Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Zito bora ukakaa kimya maana naona kila siku inaanzishwa thread mpya juu yako

Ni kweli bwana Belo. This all hogwash! Juzi juzi Zitto katoa thread ya mahojiano na gazeti moja na kutoa msimamo wake kwamba yeye ni Chadema na wote tumesoma hapa hapa. ili la uzushi ni diversionary tu. Zitto amekuwa kama punching bag. Jamani JF sio kama kijiwen!
 
Sinkala ni heri uwaonyeshe manake wengine hawajui kusoma!!!, hawakuona kuwa majibu ya Zito yako kwenye habari yenyewe.
 
Mimi nadhani kujadili kitu sio mbaya muhimu kimeletwa na kujadiliwa ni vizuri na issue ya kusema kwamba imeshawahi kujadiliwa hiyo ndani sio sahihi kwani inawezekana hapo alipozushia mara ya kwanza ilikuwa hajawa tayari kuingia huko na sasa pengine mipango yake imekaa sawa, kwani mbona kuna viongozi wengi awali walisingiziwa wanatoka katika vyama vyao na kuingia vyama vyengine lakini mwanzo walisikika wakikataa na baadae tukawasikia wamejiunga na kukuabishiwa kadi zao kwa mbwembwe nyingi?

sina shaka na Zitto juu ya msimamo wake katika kubakia chadema ila naamini kwamba kama wengine walivyokuwa na haki ya kuingia katika chama kengine naye ana haki kamili kuwepo katika chama unaweza kubakia kutokana na sera nzuri na kuziamini na unaweza kubakia kwa ajili ya maslahi yao lakini jengine na kubwa ni kulinda heshima ya chama chako na wewe mwenyewe kama ilivyo kubakia katika chama ni hivyo hivyo kutoka na kuingia kwengine mtu anatakaiwa ayaone hayo pia.

salma
 
Nyote hamjui kitu. Habari sahihi ni kwamba Zitto anataka kuweka historia hapa nchini kwa kujiuzulu ubunge -- hatua ambayo atachukua mara tu akirudi kutoka huko aliko majuu. Habari zinasema anaachana na siasa na anakwenda kufundisha katika chuo kimoja nchini Rwanda.Lakini pia habari nyingine zinasema amepewa kazi na swahiba wake RA kusimamia baadhi ya shughuli zake zinazohamishiwa nchi jirani ya Kenya. Hawezi kurudi CCM labda baada ya miaka mingi sana watu wakianza kusahau "usaliti" wake kwa Watanzania. lakini pia anatambua fika kuwa hawezi kamwe kulipata tena jimbo lake akisimama mwaka kesho -- kwa kupitia Chadema. mimi naona ule uamuzi wa Chadema waa kumzuia kuingia katika 18 katika azma yake ya kutaka kuukwaa ubosi wa Chadema ulikuwa sahihi kwani akina RA walikuwa wametayarisha kitita cha msimamo kwa delegates ili ambwage Mbowe.Na angeukwaa tu, basi akina Slaa na wengine wangetokomezwa huko wanakojua na maswahiba wa RA kukiteka chama. lakini mambo yote hayo yameharibika vibaya mno na ndiyo maana ameamua kujiuzulu ubunge.
 
Nyote hamjui kitu. Habari sahihi ni kwamba Zitto anataka kuweka historia hapa nchini kwa kujiuzulu ubunge -- hatua ambayo atachukua mara tu akirudi kutoka huko aliko majuu. Habari zinasema anaachana na siasa na anakwenda kufundisha katika chuo kimoja nchini Rwanda.Lakini pia habari nyingine zinasema amepewa kazi na swahiba wake RA kusimamia baadhi ya shughuli zake zinazohamishiwa nchi jirani ya Kenya. Hawezi kurudi CCM labda baada ya miaka mingi sana watu wakianza kusahau "usaliti" wake kwa Watanzania. lakini pia anatambua fika kuwa hawezi kamwe kulipata tena jimbo lake akisimama mwaka kesho -- kwa kupitia Chadema. mimi naona ule uamuzi wa Chadema waa kumzuia kuingia katika 18 katika azma yake ya kutaka kuukwaa ubosi wa Chadema ulikuwa sahihi kwani akina RA walikuwa wametayarisha kitita cha msimamo kwa delegates ili ambwage Mbowe.Na angeukwaa tu, basi akina Slaa na wengine wangetokomezwa huko wanakojua na maswahiba wa RA kukiteka chama. lakini mambo yote hayo yameharibika vibaya mno na ndiyo maana ameamua kujiuzulu ubunge.

kweli kaka, ila jiweke nafasi ya Zito hivi sasa, zushiwa na andikwa kama hapo juu, bila vithibitisho!

Halafu kesho, tutalia tunataka upinzani mzuri, ukue, tunataka mabadiliko!! nataka unieleze kwa style hii kama mwana CCM kaamua kukaa chini na kutunga, tutafika ni mpinzani gani ataweza kusimama nchi hii, ikiwa kuanzia intelectual mpaka vijiweni they think the same!

Umesema pia msaliti! alianza lini? mtu anakuwa msaliti baada ya kusimamishwa ubunge na kufunua ishu za Buzwagi?? na je mtu akiwa na mawazo tofauti ni kwa namna gani tutamtofautisha na asiye msaliti?

Nipe jina la mtu mwenye mawazo na mtazamo tofauti ambaye hakuitwa msaliti nchi hii!

'tunataka kila mtu awaze kama sisi' athari za zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa chama ni kubwa, maana zinaanzia ngazi ya familia, hivyo kwa kila baba anayeongoza familia anaweza kuwa nazo!!!

I surmise that we are matching at the same point, CCM will rule for long time....!!!! maana kila mpinzani atatungiwa kitu

we need to re-think

ni maoni tu, you may think what you want!
 
zittokabwe.jpg


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, ambaye anamuunga mkono aliyekihama chama hicho.

Na Elizabeth Ernest

NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ametangaza kumuunga mkono swahiba wake David Kafulila kugombea ubunge jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi na tayari ametoa magari matatu kwa ajili ya kumsaidia kujiimarisha jimboni huko.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka kwa watu walio karibu na Zitto na Kafulila vinasema kwamba, kiongozi huyo wa Chadema ameamua kumuunga mkono Kafulila ili kuhakikisha jimbo hilo linaondoka mikononi mwa CCM na kwenda upinzani.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, NCCR-Mageuzi ilishika nafasi ya pili huko Chadema ikishika nafasi ya tatu kwenye matokeo ya ubunge. Katika uchaguzi wa mwaka 2000, jimbo hilo lilichukuliwa na NCCR-Mageuzi kabla ya 2003 kuchukuliwa na CCM katika uchaguzi mdogo.

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa hivi karibuni, Chadema kilijizolea viti 12, NCCR-Mageuzi 11 na CCM kilipata viti 20. Kulingana na takwimu hizo, upinzani uliongoza.

Mwaka 2005 kama Chadema ambacho kilishika nafasi ya tatu kingeiunga mkono NCCR-Mageuzi, Jimbo hilo sasa lingekuwa katika mikono ya upinzani kwa kuwa kura za kambi hiyo zilikuwa nyingi kuliko za CCM.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, Zitto anaamini kwamba, Kafulila ndiye aliyejenga Chadema kama chama ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano na NCCR-Mageuzi katika maeneo ambayo chama hicho kina nguvu.

"Zitto amekwisha weka bayana kuwa katika Uchaguzi Mkuu ujao upande wa jimbo hilo anamuunga mkono Kafulila kwa kuwa anaamini atashinda na kuimarisha upinzani," kilisema chanzo cha kuaminika.

Maelezo hayo ya Kabwe yamekuja huku Kafulila akijiandaa kwenda jimboni humo kuhutubia mikutano ya hadhara akitumia magari ya Zitto.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zinasema kuwa Kafulila ambaye sasa ni mwanachama wa NCCR-Mageuzi ataanza ziara yake mkoani humo Desemba 8, mwaka huu akiwa na viongozi wa kitaifa wa NCCR-Mageuzi.

Kwa mujibu wa habari hizo, Kafulila pia anatarajia kuzungumza na wanachama wa Chadema mkoani Kigoma na kuzunguka maeneo mbalimbali kwa magari ya Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini.

Kafulila aliliambia gazeti hili jana kuwa atatumia magari ya Zitto kwa kuwa ni rafiki yake wa karibu.

“Mimi na Zitto ni marafiki wa siku nyingi, tayari nimezungumza naye na amekubali kunisaidia kama rafiki yake wala sijakodisha," alisema Kafulila jana na kuongeza:

"Amenipa magari yake kwa ajili ya usafiri kwa sababu nitaondoka na watu wangu huku Dar kwenda Kigoma".

Alifafanua kuwa jambo kubwa analokwenda kufanya Kigoma ni kuwaeleza wanachama wa Chadema sababu zilizomwondoa kwenye chama hicho na hatima yake kisiasa.

Zitto hakupatikana jana kuzungumzia ufadhili wake kwa Kafulila na taarifa iliyopatikana kutoka kwenye familia yake ilieleza kuwa yuko masomoni Ujerumani.

Alipoulizwa kuhusu magari hayo, mama wa mzazi Zitto, Shida Salum alisema kuwa Kafulila na Zitto ndio wanaostahili kuzungumzia suala hilo.

"Mimi siwezi kusema chochote, hawa ni marafiki nadhani wenyewe ndio wanaoweza kuzungumza zaidi," alisema.

Awali mmoja wa wanachama wa Chadema atakayekuwa katika ziara hiyo ambaye hakutaka kutajwa gazetini, alieleza kuwa msafara huo utakuwa na magari manane; matatu ya Zitto Kabwe na magari matano ya NCCR-Mageuzi

"Magari hayo yatabeba watu mbalimbali wakiwemo wanachama wa Chadema zaidi ya 50 ambao watatangulia kwa ajili ya kwenda kuandaa mazingira ya kumpokea Kafulila na msafara wake na katika maandamano maalum yaliyoandaliwa kwa ajili yake," alisema mwanachama huyo na kuongoza:

"Kimsingi Kigoma yote hakuna mwanachama wa Chadema aliyefurahishwa na kitendo kilichofanywa na viongozi wa chama hicho kuwaengua na wote wana hamu kubwa kumsikiliza Kafulila".

Alisema katika ziara hiyo, wanachama hao wanatarajia kurudisha kadi za Chadema na kujiunga rasmi na chama cha NCCR-Mageuzi.

Takribani wiki moja na nusu iliyopita, Dk Slaa alifuta nyadhifa za afisa habari wa chama hicho, David Kafulila pamoja na Afisa Mwandamizi wa Bunge na Halmashauri, Danda Juju na kuwa wanachama wa kawaida ambapo baada ya uamuzi huo, Kafulila na Juju kwa nyakati tofauti walitangaza kujiengua katika chama hicho huku Kafulila akijiunga na Chama cha NCCR-Mageuzi.

Kafulila na Juju walifutwa nyadhifa zao kwa madai kuwa walikuwa wakitoa habari za chama hicho kwa vyombo vya habari kinyume na taratibu, jambo ambalo walilipinga vikali na kudai kuwa walifanyiwa hivyo kwa kuwa walikuwa mstari wa mbele kuzungumza ukweli na kutetea haki kwa maslahi ya chama.

Habari hizo zilidai kuwa katika mazungumzo hayo, Dk Slaa alisema kitendo cha Mbowe kumtaka atekeleze agizo lake la kuwafuta uanachama Kafulila na Juju amemfanya aeleweke vibaya kwa watu wake wa karibu.

Habari zilifafanua kuwa Dk Slaa alimweleza Mbowe kuwa shughuli nyingi ndani ya chama hicho anazifanya kwa kujitolea na kwamba kama ni Ubunge angeweza kuupata hata kama angekuwa mwanachama wa chama kingine na kusisitiza kuwa anayoshutumiwa na watu kuhusu uamuzi wa kuwavua nyadhifa Kafulila na Juju aliujua kabla.

Tangu Juju na Kafulila watangaze kujitoa Chadema, Mbowe hajawahi kuzungumza lolote licha ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake ambazo zilipigiliwa msumali na Juju ambaye alidai kuwa kama Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali(CAG) atakikagua chama hicho na kukuta mambo shwari atakuwa tayari kwenda jela.

Habari zaidi zilieleza kuwa mara baada ya kikao hicho, Dk Slaa wakati anatoka alikutana mlangoni na Muasisi wa chama hicho na Gavana wa kwanza mzalendo Benki Kuu ya Tanzania, Edwin Mtei alimwomba wazungumze, lakini Dk Slaa alisisitiza kuwa ana safari ila baada ya kuombwa kwa muda mrefu na Mtei alikubali. Inadaiwa kuwa mazungumzo yao yalidumu kwa saa mbili.

Habari hizo zilieleza kuwa maofisa wawili wa juu wa chama hicho (majina tunayo) wako katika hatua za mwisho za kujivua uanachama na inadaiwa kuwa mmoja wao ameshaandika barua ya kujivua uanachama kwa madai kuwa mchango wake katika chama umekuwa hauthaminiwi na kwamba shughuli zake nyingi zimekuwa zikifanywa na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chama hicho, John Mnyika.

Mwananchi lilipomtafuta Dk Slaa kuzungumzia suala hilo, alisema kuwa chama hicho hakiwezi kukaa na kujadili masuala ya Kafulila na Juju kwa madai kuwa ni ya kipuuzi.

“Hivi wewe una cheti kweli cha uandishi wa habari. Nikuulize swali kwamba, hapo kwenu Mwananchi wamefukuzwa watu wangapi tena bila hata uongozi kujua mbona hamuandiki, Chadema tuna mambo mengi ya msingi ya kuzungumza hatuwezi kukaa na kujadili suala la Kafulila na Juju" alisema Dk Slaa na kuongeza:

"Maswali haya kuanzia leo iwe mwisho kuniuliza, sisi hatuwezi kukaa na kujadili upuuzi wa Kafulila na Juju, tena andika mwandishi wala usiogope; nasema ni upuuzi"

Dk Slaa alisema kuwa ndani ya Chadema mtu yeyote akifanya mambo kinyume na utaratibu lazima achukuliwe hatua kali za kinidhamu kwa kufuata katiba ya chama hicho. Alisisitiza kwamba, mambo yote yanayozungumzwa kuhusu chama hicho hayana msingi na yanatolewa na watu wasioipenda Chadema na wanaotaka kukiona chama hicho kikipoteza dira.


nina wasiwasi na habari zinazoandikwa sasa na Mwananchi inaelekea RA ameshawadakisha!
 
Zitto fatigue has set in here.

Zitto this, Zitto that, give me a break.

Who is Zitto? The Tanzanian Octomom?

Even Octomom took a break from the news.
 
Zitto fatigue has set in here.

Zitto this, Zitto that, give me a break.

Who is Zitto? The Tanzanian Octomom?

Even Octomom took a break from the news.

Ahahahahahahaaa...Zitto fatigue this quick? Aren't you the one who sort of co-signed on his potential? And now you claim Zitto fatigue? Well, you better brace yourself coz he's just getting started. He's not fitting to go away anytime soon.

To me Zitto is an attention ho and he savors the limelight he is in.
 
Ahahahahahahaaa...Zitto fatigue this quick? Aren't you the one who sort of co-signed on his potential? And now you claim Zitto fatigue? Well, you better brace yourself coz he's just getting started. He's not fitting to go away anytime soon.

To me Zitto is an attention ho and he savors the limelight he is in.

Co-signed his potential? Where? Could you kindly point me to the post?

Mimi nimeanza kumuua Zitto tangu hajawa celebrity politician.Nimemuua Zitto mara baada ya kuchaguliwa ubunge katika scandal lake la kwanza na marehemu Chifupa katika kuhesabu kura za uchaguzi wa Spika.

Wewe unaona mimi mtu wa kum cosign kirahisi rahisi mwanasiasa?
 
Co-signed his potential? Where? Could you kindly point me to the post?

Mimi nimeanza kumuua Zitto tangu hajawa celebrity politician.Nimemuua Zitto mara baada ya kuchaguliwa ubunge katika scandal lake la kwanza na marehemu Chifupa katika kuhesabu kura za uchaguzi wa Spika.

Wewe unaona mimi mtu wa kum cosign kirahisi rahisi mwanasiasa?

You did cosign on him. Bahati mbaya sina muda wa kupitia mada zote kukuonyesha ni wapi.
 
Co-signed his potential? Where? Could you kindly point me to the post?

Mimi nimeanza kumuua Zitto tangu hajawa celebrity politician.Nimemuua Zitto mara baada ya kuchaguliwa ubunge katika scandal lake la kwanza na marehemu Chifupa katika kuhesabu kura za uchaguzi wa Spika.

Wewe unaona mimi mtu wa kum cosign kirahisi rahisi mwanasiasa?

Watu tunaweza ingia machimboni kutafuta hizo dataz mzee, usibishe hapa aisee..labda kama umesahau
 
Kama huwezi kuthibitisha unapoteza credibility. Huwezi kuaminika.

You say whatever you want to say but I do remember you sort of cosigning. Specifically sikumbuki title ya thread lakini majadiliano yalikuwa ni ukigeugeu (flip-flopping) wa Zitto. Ipo hapa sehemu...wenye muda kama wakitaka wataifukua.
 
Kuna habari nyingine ambazo zinachochea migogoro zaidi. Kafulila ni mwanasiasa mchanga, nadhani hajui siasa ni nini. Kwa mwendo anaokwenda nao anaweza kujikuta anajimaliza mwenyewe bila kujua.

Tatizo ninaloliona, kijana anataka kuwa kwenye media akifikiri kwamba inampandisha chati, lakini ukweli ni kwamba media inamuongezea maadui badala ya kumjenga.

Ingekuwa ni busara angeenda huko Kigoma Kusini akasema na wananchi wa huko ambao ndiyo wapiga kura wake. Kuweka habari hizi kwenye magazeti ni kama vile anatumia jina la Zitto kuomba aungwe mkono na supporters wa CHADEMA jimboni. Pia in a way, ni kama anamchonganisha Zitto na CHADEMA.

Anaongelea kuchukua jimbo wakati serikali za mitaa viti 20 vimeenda CCM, na wao (CHADEMA + NCCR) walipata viti 23, je ana uhakika gani kwamba waliopigia kura CHADEMA na NCCR wote watampa kura yeye?

Hakutakiwa ku-reveal details za hiyo safari yake wala support anayoipata toka kwa Zitto. Pili, kutoa habari kama hiyo kunamfanya ajiweke kwenye mazingira ya utata kwa kuwa aligoma kurudisha kadi ya CHADEMA (kama taarifa hizo zilikuwa sahihi). Je, ana uhakika gani kwamba NCCR-Mageuzi watampa nafasi ya kugombea kwenye hilo jimbo? Asije akashangaa ikifika wakati wa uteuzi wakamtema kwa sababu nyepesi sana kwamba hawana imani naye.

Zitto, mshauri rafiki yako kwamba kwenye siasa na hasa kabla hujajenga jina unatakiwa kuwa makini sana. Jina linajengwa kuanzia jimboni kwako na siyo kuanzia kwenye magazeti. Wanaopiga kura ni wananchi wa jimboni, sio sisi wasoma magazeti. Hizo habari za kwenye magazeti zinatoa mwanya wa wapinzani wengine wanaonyemelea hilo jimbo kutafuta njia za kukumaliza kirahisi zaidi.

Atakuja kushangaa atakapokuja kujikuta jina lake limepigwa red na chama chake na wala asijue ilikuwaje. Kwani aliyegombea Ubunge 2005 kupitia NCCR amesema hataki tena kugombea?

Hizi siasa za kwenye magazeti tuwaachie wenyewe wanaojua, wengine naona tunazivamia tu bila kujua how to play the dirty game. Mimi sikumfahamu Zitto wala Mnyika kabla ya uchaguzi wa 2005, nimemfahamu Zitto baada ya kushinda na pia Mnyika nimemfahamu baada ya kuitikisa CCM jimboni Ubungo.

Kwa hiyo a good starting point ni sera zake huko jimboni kwake na siyo publicity kwenye magazeti. Atajimaliza kirahisi sana. Akomae na wapiga kura wa jimbo lake maana ndio watakaomchagua, sisi wengine ni wapiga domo tu.

Pia inahitaji understanding ya hali ya juu na ukomavu wa kisiasa CHADEMA kumwelewa Zitto kwamba hana nia ya kukihujumu chama chake. Pamoja na kwamba lengo ni kuimarisha upinzani, lakini ushirikiano wa dhati kati ya vyama vya upinzani haupo, wao wenyewe wanaonana kama maadui, lakini at personal level watu wanaweza kushirikiana lakini kwa njia za kimya kimya na siyo kuropoka magazetini kama jinsi dogo Kafulila anavyofanya.
 
Jamani watanzania tumefikisha kubaya na habari za tetesi zisizo na maoni ya side zote mbili. Nafikiri huyu mwandishi yupo kwenye pay roll ya kafulila ili ampambe na safari yake ya kwenda mwisho wa reli. Lakini yote kwa yote kama zitto anaurafiki na kafulila hayo ni mambo yao binafsi na kuazimishwa gari ni kitu personal sana, wangapi wanaazimishwa magari na rafiki zao na hawaandikwi kwenye magazeti? Jamani umefika wakati wa tumeme know kwenye upuuzi kama huu.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom