ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,593
- 21,635
Mastory ya bey
My people,
Ni 1815hrs saa Za Afrika Mashariki nikiwa njiani kurudi home ndani ya basi aina ya Tata,nikiwa nasoma soft copy ya kitabu kinaitwa "When you die who will cry for you"
Huku unasikika mziki mkubwa kwenye hili basi huku Playlist ikiwa ni Mboso na ngoma yake "Naishiwa pawa"
Mara anasikika mhubiri mmoja at the back of the bus akihubiri neno la Mungu, tunajikuta abiria wote kama tumetekwa na sauti ile,hata na dereva nae akazima muziki kusikia nini kinaendelea
Tukiwa tunaendelea kula neno,mara mtu mmoja ambaye haifahamiki ana imani gani,akapaza sauti kujibizana na yule mhubiri ambaye amemua kutupa neno la bure kabisa
Akamwambia kama unataka kutangaza neno la Mungu nenda kanisani na sio unatupigia makelele humu,wakati huo huo dereva nae kaona isiwe tabu akafungulia mziki wake,sasa tukawa tunapata mambo mawili kwa pamoja,huku mziki na huku neno la Mungu na huku kuna abiria anapinga kitendo cha mhubiri kuhubiri ndani ya gari.
Sasa wakati haya yanaendelea nikawa najiwazia kwenye halmashauri yangu ya kichwa,kati ya mhubiri na mziki unaopigwa ndani ya basi,nani ndio anapiga makelele?
Kwa mtazamo wangu mziki ndio ulikuwa unapiga makelele na umejaa maneno ya kipuuzi wakati mhubiri alikuwa analeta maneno ya Mungu,sasa ilikuwaje yule abiria ashindwe kuona ukweli uko wapi? Au ndio ile inasemwa kipenda roho hula nyama mbichi.
Mabishano yakaendelea,yule abiria anasema kama unataka kutangaza injili basi nenda kanisani,maana humu kuna watu wana dini mbali mbali, mhubiri nae akasema wewe ndio unabagua kwasababu sote Mungu wetu ni mmoja
Abiria yule mbishi akasema, hata serikali inakataza mambo ya mahubiri kwenye mabasi,ndipo yule mhubiri akajibu kwa hoja kwamba mbona hata Viongozi wa serikali wakiapishwa huwa wana apa kwa maneno ya Mungu mbele ya hadhira na sio kwenye manyumba ya ibada?
Kiufupi siku yangu kazini leo ilikuwa tough ila baada ya kukutana na kisanga hiki siku yangu ikawa kama imechipua tena na kuwa ya kijani kibichi
Ule mjadala uliendelea kwenye back ground ingawa dereva nae aliamua kuongeza sauti ya mziki hivyo tulio kaa huku kati hatuweza tena kufuatilia mjadala ule
Ingawa nikaachwa na maswali mengi tu,hivi Shetani ana nguvu kiasi gani kiasi cha kumfanya yule abiria akerwe na yale mahubiri? Na shetani ana nguvu gani na kumfanya dereva adharau mahubiri na kuongeza sauti ya mziki iwe juu
Nikiwa naandika andiko hili kwenye notes za simu yangu,nikajikuta naweka umakini kwenye kuandika na mwisho nikapitishwa kituo ninachoshuka
Hivyo ndivyo siku yangu ilivyoishia,hakika maisha yana mambo mengi sana,ukostaajabu ya Mussa basi utayaona ya Furauni
Ni hayo tu!