Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,884
- 12,134
Kongamano la Wadau kuhusu Wajibu wa Vyombo vya Habari katika Kuhakikisha Uchaguzi wa Kuaminika (Agenda for Stakeholders’ Conference on the Role of the Media in Ensuring Credible Elections), linafanyika kwenye Ukumbi wa New Dodoma Hoteli, leo Aprili 30, 2024
Baadhi ya Washiriki na ambao wanatarajia kuchangia mada katika kongamano la leo Aprili 30, 2024 ni:
Kongamano hilo linafanyika wakati #Tanzania ikijiandaa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025. Pia, linashirikisha Wadau kutoka Vyama vya Siasa, Taasisi za Kiserikali na zisizo za Kiserikali
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Hali halisi ya Uandishi wa Habari Nchini #Tanzania wakati wa Uchaguzi, Vyombo vya Habari mara nyingi huwa havina Maandalizi ya pamoja kuanzia hatua za awali hadi kwenye Uchaguzi wenyewe na hadi wakati wa kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi.
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Uzoefu wangu unaonesha wakati wa Uchaguzi Vyombo vya Habari vya Tanzania vinajikita katika vitu ambavyo havina umuhimu
Kwa Lugha ya Mtaani tunaweza kusema ni ‘Media’ zinaelekeza nguvu kwenye ‘blabla flani hivi’, wanaangalia Maisha binafsi ambayo hayana uhusiano na athari kwa Wananchi moja kwa moja
Vyombo vya Habari vinakuwa vinadili na Wagombea ambao ama wamewapa posho au kuna lolote linafanyika ili wapate kula.
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Tunatambua kukua kwa Demokrasia Tanzania kunaendana na Uchaguzi wa Viongozi Kidemokrasia na kwamba Uchaguzi huu unahitaji Mazingira ya Haki, Uwazi na Uwajibikaji, Vyombo vya Habari vikifanya kazi kwa Weledi vinachagiza kuwepo kwa Haki, Uwazi na Uwajibikaji
Ni kwa msingi huo MCT tunaamini katika kaulimbiu ya Kongamano ambayo ni: Uandishi wa Habari za Uchaguzi kwa Weledi hujenga Usawa, Haki na Uwajibikaji
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Vyombo vya Habari vya Tanzania huwa havina uelewa mpana wa viwango vya Kimataifa vya masuala ya Uchaguzi, Sheria na Kanuni mbalimbali za Uchaguzi, Mifumo ya usimamizi wa Uchaguzi Tanzania, uelewa mpana wa Sera, itikadi ya Vyama vya Siasa na ilani zao za Uchaguzi.
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji (MCT): Nini MCT imekusudia kufanya? Kuviandaa Vyombo vya Habari mapema kwa kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa unaolenga kuvisaidia kufanya kazi ya kihabari ya kutoa taarifa sahihi kwa wakati sahihi (Information role), kufichua uovu na kuwajibisha (Watchdog role) na kuibua masuala ili yajadiliwe (Agenda setting role)
Kuratibu utafutaji na ukusanyaji rasilimali na kuvisaidia Vyombo vya Habari viwe na Uhuru wa Uhariri wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025. Ni matamanio ya MCT vyombo vya Habari Tanzania viwe na usafiri na posho zao wakati wa Kampeni badala ya usafiri na posho kutoka kwa Wagombea
Ernest Sungura, Mkurugenzi Mtendaji (MCT): Haki, Uwazi na Uwajibikaji katika masuala ya Uchaguzi yataletwa na Uandishi wa Habari za Uchaguzi unaozingatia Weledi na Maadili ya Kitaaluma. Hii ndiyo Kaulimbiu yetu tunapoelekea Uchaguzi
Matinyi Mobhare (Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa MAELEZO): Vyombo vya Habari vina wajibu mkubwa katika Jamii yoyote ambayo inapenda Demokrasia kwa kuwa vina uwezo wa kuelimisha na kuratibu Mijadala kwenye Umma
Tunapokaribia Uchaguzi jukumu la Vyombo hivyo linakuwa ni muhimu kwa kuwa kupitia wao Wananchi wanapata Habari na kuelimishwa jinsi ya kushiriki Uchaguzi ili kufanya Maamuzi sahihi wakati wa kupiga kura yenye manufaa kwao
Matinyi Mobhare (Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Habari Maelezo): Majukumu ya MCT katika kuendeleza Weledi, Maadili na Uwajibikaji katika Tasnia ya Habari, majukumu hayo ni muhimu katika Demokrasia inayostawi kama Tanzania, hivyo inapaswa kupongezwa, kwa nafasi yangu naelewa na kuthamini michango ya Vyombo vya Habari
Vyombo vya Habari vina wajibu wa kuripoti usawa na kuhakiki Habari kabla, wakati na baada ya Uchaguzi, hivyo ni nguzo muhimu kwa Demokrasia yetu
Msemaji wa Ubalozi wa Marekani, Kalisha Holmes: Akiwa katika Kongamano la Kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi, Msemaji wa Ubalozi wa Marekani, Kalisha Holmes amesema "Mitandao ya Kijamii imefanya baadhi ya mambo kuwa na nguvu kuliko tulivyotarajia, yamekuwa yakisambaa kwa kasi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma"
Ameongeza "Tumeingia katika nyakati ambazo Wananchi wetu wanahitaji kuelewa umuhimu wa taarifa ambazo zimehakikiwa, kwani chombo cha Habari kikiwa huru kinakwepa kulaghaiwa"
Jaji Joseph Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu: Akihudhuria Kongamano la Kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi, Jaji Joseph Warioba amesema "Mara nyingi katika mchakato wa #Uchaguzi ndipo ambapo kuna changamoto, unaanzia wakati wa uandikishaji, ukiharibu hapo basi unaharibu Uchaguzi wote"
Amesema "Baada ya hapo hatua inayofuata ni mpangilio wa Vituo vya Kupiga Kura, nia ni kurahisisha na kumwezesha Mwananchi kufika kwenye kituo akapiga kura kwa Usalama na haraka"
Ameongeza "Uandaaji wa vifaa pia ni muhimu, siku ya kupiga kura kukiwa na dosari ya vifaa inaweza kuharibu Uchaguzi, Mfano; Kusababisha baadhi ya Watu kutopiga kura kwa upungufu wa vifaa au kuchelewea kufikishwa kituoni"
Jaji Joseph Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu: "Tunaelekea kwenye #Uchaguzi wa 2024 na 2025, tuliona kilichotokea 2019 na 2020, yakijirudia inaweza kuwa mwanzo wa vurugu. Tunakumbuka yaliyotokea #Zanzibar pia miaka ya nyuma, yasije yakajitokeza tena"
Akiwa katika Kongamano la kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi amesema "Mwaka 2020 Wagombea tuliowapeleka hatuwezi kusema walikuwa ni chaguo la Wananchi, tujitahidi tutumie taratibu ili kuwapelekea Wananchi wagombea ambao wanatambulika"
Ameongeza "Tusipofanya hivyo #Demokrasia haitakuwa ya ukweli, Demokrasia isiyozingatia maoni ya Wananchi hiyo siyo Demokrasia, tutakuwa tunajidanganya. Tusiwe CAG wa Uchaguzi, kazi yetu iwe kuchambua makosa ya Uchaguzi, tujenge Demokrasi ya kweli"
Akishiriki Kongamano la Kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi, Mwanahabari Mkongwe, Jenerali Ulimwengu amesema "Chombo cha Habari cha Umma kama TBC kinatakiwa kuwa cha Umma, hakitakiwi kuegemea upande mmoja wa Kisiasa. Pili, hakitakiwi kuchukua matangazo ya biashara, kikifanya hivyo inamaanisha chombo ambacho kinaendeshwa kwa Kodi za Mwananchi kinaingia kwenye ushindani na Vyombo Binafsi, sio haki hata kidogo"
Pia, amesema Wakati wa Uchaguzi ni bora kuweka wazi msimamo wa Taasisi (Chombo cha Habari) kuwa ipo upande gani kuliko kufanya mambo kimyakimya na mwisho wake ni kukiuka weledi wa kazi
Ameongeza "Pia, kuna vyombo vya Serikali mfano Daily News, TBC, Habari Leo nakadhalika vinavyoendeshwa kwa fedha za Wananchi, vinakuwa sio vya Wananchi tena badala yake vinakuwa vya Serikali na hatimaye vinakuwa ni vya Mwenyekiti wa CCM"
Mwanahabari Mkongwe, Jenerali Ulimwengu amesema kuwa Tume ya Jaji Francis Nyalali iligusia kuondolewa kwa baadhi ya Sheria Kandamizi, badala ya kuondolewa au kupunguzwa zikaongeka
Amesema "Jaji Nyalali alishauri mali ambazo zilikuwa chini ya Chama Tawala na zilichangiwa na Wananchi wote zirejeshwe kwa Wananchi, hilo halikufanyika (Mfano viwanja vya Chama)"
Ameongeza "Pia, aligusia uwepo wa Wagombea Huru, hilo halijafanyika badala yake lazima uwe chini ya Chama ndio uruhusiwe kugombea"
MAXENCE MELO (Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums): Miaka ya nyuma kulikuwa na mabadiliko ya Habari, Mwaka 2020 kuna ‘Malaika’ walitokea wakazima Mtandao, tunaamini hilo halitajitokeza Mwaka 2025
Watanzania wanategemea Wanahabari kuwapa habari, wasipozipata kutoka kwa Wanahabari watatafuta kwa njia nyingine ya kuzipata na hiyo itamaanisha Vyombo vya Habari kupoteza tunu ya taaluma yao
JENERALI ULIMWENGU (Mwanahabari Mkongwe): Uchaguzi wa Mwaka 2020, Wanahabari waliandaa Mdahalo wa Wagombea kwa kushirikiana na JamiiForums, sote tulitarajia uwe mkubwa licha ya Sheria kadhaa kupitishwa kwa wakati huo kwa lengo la kudhibiti mambo kadhaa, kilichotokea Saa 48 kabla ya Mdahalo walishuka ‘Malaika’ fulani na Mdahalo ukafa
Wananchi hawakujua kwa kuwa tulikuwa hatujatangaza lakini ilitupa wakati mgumu kutokana na jitihada zilizotumika kuuandaa
MAXENCE MELO (Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums): Mwananchi ana nafasi ya kufanya maamuzi ya mabadiliko kwa kushiriki katika uchaguzi, hilo linawezekana kwa kupiga kura
Pia, kwa ambao wanahitaji kupaza sauti lakini hawataki kujulikana, JamiiForums imewapa nafasi ya kufanya hivyo kupitia Jukwaa la #FichuaUovu, hapo wanapata nafasi ya kueleza hoja na mitazamo yao kwa nia ya kujenga bila kujulikana na hilo linafanyika bure bila utambulisho wao kujulikana ndani ya Tovuti ya JamiiForums.com
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Mara nyingi Wanawake hawajitokezi kwenye Uchaguzi, hiyo inatokea ili kukwepa ukatili wa Kijinsia. Wanahabari wanatakiwa kuhakikisha wanalipigania hilo kwa lengo la kuwawezesha Wanawake wajitokeze kushiriki
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Kuna matukio ya Ukatili wa Kijinsia kwenye Mitandao ya Kijamii, wakati mwingine hata kurasa rasmi za Vyombo vya Habari zinaweka Picha au Video ambazo zinaruhusu maoni mengi ya kudhalilisha Wanawake
Komenti zinatakiwa kufutwa lakini zimekuwa zikiachwa, hilo ni jukumu la Chombo cha Habari, Mtu anatakiwa apingwe kwa hoja na sio jinsia yake
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Kuna suala la false news’ na ‘misinformation’, Wanahabari mnatakiwa kujipanga kuhakikisha Habari haitoki pasipokuwa na uhakiki wa hizo taarifa kwa faida ya kufanya Jamii ipate taarifa sahihi
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema Mwandishi anatakiwa kutambua kuwa Usalama unaanza na yeye mwenyewe. Mfano; Akienda kuchukua Habari kwenye tukio la Uchaguzi anatakiwa kuzingatia mazingira anayoyakuta hasa ya kiusalama kabla ya kuendelea na majukumu yake.
Akishiriki Kongamano la Kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi amesema "Ni jukumu la Vyombo vya Habari kuwapa Elimu Waandishi wake kuhusu Mazingira ya Usalama pamoja na kuwapa vitendea kazi vya kujilinda au utambulisho"
Ameongeza "Mfano anapokuwa katika majukumu kisha kukatokea vurugu, mavazi yenye utambulisho Mfano ya neno “PRESS” yanaweza kumsaidia na kutambulika kirahisi"
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema "Jeshi la Polisi linazingatia kuwa hakuna aliye juu ya Sheria, iwe ni Mwanasiasa, Askari Polisi au Mwandishi wa Habari. Pia, tunaheshimu Haki za Binadamu, mfano Watu wana Haki ya kukusanyika na kujieleza"
Akiongea katika Kongamano la kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi, Misime amesema "Tunapotimiza majukumu yetu kwa mujibu wa Sheria, Jeshi la Polisi linakuwa linamhakikishia Mwandishi wa Habari kufanya kazi yake kwa Amani na Utulivu"
- Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu
- Dr. Joyce Bazira, Mjumbe wa Bodi ya Uongozi Baraza la Habari la Tanzania (MCT)
- Ernest Sungura, Mkurugenzi Mtendaji MCT
- Matinyi Mobhare, Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa MAELEZO
- Rosemary S. Senyamule, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
- Dr. Michael Anthony Battle, Balozi wa Marekani
- Jenerali Ulimwengu, Media Consultant
- Edda Sanga, Media Consultant
- Pili Mtambalike, Media consultant and trainer
- Maxence Mello, Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums
- Ludovick Utouh, Director Wajibu Institute
- Engineer Andrew Kisaka, Principal Broadcast Engineer (Tanzania Communication Regulatory Authority -TCRA)
- Zitto Kabwe, ACT- Wazalendo
- David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi
- Thabit Idarous Faina, Director Zanzibar Election Commission
- Hamad Masoud Hamad, CUF Secretary General
- Jacob Nyukuri Nyongesa, Senior Officer Research Planning and Strategy - Media Council of Kenya
- Jennifer Thomas, Associate Professor, Department of Media, Journalism and Film, Howard University
- Absalom Kibanda, Senior Editor
Kongamano hilo linafanyika wakati #Tanzania ikijiandaa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025. Pia, linashirikisha Wadau kutoka Vyama vya Siasa, Taasisi za Kiserikali na zisizo za Kiserikali
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Hali halisi ya Uandishi wa Habari Nchini #Tanzania wakati wa Uchaguzi, Vyombo vya Habari mara nyingi huwa havina Maandalizi ya pamoja kuanzia hatua za awali hadi kwenye Uchaguzi wenyewe na hadi wakati wa kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi.
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Uzoefu wangu unaonesha wakati wa Uchaguzi Vyombo vya Habari vya Tanzania vinajikita katika vitu ambavyo havina umuhimu
Kwa Lugha ya Mtaani tunaweza kusema ni ‘Media’ zinaelekeza nguvu kwenye ‘blabla flani hivi’, wanaangalia Maisha binafsi ambayo hayana uhusiano na athari kwa Wananchi moja kwa moja
Vyombo vya Habari vinakuwa vinadili na Wagombea ambao ama wamewapa posho au kuna lolote linafanyika ili wapate kula.
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Habari la Tanzania (MCT): Tunatambua kukua kwa Demokrasia Tanzania kunaendana na Uchaguzi wa Viongozi Kidemokrasia na kwamba Uchaguzi huu unahitaji Mazingira ya Haki, Uwazi na Uwajibikaji, Vyombo vya Habari vikifanya kazi kwa Weledi vinachagiza kuwepo kwa Haki, Uwazi na Uwajibikaji
Ni kwa msingi huo MCT tunaamini katika kaulimbiu ya Kongamano ambayo ni: Uandishi wa Habari za Uchaguzi kwa Weledi hujenga Usawa, Haki na Uwajibikaji
Ernest Sungura (Mkurugenzi Mtendaji (MCT): Nini MCT imekusudia kufanya? Kuviandaa Vyombo vya Habari mapema kwa kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa unaolenga kuvisaidia kufanya kazi ya kihabari ya kutoa taarifa sahihi kwa wakati sahihi (Information role), kufichua uovu na kuwajibisha (Watchdog role) na kuibua masuala ili yajadiliwe (Agenda setting role)
Kuratibu utafutaji na ukusanyaji rasilimali na kuvisaidia Vyombo vya Habari viwe na Uhuru wa Uhariri wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025. Ni matamanio ya MCT vyombo vya Habari Tanzania viwe na usafiri na posho zao wakati wa Kampeni badala ya usafiri na posho kutoka kwa Wagombea
Ernest Sungura, Mkurugenzi Mtendaji (MCT): Haki, Uwazi na Uwajibikaji katika masuala ya Uchaguzi yataletwa na Uandishi wa Habari za Uchaguzi unaozingatia Weledi na Maadili ya Kitaaluma. Hii ndiyo Kaulimbiu yetu tunapoelekea Uchaguzi
Tunapokaribia Uchaguzi jukumu la Vyombo hivyo linakuwa ni muhimu kwa kuwa kupitia wao Wananchi wanapata Habari na kuelimishwa jinsi ya kushiriki Uchaguzi ili kufanya Maamuzi sahihi wakati wa kupiga kura yenye manufaa kwao
Matinyi Mobhare (Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Habari Maelezo): Majukumu ya MCT katika kuendeleza Weledi, Maadili na Uwajibikaji katika Tasnia ya Habari, majukumu hayo ni muhimu katika Demokrasia inayostawi kama Tanzania, hivyo inapaswa kupongezwa, kwa nafasi yangu naelewa na kuthamini michango ya Vyombo vya Habari
Vyombo vya Habari vina wajibu wa kuripoti usawa na kuhakiki Habari kabla, wakati na baada ya Uchaguzi, hivyo ni nguzo muhimu kwa Demokrasia yetu
Ameongeza "Tumeingia katika nyakati ambazo Wananchi wetu wanahitaji kuelewa umuhimu wa taarifa ambazo zimehakikiwa, kwani chombo cha Habari kikiwa huru kinakwepa kulaghaiwa"
Amesema "Baada ya hapo hatua inayofuata ni mpangilio wa Vituo vya Kupiga Kura, nia ni kurahisisha na kumwezesha Mwananchi kufika kwenye kituo akapiga kura kwa Usalama na haraka"
Ameongeza "Uandaaji wa vifaa pia ni muhimu, siku ya kupiga kura kukiwa na dosari ya vifaa inaweza kuharibu Uchaguzi, Mfano; Kusababisha baadhi ya Watu kutopiga kura kwa upungufu wa vifaa au kuchelewea kufikishwa kituoni"
Jaji Joseph Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu: "Tunaelekea kwenye #Uchaguzi wa 2024 na 2025, tuliona kilichotokea 2019 na 2020, yakijirudia inaweza kuwa mwanzo wa vurugu. Tunakumbuka yaliyotokea #Zanzibar pia miaka ya nyuma, yasije yakajitokeza tena"
Akiwa katika Kongamano la kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi amesema "Mwaka 2020 Wagombea tuliowapeleka hatuwezi kusema walikuwa ni chaguo la Wananchi, tujitahidi tutumie taratibu ili kuwapelekea Wananchi wagombea ambao wanatambulika"
Ameongeza "Tusipofanya hivyo #Demokrasia haitakuwa ya ukweli, Demokrasia isiyozingatia maoni ya Wananchi hiyo siyo Demokrasia, tutakuwa tunajidanganya. Tusiwe CAG wa Uchaguzi, kazi yetu iwe kuchambua makosa ya Uchaguzi, tujenge Demokrasi ya kweli"
Pia, amesema Wakati wa Uchaguzi ni bora kuweka wazi msimamo wa Taasisi (Chombo cha Habari) kuwa ipo upande gani kuliko kufanya mambo kimyakimya na mwisho wake ni kukiuka weledi wa kazi
Ameongeza "Pia, kuna vyombo vya Serikali mfano Daily News, TBC, Habari Leo nakadhalika vinavyoendeshwa kwa fedha za Wananchi, vinakuwa sio vya Wananchi tena badala yake vinakuwa vya Serikali na hatimaye vinakuwa ni vya Mwenyekiti wa CCM"
Amesema "Jaji Nyalali alishauri mali ambazo zilikuwa chini ya Chama Tawala na zilichangiwa na Wananchi wote zirejeshwe kwa Wananchi, hilo halikufanyika (Mfano viwanja vya Chama)"
Ameongeza "Pia, aligusia uwepo wa Wagombea Huru, hilo halijafanyika badala yake lazima uwe chini ya Chama ndio uruhusiwe kugombea"
MAXENCE MELO (Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums): Miaka ya nyuma kulikuwa na mabadiliko ya Habari, Mwaka 2020 kuna ‘Malaika’ walitokea wakazima Mtandao, tunaamini hilo halitajitokeza Mwaka 2025
Watanzania wanategemea Wanahabari kuwapa habari, wasipozipata kutoka kwa Wanahabari watatafuta kwa njia nyingine ya kuzipata na hiyo itamaanisha Vyombo vya Habari kupoteza tunu ya taaluma yao
JENERALI ULIMWENGU (Mwanahabari Mkongwe): Uchaguzi wa Mwaka 2020, Wanahabari waliandaa Mdahalo wa Wagombea kwa kushirikiana na JamiiForums, sote tulitarajia uwe mkubwa licha ya Sheria kadhaa kupitishwa kwa wakati huo kwa lengo la kudhibiti mambo kadhaa, kilichotokea Saa 48 kabla ya Mdahalo walishuka ‘Malaika’ fulani na Mdahalo ukafa
Wananchi hawakujua kwa kuwa tulikuwa hatujatangaza lakini ilitupa wakati mgumu kutokana na jitihada zilizotumika kuuandaa
Pia, kwa ambao wanahitaji kupaza sauti lakini hawataki kujulikana, JamiiForums imewapa nafasi ya kufanya hivyo kupitia Jukwaa la #FichuaUovu, hapo wanapata nafasi ya kueleza hoja na mitazamo yao kwa nia ya kujenga bila kujulikana na hilo linafanyika bure bila utambulisho wao kujulikana ndani ya Tovuti ya JamiiForums.com
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Mara nyingi Wanawake hawajitokezi kwenye Uchaguzi, hiyo inatokea ili kukwepa ukatili wa Kijinsia. Wanahabari wanatakiwa kuhakikisha wanalipigania hilo kwa lengo la kuwawezesha Wanawake wajitokeze kushiriki
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Kuna matukio ya Ukatili wa Kijinsia kwenye Mitandao ya Kijamii, wakati mwingine hata kurasa rasmi za Vyombo vya Habari zinaweka Picha au Video ambazo zinaruhusu maoni mengi ya kudhalilisha Wanawake
Komenti zinatakiwa kufutwa lakini zimekuwa zikiachwa, hilo ni jukumu la Chombo cha Habari, Mtu anatakiwa apingwe kwa hoja na sio jinsia yake
NEEMA LUGANGIRA (Mbunge): Kuna suala la false news’ na ‘misinformation’, Wanahabari mnatakiwa kujipanga kuhakikisha Habari haitoki pasipokuwa na uhakiki wa hizo taarifa kwa faida ya kufanya Jamii ipate taarifa sahihi
Akishiriki Kongamano la Kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi amesema "Ni jukumu la Vyombo vya Habari kuwapa Elimu Waandishi wake kuhusu Mazingira ya Usalama pamoja na kuwapa vitendea kazi vya kujilinda au utambulisho"
Ameongeza "Mfano anapokuwa katika majukumu kisha kukatokea vurugu, mavazi yenye utambulisho Mfano ya neno “PRESS” yanaweza kumsaidia na kutambulika kirahisi"
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema "Jeshi la Polisi linazingatia kuwa hakuna aliye juu ya Sheria, iwe ni Mwanasiasa, Askari Polisi au Mwandishi wa Habari. Pia, tunaheshimu Haki za Binadamu, mfano Watu wana Haki ya kukusanyika na kujieleza"
Akiongea katika Kongamano la kujadili Tasnia ya Habari kuelekea Uchaguzi, Misime amesema "Tunapotimiza majukumu yetu kwa mujibu wa Sheria, Jeshi la Polisi linakuwa linamhakikishia Mwandishi wa Habari kufanya kazi yake kwa Amani na Utulivu"