Hiyo red unamaanisha Vatican? Sisi tunaangalia katiba yetu ya nchi na leseni za bishara zinavyosema - hii kitu ni kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutokufuata sheria za biashara na kibenki za nchi yetu. Huu ni ubaguzi, upendeleo na ubaguzi dhahiri ambao Shekh Simba anadhiirisha hapo juu - kuwa waislamu mameumia sana na 'high interest rate' sasa hizi interest rate nani azilipe? Muumini wa dini ya kimila na mkristo?
Je Tanzania inachanganya civil na islamic law katika kuendesha nchi?
Hebu nieleweshe wapi katika Katiba imemtaja Mwanamke kuwa sehemu tofauti na Mtanzania mwengine? Au wapi Mkiristo au Muislamu ametajwa kwa jina kama sehemu ya Katiba? Mwanamke, Muislamu, Mkristo ni sehemu ya jamii na wanahitaji huduma za kijamiina kwa maana hiyo si kosa la Kikatiba kuwa na Hospitali ya Wakristo, kuwa na Chuo cha Waisllamu na si kosa kuwa na Benki ya Wanawake na si kosa kuwa na Benki ya Waislamu na kama itaonekana kuna haja basi na kuwe na Benki ya Wakristo (kama wanataka kufuata misingi halisi ya dini yao) na hata kina Kingunge nao nawafungue Benki yao.
Tanzania na ulimwengu wote kwa jumla tunaishi kwa kuwa na imani na matamanio tofauti na haya ndio yanayosababisha tuwe na mabaa, tuwe na makanisa na misikiti ndani mwetu.