JamiiForums Usiku wa manane

Mastory ya bey​


My people,​


Ni 1815hrs saa Za Afrika Mashariki nikiwa njiani kurudi home ndani ya basi aina ya Tata,nikiwa nasoma soft copy ya kitabu kinaitwa "When you die who will cry for you"

Huku unasikika mziki mkubwa kwenye hili basi huku Playlist ikiwa ni Mboso na ngoma yake "Naishiwa pawa"

Mara anasikika mhubiri mmoja at the back of the bus akihubiri neno la Mungu, tunajikuta abiria wote kama tumetekwa na sauti ile,hata na dereva nae akazima muziki kusikia nini kinaendelea

Tukiwa tunaendelea kula neno,mara mtu mmoja ambaye haifahamiki ana imani gani,akapaza sauti kujibizana na yule mhubiri ambaye amemua kutupa neno la bure kabisa

Akamwambia kama unataka kutangaza neno la Mungu nenda kanisani na sio unatupigia makelele humu,wakati huo huo dereva nae kaona isiwe tabu akafungulia mziki wake,sasa tukawa tunapata mambo mawili kwa pamoja,huku mziki na huku neno la Mungu na huku kuna abiria anapinga kitendo cha mhubiri kuhubiri ndani ya gari.

Sasa wakati haya yanaendelea nikawa najiwazia kwenye halmashauri yangu ya kichwa,kati ya mhubiri na mziki unaopigwa ndani ya basi,nani ndio anapiga makelele?

Kwa mtazamo wangu mziki ndio ulikuwa unapiga makelele na umejaa maneno ya kipuuzi wakati mhubiri alikuwa analeta maneno ya Mungu,sasa ilikuwaje yule abiria ashindwe kuona ukweli uko wapi? Au ndio ile inasemwa kipenda roho hula nyama mbichi.

Mabishano yakaendelea,yule abiria anasema kama unataka kutangaza injili basi nenda kanisani,maana humu kuna watu wana dini mbali mbali, mhubiri nae akasema wewe ndio unabagua kwasababu sote Mungu wetu ni mmoja

Abiria yule mbishi akasema, hata serikali inakataza mambo ya mahubiri kwenye mabasi,ndipo yule mhubiri akajibu kwa hoja kwamba mbona hata Viongozi wa serikali wakiapishwa huwa wana apa kwa maneno ya Mungu mbele ya hadhira na sio kwenye manyumba ya ibada?

Kiufupi siku yangu kazini leo ilikuwa tough ila baada ya kukutana na kisanga hiki siku yangu ikawa kama imechipua tena na kuwa ya kijani kibichi

Ule mjadala uliendelea kwenye back ground ingawa dereva nae aliamua kuongeza sauti ya mziki hivyo tulio kaa huku kati hatuweza tena kufuatilia mjadala ule

Ingawa nikaachwa na maswali mengi tu,hivi Shetani ana nguvu kiasi gani kiasi cha kumfanya yule abiria akerwe na yale mahubiri? Na shetani ana nguvu gani na kumfanya dereva adharau mahubiri na kuongeza sauti ya mziki iwe juu

Nikiwa naandika andiko hili kwenye notes za simu yangu,nikajikuta naweka umakini kwenye kuandika na mwisho nikapitishwa kituo ninachoshuka

Hivyo ndivyo siku yangu ilivyoishia,hakika maisha yana mambo mengi sana,ukostaajabu ya Mussa basi utayaona ya Furauni

Ni hayo tu!
 

Mastory ya bey​

My people,​



Kama ukipewa nafasi ya kuwa kitu kimoja tu maishani basi chagua kuwa mkarimu, ukarimu huleta mapenzi ya watu kwako,ukarimu humgeuza adui yako kuwa rafiki yako,ukarimu ndio ubinadamu wenyewe

Unaweza kuamua kuwa mtu wa kwanza kuwasalimia watu mara pale unapokutana nao, haikugharimu kitu chochote sana sana unavutia mapenzi kwako

Kuna kipindi fulani niliongazana na fundi fulani ambaye ni mgeni mazingira ya kwetu,aisee alinifundisha kitu,alikuwa anasalimia kila mtu ambaye anakutana nae,tena anasalimia kwa tabasamu kabisa,nilimkubali sana yule fundi

Unaweza kumfanya mtu atabasamu kwa sababu yako,hakika hilo ni jambo jema sana,siku zote wafanye watu wafurahie uwepo wako maishani mwao,iwe kazini,kwenye burudani,na popote pale ambapo utakuwa na watu pamoja

Unaweza kumlipia mtu nauli ya basi au kumnunulia kinywaji,kwako wewe unaweza ona ni jambo dogo lakini kwa mtendewa ni jambo kubwa sana kwake ambalo linabakia kwenye kumbu kumbu zake siku zote

Unaweza kumpisha mama mjazito kwenye siti ya daladala au mzee,au ukampakata mtoto mdogo ambaye mlezi wake amesimama kwenye daladala

Unaweza kumuelekeza mtu aliyepotea njia au kumfahamisha sehemu fulani ambayo anataka kuelekezwa

Kikubwa kadri ya uwezo wako jitahidi kuwa mkarimu kwa watu unao wajua na usio wajua,na hata kwa upande wa imani tunafahamishwa kwamba hakika watu wenye ukarimu wana thawabu zao kwa Mola wao

Siku zote jitahidi na azimia kuwa mwangaza kwa watu wengine

Ni hayo tu!
 
Back
Top Bottom