Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Kwani Zitto ndio chadema? Chama kilikuwepo kabla yeye ya kuwa mwanachama.
 
Kwa CHEDEMA ni ZITTO au kambla ya zito chadema haikuwepo? Nafikiri SLAA ni zaidi ya ZITTO, tukatae tusikatae. kwanza zitto hafai kuwa kiongozi kwani ana hasira pia ana jazba. Alafu ni wale wa fikra za mwenyekiti wa chama zidumishwe.
 
Zitto azushiwa tuhuma nzito

Wakati Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mheshimiwa Zitto Kabwe yuko nje ya nchi, hapa nchini amezuliwa tuhuma nzito kwamba ana mpango wa kukitosa chama chake cha CHADEMA na kujiunga na chama cha Mapinduzi, CCM.

Uvumi huo ambao umeibuka na kuzagaa kwa kasi katika mitaa kadhaa ya Jiji la Dar es Salaam, umeibuka ikiwa ni siku chache tu tangu swahiba wake wa karibu, ambaye alikuwa Afisa Habari wa CHADEMA, David Kafulila kutimkia chama cha NCCR-Mageuzi.

Aidha uvumi huo umekuja ikiwa imepita miezi michache tangu mbunge huyo, aliporipotiwa kuwa katika mvutano wa kuwania nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA, ili kuvaana na mwenyekiti wa sasa, Bw. Freeman Mbowe.

Mhe. Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, alijitosa kwenye uchaguzi mkuu wa chama hicho akitaka agombee nafasi ya uenyekiti, lakini akaondoa jina lake kwa kile kilichodaiwa kuwa aliombwa kufanya hivyo na wazee kwa maslahi ya chama.

Miongoni mwa madai yanayotolewa na watu mbalimbali dhidi ya Mhe. Zitto ni kwamba huko CCM ameahidiwa cheo kikubwa baada ya uchaguzi mwakani.

Hata hivyo Alasiri imewasiliana na Mhe. Zitto aliyepo nje ya nchi hivi sasa kwa njia ya mtandao, ambapo mwenyewe amepinga vikali uvumi huo.

Amesema uvumi huo hauna ukweli wowote na kwamba wanaomzushia, wana mpango wa kumchafulia jina kwa wapiga kura wake.

“Sina mpango wala sifikirii kuhama CHADEMA kwenda chama chochote, sembuse CCM. Sijawahi kukaribisha wala kufikiria wazo hilo katika kichwa changu na ninamwomba Mungu, wazo hilo lisije,” alisema Mhe. Zitto katika ujumbe wake mfupi kwa gazeti hili alioutuma kwa njia ya mtandao.

Tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa CHADEMA, viongozi wake wamekuwa na malumbano ambayo hivi karibuni yalisababisha Katibu Mkuu wa chama hicho, kuwatimua kwenye uongozi baadhi ya wanachama. Mmoja wa waliotimuliwa baadaye alitangaza kuhamia NCCR- Mageuzi.


CHANZO: ALASIRI
 
Zito bora ukakaa kimya maana naona kila siku inaanzishwa thread mpya juu yako
 
Mod Tetesi tetesi ziende kunakohusika

Zitto kaenda Trinidad kwenye kikao cha commonwelth atakujibu baadae au m pm
 

Sasa huu ni upumbavu kabisa, hebu mwandishi wa thread hii jaribu kusoma thread za nyuma na utaona zitto ameulizwa na amejibu haya maswali unayomuuliza. Uvivu wako wa kuanzisah thread bila kusoma zilizopo usitusumbue wote. Watu wengine bana
 
.....
 
Zitto sio mtu wa kukurupuka wala tamaa aende CCM ili iwe nini cheo au pesa? Kama ni pesa akitaka anaweza kuzipata nyingi tu akiwa huko huko Chadema. Remember ile miburungutu aliyo ikataa ya Barrick?
 
Na mie uvivu wangu umetoka wapi?

Mtoa post amewakilisha kilichoandikwa kwenye gazeti...not his idea..Sasa kwa vile ni Zitto mnataka isijadiliwe...mbona JK katoka kwenye gazeti anabembea tayari watu wana comment heavily...kwani JK hajajadiliwa huko nyuma?mbona hamsemi agenda zake zisitishwe?....lets be a little bit democratic...kama issue ya Zitto ilijadiliwa kabla si umredirect mtoa thread easily na sio kukashifu watu..pengine ilipojadiliwa alikuwa sio member wa JF....

Tuache jazba na utemi humu....nasi twaweza pia
 
Jamani eee mwacheni Zitto wa watu apumzike,kila siku Zitto Zitto tumechoka,Hivi hamna mambo mengine ya kujadili?Zitto dont bodha kujibu hoja za hii thread jisomee mwaya rafiki yangu usije ukafeli bure.Nadhani huu ni mkakati maalumu wa kukuchafua na kukupotezea muda wako halafu ufeli wapate kingine cha kusemea.Bika buku kamanda kaza msuli.
 

Kuambiwa mvivu si jazba, ulipaswa kusoma hiyo post uielewe, majibu ya zitto yamo humohumo, sasa ulitaka zitto afafanue nini???
 
Sasa huu ni upumbavu kabisa, hebu mwandishi wa thread hii jaribu kusoma thread za nyuma na utaona zitto ameulizwa na amejibu haya maswali unayomuuliza. Uvivu wako wa kuanzisah thread bila kusoma zilizopo usitusumbue wote. Watu wengine bana
hata hivyo hili gazeti huwa ni kama la udaku vile, kwa hiyo inabidi uwe makini wakati unalisoma.
 
Sasa huu ni upumbavu kabisa, hebu mwandishi wa thread hii jaribu kusoma thread za nyuma na utaona zitto ameulizwa na amejibu haya maswali unayomuuliza. Uvivu wako wa kuanzisah thread bila kusoma zilizopo usitusumbue wote. Watu wengine bana
hata hivyo hili gazeti huwa ni kama la udaku vile, kwa hiyo inabidi uwe makini wakati unalisoma.
 
KUNA UVUMI?? Mvomo ktk kichwa cha mtu sii hoja ya kujadili hapa JF jameni. Zitto fanyia kazi facts not rumours!!!!!
 
Politics.... sorry.... Politricks is the dirtiest game! You aint seen nothing yet! This is an appetizer, we're not even at the main course, yet, let alone dessert! Game on!
 
Wazushi ni hao hao wa Alasiri , sasa wao wanasema kuna uvumi kumbe wao ndio wanataka kuvumisha huo uvumi.

Zitto, huna sababu ya kujibu haya .
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…