Jamani hapa kuna mapenzi kweli?

Jamani hapa kuna mapenzi kweli?

Noma sana aisee. Na yeye hataki mkae pamoja?
Ishu ni kukaa pamoja? Basi mjaribu mwambie unataka ukienda kujitambulisha utoe na mahari kabisa mmalize. Uone atasemaje.
Ila kwa uzoefu mdogo tu, hapo kaka huyo mwanamke hakupendi yupo kwako kimsalahi tu, kuna mtu mwingine ambae ndo anampenda na wana future pamoja.
 
Yaani anataka kuwa independent alafu bado anakupiga mzinga wa hela ya chakula, nauli n.k!!!! Muulize anajua maana ya kuwa independent?

Piga chini

Kikosi cha mizinga hicho
Amenisikitisha sana. Anataka kua independent wkt mpaka nauli ya kumpeleka kazini na kumrudisha anaomba. Kuna mda nahisi anapenda tu na yeye aonekane ana kazi anatoka asubuhi na kurudi jioni lkn sio kwa ajili ya maslahi.

Au yawezekana mm sio mwanaume wa ndoto zake ananidanga tu
 

Nimevuta picha hapo analia na kulalamika unamchezea....
Hapo hamna mke... ana kitu anaficha.
Mwanamke anayekupenda na analalamika maisha magumu ma unampa option ya kuja kukaa nawe na kutafuta njia ya kumtafutia mradi wa kufanya hawezi kataa ofa...
Huyo anakutumia wewe kujinufaisha yeye na ukitimiza hilo ombi lake atakupiga tukio...
kutokana na huo muda mfupi na anavyokataa kuishi nawe ni wazi ana kitu anaficha na haumjui kabisa...
Basi yawezekana ana mwanaume wa ndoto zake ambae sio mimi. Huenda ananidanga tu. Nipo ktk harakati za kumpiga chini aisee.
 
Ushauri wangu.
1. Yeye kukataa kuja kuishi na wewe sio vibaya kila mtu na malengo yake.
2. Wewe kumwambia ahamie kwako pia ili akupunguzie gharama hujakosea.

Binti angekua anataka kuwa independent angepambana ajitegemee hata kwa vocha chakula na kodi hata kiasi kama hana uwezo wa kujimudu.

Kama kweli una malengo nae muulize kama yuko tayari kwa ndoa. Akihamia mji uliopo atakupunguzia hizo gharama unazosema.
Anasema yupo tayari kwa ndoa lkn mpaka akiwa na kwake.
 
Onyo
Usije ukamuoa mwanamke kwa kumuonea huruma maana utakuja lia siku moja.
Huyo anakutumia ili afanikishe mambo yake. Miaka 25 ni mwanamke mkubwa sana na ndiyo umri wa kuolewa. Siku zote weka misimamo yako kama mwanamke hataki kuifuta achana naye
Nashukuru kwa ushauri kaka. Nipo ktk hatua za kumbwaga taratibu taratibu
 
Hatupangi, tunaishi wote hapa kwangu. Nina nyumba ila naishi mwenyewe. Ninachohitaji ni kusettle na kua na familia. Nimeona yeye ni mtu sahihi kwangu na wala sina nia ya kumpoteza. A man needs to settle sometimes.
Hataki kuolewa mwenzio,. Wee tafuta anaetaka kuolewa, otherwise msubiri had atakapotaka yeye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom