kitu kimoja tu maishani basi chagua kuwa mkarimu, ukarimu huleta mapenzi ya watu kwako,ukarimu humgeuza adui yako kuwa rafiki yako,ukarimu ndio ubinadamu wenyewe

Unaweza kuamua kuwa mtu wa kwanza kuwasalimia watu mara pale unapokutana nao, haikugharimu kitu chochote sana sana unavutia mapenzi kwako

Kuna kipindi fulani niliongazana na fundi fulani ambaye ni mgeni mazingira ya kwetu,aisee alinifundisha kitu,alikuwa anasalimia kila mtu ambaye anakutana nae,tena anasalimia kwa tabasamu kabisa,nilimkubali sana yule fundi

Unaweza kumfanya mtu atabasamu kwa sababu yako,hakika hilo ni jambo jema sana,siku zote wafanye watu wafurahie uwepo wako maishani mwao,iwe kazini,kwenye burudani,na popote pale ambapo utakuwa na watu pamoja

Unaweza kumlipia mtu nauli ya basi au kumnunulia kinywaji,kwako wewe unaweza ona ni jambo dogo lakini kwa mtendewa ni jambo kubwa sana kwake ambalo linabakia kwenye kumbu kumbu zake siku zote

Unaweza kumpisha mama mjazito kwenye siti ya daladala au mzee,au ukampakata mtoto mdogo ambaye mlezi wake amesimama kwenye daladala

Unaweza kumuelekeza mtu aliyepotea njia au kumfahamisha sehemu fulani ambayo anataka kuelekezwa

Kikubwa kadri ya uwezo wako jitahidi kuwa mkarimu kwa watu unao wajua na usio wajua,na hata kwa upande wa imani tunafahamishwa kwamba hakika watu wenye ukarimu wana thawabu zao kwa Mola wao

Siku zote jitahidi na azimia kuwa mwangaza kwa watu wengine

Ni hayo tu!
 
Saiv ni saa 2 Am lkn Kuna daladala ya kwenda tabata imejaa sasa huwa mnalala sangapi
 
Back
Top Bottom