Jamani hapa kuna mapenzi kweli?

Jamani hapa kuna mapenzi kweli?

Sasa kinachonisikitisha ninapompa taarifa za kuvunja uhusiano analalamika na kunilaumu nimemchezea na kumpotezea mda. Wkt in reality yeye ndio naona anataka kunipotezea mda sasa...
Kwani akilalamika kuna shida gani? Muache alalamike Mpe Option Mbili achague 1.

Be a man,mpe chaguo aamue mwenyewe acha kubembeleza sanaaa hivi viumbe sometimes act kama humpendi vile, Ukauzu nnje ndani ila kumbe unamkubali.
 
So what did you advice him to do? Mind you, there's no where in my comment forcing him to take my advice, I only gave him my point of view concerning the matter
Thats a stupid advice, mwanamke akimfanyia hayo unayomshauri atazidi kumuona stupid
 
Huyu mwanamke nilikutana nae miezi mitatu iliyopita nikiwa katika harakati zangu za kikazi mkoa flani. Alinivutia muonekano wake na tabia (napenda wanawake wapole). Tukaanza mahusiano baada ya wiki mbili za kufahamiana. Mkoa aliopo anaishi kwa ndugu.

Umri ana miaka 25. Anafanya kazi kiwanda cha wahindi. Hawamlipi vizuri kutokana na maelezo yake na kazi anafanya siku sita za wiki, masaa 12 kwa siku. Hua anapewa siku moja tu ya kupumzika. Kwahyo ili tuwe tunaonana inalazimika mimi ndio niwe nasafiri kila napopata nafasi kwa vile tunaishi mikoa tofauti ni umbali wa masaa matatu kati yetu.

Tatizo binti shida hazimkauki. Binti anaomba sana ela. Kuanzia pesa ya nauli ya kwenda na kurudi kazini. Vocha. Kula. Mahitaji yake yote lazima aombe kubustiwa. Nimepiga hesabu kwa wiki pesa ndogo akiomba ni elfu 80, hua haipungui hapo. Sasa hivi ameomba nimpangie chumba nimnunulie na furniture ili tuwe tunakutana kwa uhuru tofauti na hivi tunavyokutana lodge kila nikija.

Kwahiyo nilimkalisha chini. Mshahara wangu haujui lakini ni zaidi ya mara tisa ya ule anaopokea yeye. Nikampa wazo anipe utaratibu nikajitambulishe kwao wanijue. Then aje tuishi wote huku tukitafta project iwe ya biashara au chochote ambacho ataweza kufanya akiwa huu mkoa niliopo mimi kuliko kuendelea kufanya kazi ambayo haimlipi huku akizidi kuniingizia unnecessary costs. Mipango ya ndoa then iendelee.

Amegoma katakata. Anadai kwa sasa kuishi na mwanaume ni mapema mno. Anataka kua independent awe na chumba chake, afanye kazi zake na maisha mengine. Nimemuambia kama haiwezekani basi kila mtu aendelee na maisha yake kuliko kupotezeana mda. Analia. Analalamika nimemchezea. Eti simpendi na simjali na nimebadilika! Binafsi nimeshindwa kumuelewa!
anataka awe huru kugegedwa na wahuni wengine,
achana naye mkuu, usijibu sms zake wala kupokea simu zake
 
Kama mtu amefika umri wa kuolewa, na we upo vizur hasahasa kiuchumi na uka-propose akawa anasita sita achana nae bro

Watakuja wamuoe wengine na wewe utakuja kuoa mwingine

As a man ikifikia point ukahis wewe ndie muhitaji zaid wa ndoa kuliko huyo mwanamke wako, piga chini haraka something is wrong

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo ambae bado yupo kwako ndio mzuri sasa, mbebee huko huko. Kuishi mwenyewe hujenga ubinafsi mbaya sana na hapa ndipo hata shida nyingi za kwenye ndoa huanzia.

Usikubali kumpangishia. Ila pia kama bado anahitaji kuishi mwenyewe inamaana hajakua bado na hayuko tayari kwa ndoa.
 
Hatupangi, tunaishi wote hapa kwangu. Nina nyumba ila naishi mwenyewe. Ninachohitaji ni kusettle na kua na familia. Nimeona yeye ni mtu sahihi kwangu na wala sina nia ya kumpoteza. A man needs to settle sometimes.
Sawa kama ni mtu sahihi...au hiyo sahihi umeitumia bahati mbaya
 
Miezi 3 ! Ni mapema sana kufikiria kumuoa...hebu relax kwanza upunguze haraka
 
Jibu Unalo Tayari 👉👉👉Nimemuambia kama haiwezekani basi kila mtu aendelee na maisha yake kuliko kupotezeana mda.....
Thanks
 
Analalamika nimempotezea mda na kumchezea
Mtumie meseji au mpigie simu, mwambie ana option mbili tu, na uamuzi ni wa kwake.
Option 1: Wewe uende kujitambulisha kwao na kukamilisha taratibu zote pamoja na mahari, kisha ahamie ulipo huku mkiendelea na taratibu za ndoa za kanisa.
Option 2: Aendelee na maisha yake huko aliko na wewe uendelee na ya kwako.
The ball should be in her court to decide.
 
Nimejaribu kupiga chini, anatuma sana text za kulalamika na kulia lia.
Its simple, mkalishe chini umueleze nia yako kwake. Na mwambie kama hayuko tayari basi aendelee na maisha yake then atakapokuwa tayari ndipo atakapompata anayemtaka.

Lakini pia yawezekana ameona unataka kumbeba kihuni tu wakati umri huo akili inawaza ndoa ni booonge la sherehe nk.
 
Yes ni mchaga. Umejuaje?
..

Unaweza kuta hiyo ndo Biashara yake inayomlipa.. Yani anao kumi hivi kama wewe

Embu chunguza sikuhizi wanawake wengi watoto wa mjini hawana kazi na hawajasoma lakini waishi vizuri kuliko wenye degree..

Nina manzi mmoja anafanya kazi kwenye Yale maduka ya simu kkoo.. Aisee nilimtegaga na vihela mwanzo nikamla show takatifu.. Baadae akawa akiomba hela simpi ya kuniacha anataka lakini akiwaza show anakuja chap kwa simu moja tuu..

Siku akaniambia hivi unadhani waume wote Wana akili kama wewe..?? Wapo wajinga ambao nikiwaomba wanatoa..


Aisee.. Kabla hujampa mwanamke pesa hakikisha Mama yako umemtumia zaidi.. Au kama una familia pia mkeo umempa zaidi

Mwanamke ambae ni wa kupita ukimpa pesa ataishia kukudharau tu.. Na kukuweka kundi la mabwege

Imefika mahali kuzaa mtoto wa kike imekuwa neema kuliko mtoto wa kiume.. Sababu now days imeonekana mtoto wa kike kusaidia nyumbani kuliko wa kiume..

#tujiangalie
 
Back
Top Bottom