Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
  • Hii ni baada ya kusema “Nitafanya maamuzi ambayo hayajawahi kufikiriwa"
  • Chadema yaharisha damu!
  • CCM yapiga vigelele kama vile mwana kakutwa bikra kwenye harusi ya ndoa!
Dar Es Salaam, Tanzania.

Baada ya kusoma maelezo ya Mhe Zitto katika gazeti la Mwananchi la jana, ile network ya watafutaji wa habari za kweli na za kuaminika hapa Tanzania (yaani Wagagagigikoko) waliingia kazini na kuzungumza na Watanzania kadhaa mjini DSM na kwenye vitongoji vyake, ili kujua wanategemea Mhe Zitto atafanya maamuzi gani ambayo hayajawahi kufikiriwa.

“Mhe Zitto tayari keshajiunga na CCM na kadi keshapewa”, alisema mwananchi mmoja ambae hakutaka jina lake litajwe mpaka mwenyewe Mhe Zitto atamke hadharani. “Hizi ndio lugha zao, mwanasiasa akisema nitafanya kitu, basi ujue tayari keshafanya hicho kitu na Mhe Zitto ndio hivyo hivyo”, aliendelea mwananchi huyo.

Mwananchi mwengine ambae kajitambulisha kama ni mwanachama asilia wa Chadema alisema huku machozi yakimtoka kuwa, ” I say, sina hata nguvu. Huyu Mhe Zitto tukimtegemea atuokoe Watanzania katika hili janga la CCM, tukimuona yeye kama Obama wa kitanzania, lakini inaonesha na yeye ndio keshajiunga nao. Anyway, mimi tokea alivyomsifia yule Dr Rashid nilijua kama hapa lipo jungu linapikwa na naona sasa lishawiva”. Alipoulizwa kama kweli Mhe Zitto anaweza kujiunga na CCM baada ya shutuma zake zote zile nzito nzito dhidi ya CCM, huyu mwanachama wa Chadema alijibu kuwa,” Kwa mwanasiasa chochote kinawezekana”, alijibu na huku akikataa kujibu masuala zaidi.

Makachori wa Wagagagigikoko walimpigia simu mwanachama mmoja mashuhuri wa JF na kumuuliza anaona vipi hali ya opposition parties Bara, na yeye akajibu, “ Mhe Zitto ni mwanachama wa Chadema na madamu bado hajatamka kutoka Chadema, tafadhalini tuwaachieni akina Dr Slaa na Mbowe wayamalize wenyewe”, na huku akikata simu kama mtu aliyekasirika kwa kuulizwa suala hilo.

Mwanachama mmoja wa CCM alikutwa akipiga vigelegele na huku akigonga debe bovu kwa nyundo kama vile mwanawe wa kike kakutwa bikra katika harusi yake. Alipoulizwa anafurahia nini alijibu, ” Mimi ni CCM. CCM ndio baba na ndio mama yetu. Wakirejea CCM tutawalea kama watoto wetu na katu hatutowakataa, kwani mzee hamkatai mwanawe”.

Wagagagigikoko, wameendelea kusema kuwa political pundits wa mji wa DSM jana baada ya kusoma maelezo ya Mhe Zitto kwenye gazeti la Mwananchi, wengi walikuwa wakisikika wakisema hadharani kuwa kwa sasa hata kama Mhe Zitto atabakia Chadema, maafa (damage) tayari yashatokea na kutendeka and Chadema will never be the same again.

“Chadema itaendelea kuharisha damu mpaka Dr Slaa na Mbowe watakapo yakabili kijitukizima matatizo yaliyojitokeza. Bila ya hivyo, chama ambacho kilikuwa kikitegemewa na wengi to put up a productive opposition in the country will slowly and surely bleed to an ignominious death!”, walimalizia Wagagagigikoko.


Sources: Wagagagigikoko News Network (Wanene)
 
Hii si ndio wamarekani wanaita Shit ya Ng'ombe dume?
 
Zitto nilisha kushauri usijibu lolote acha kucheza na media hawa watakuharibia mambo yako.
 
Sisimizi: Braza Z, tugombee uenyeviti na sisi mwisho wa reli taifa lijue tuumo.
Z: Emama wacha! hilo wazo linaonesha kweli umeshiba mawese ya kwetu, mi nigombee uenyekiti Taifa, na wewe uenyekiti BAVICHA!

Wenye chama: Uenyekiti hauendi popote palle, wewe sito jitoe na wewe sisimisi japo umeshinda, yezu na malia hamna matokeo.

NAAM, HAPA NDIPO GOGORO LILIPOANZIA
 
>.....wengi walikuwa wakisikika wakisema hadharani kuwa kwa sasa hata kama Mhe Zitto atabakia Chadema, maafa (damage) tayari yashatokea na kutendeka and Chadema will never be the same again.

Kwa mara ya mwanzo Wagagagigikoko ninakubliana na nyinyi. Hii ni kweli tupu. Mkiwa mnasema ya ukweli kama hapo juu bila ya kujali kama nyinyi ni makada wa chama gani, basi thread zenu hazitokuenda na maji kama huko nyuma, kwasababu tupo hapa kufunguana macho na sio kurushiana michanga ya macho.

>"Chadema itaendelea kuharisha damu mpaka Dr Slaa na Mbowe watakapo yakabili kijitukizima matatizo yaliyojitokeza.

This is a good advice to Dr Slaa na Mbowe na siamini kama advice hii inatoka kwa Wagagagigikoko. Lazima hii hali ikabiliwe, kurushiana makombora baina ya wana-chadema haisaidia Chadema hata kidogo.

>Bila ya hivyo, chama ambacho kilikuwa kikitegemewa na wengi to put up a productive opposition in the country will slowly and surely bleed to an ignominious death!", walimalizia Wagagagigikoko.


This is definitely true pia. Wengi tuliona kuwa Chadema kitatuokoa, lakini ndio hivyo tena, inaonesha opposition Tanzania bado haijakuwa. In fact ikiwa hawawezi kuungana katika chaguzi ili wakashinda unategemea nini? Kila mmoja anaona atashinda yeye na yeye ndio atakuwa Rais. Hakuna mmoja anaefikiria kwamba waungane ili waiokoe nchi. Wao wanafikiria kujiokoa wao tu!
 
Historia ina tabia moja ya kujirudia. Kwa mbali nakumbuka ugomvi wa Kabourou na uongozi wa Chadema - mafisi walitokwa mate wakisema mkono wa binadamu hatimaye unadondoka, haukudondoka. Badala yake, Chadema ikachipuka upya na kushamiri na kijana mdogo Zitto akaukwaa ubunge tena kilaini kabisa. Likaja zogo la Wangwe na uongozi wa Chadema na safari hii manyang'au wakachekelea kweli kweli lakini wapi mkono wa binadamu bado haukudondoka na kijana mwingine wa Tarime, Mwera, kaurudisha ubunge maskani. Hivi sasa linafurukuta la Zitto na kama kawaida meza imetayarishwa na walafi wamekaa mkao wa kula kwamba safari hii Chadema inaangukia pua - jamani hivi siasa tunaielewa kweli ? Mate yatawadondoka kweli kweli kwani Zitto ataondoka, Dr. Slaa ataondoka na hata Mbowe ataondoka, lakini kama ulivyo mkono wa binadamu, Chadema itabaki pale pale - subirini !
 
huyu mjinga katoka wapi? Freeman alisoma kibaha secondary school na alipata division one halafu akaenda ihungo high school kuchukua pgm. Haya nayakumbuka kwa kuwa tulisoma wote
mjinga ni mbowe anayebaki demokrasia.
 
Dk. Slaa amvaa Zitto
• Asema CHADEMA ipo tayari kwa uamuzi wowote

na Tamali Vullu
Tanzania Daima


amka2.gif

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kipo tayari kupokea maamuzi yoyote yatakayotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, ya kuamua kujiuzulu nyadhifa zote katika chama hicho ama la.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, siku moja baada ya Zitto kukaririwa na vyombo vya habari jana kuwa amekuwa akiandaa barua ya kujiuzulu nyadhifa zote ndani ya chama hicho, ikiwamo na ya ubunge. Zitto pia alituma nakala ya maelezo hayo kwa gazeti hili.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema tangu Zitto aanze kunukuliwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa anamuunga mkono aliyekuwa Ofisa Habari wa chama hicho, David Kafulula, amekuwa kimya licha ya kumtumia barua pepe kutaka kufahamu ukweli juu ya suala hilo.
“Zilipotolewa taarifa hizo kwenye vyombo vya habari mama yake Zitto, Shida Salum, alieleza kuwa mwanawe hausiki kwa kuwa e-mail yake imekuwa ikiingiliwa na watu na kutuma ujumbe huo,” alisema.
Mama huyo pia aliwasilisha madai hayo katika kamati kuu iliyokutana Desemba 2 na kwamba kutokana na hali hiyo alilazimika kumtumia taarifa kwa barua pepe (e-mail) Zitto ili ampe ukweli wa suala hilo, lakini tangu wakati huo amekuwa kimya.
“Baada ya kutolewa kwa madai hayo na kuwasilishwa katika kamati kuu, Desemba 2, nilimtumia e-mail Zitto, lakini mpaka leo (jana) hajanijibu,” alisema Dk. Slaa.
Alisema kutokana na hali hiyo, ameanza kupata wasiwasi kuwa huenda mama huyo anadanganywa na mtoto wake huyo (Zitto).
Hata hivyo, alisema asipopata majibu kutoka kwa Zitto atajua kuwa maelezo hayo yana ukweli na kusema kwamba CHADEMA ni taasisi, haitayumba kwa kuondoka kwa mtu yeyote. “Wakati ule aliondoka Kabourou (Amani Walid Kabourou) na CHADEMA imeendelea kuwapo…anaweza kuondoka Freeman Mbowe na Dk. Slaa, lakini CHADEMA itabaki,” alisema.

Aidha, alisema suala hilo linakuzwa ili chama hicho kiachane na ajenda ya kupigania ufisadi nchini na kujikita katika mizozo ya aina hiyo.
“CHADEMA haitaacha kupiga vita ufisadi na ndiyo maana hivi karibuni tumetoa tamko la kuitaka serikali ijibu hoja kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa (UN) kuichafua Tanzania kuhusu kupeleka silaha kwa kundi la waaasi katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),” alisema Dk. Slaa.
Jana, Zitto alikaririwa na gazeti moja (si Tanzania Daima) kupita barua pepe akieleza kuchukizwa na siasa chafu zinazoendelea ndani ya chama hicho na kwamba yupo tayari kujivua nyadhifa zote ndani ya chama hicho ikiwamo ubunge. Mbunge huyo kijana, alikaririwa akieleza kuwa uamuzi wa kumfukuza Kafulila haukuwa wa haki na kwamba ataendelea kumuunga mkono kama atagombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR - Mageuzi na si mgombea wa CHADEMA. Hivi karibuni, chama hicho kilimtimua Kafulila na Danda Juju, ambao walikuwa wapambe wakuu wa Zitto katika uchaguzi mkuu wa chama hicho, akiwania nafasi ya uenyekiti wa taifa kabla ya kuamua kujitoa badaa ya vikao mbalimbali vya wazee wa chama hicho vilivyomsihi asigombee ili kutokigawa chama katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.
 
Vyama vyote vya Siasa Tanzania utapeli mtupu. CHADEMA baada ya kutupa matumaini Watanzania kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuibua ufisadi mbali mbali na hivyo kujenga matumaini kwamba labda wataibuka na viti vingi vya Bunge 2010, sasa wameanza kusambaratika na kukiachia Chama cha Mafisadi njia nyeupe ya kuzoa viti vingi vya Bunge 2010. Kweli Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kwa mtaji huu chama cha mafisadi kitabaki madarakani milele na kuendelea kuifisadi nchi yetu mpaka ifilisike kabisa. 🙁
 
Slaa again is making the very same mistake kucheza na magazeti,SLAA nini kimekupata, hivi huwezi kumwita Zitto mkakaa naye chini, mpaka useme na magazeti.Haya magazeti wanawaza kutumia tumbo.Cahdema mnaiua hivi hivi,

Huyu ndiye mlisema anafaa kuwa rais?????
 
Vyama vyote vya Siasa Tanzania utapeli mtupu. CHADEMA baada ya kutupa matumaini Watanzania kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuibua ufisadi mbali mbali na hivyo kujenga matumaini kwamba labda wataibuka na viti vingi vya Bunge 2010, sasa wameanza kusambaratika na kukiachia Chama cha Mafisadi njia nyeupe ya kuzoa viti vingi vya Bunge 2010. Kweli Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kwa mtaji huu chama cha mafisadi kitabaki madarakani milele na kuendelea kuifisadi nchi yetu mpaka ifilisike kabisa. 🙁

Kweli inahuzunisha sana, ukiangalia growith curve ya hivi vyama na rate yake inahuzunsiha sana.

Slaa anasema waliondoka akina Kaborou, hata yeye na Mbowe wakiondoka leo Chadema itakuwepo tu.

Sijajua kama ameevaluate ni kwa namna gani hii migogoro inaathiri upinzani wote na kuwajenga hawa mafisadi.Sijajua kama ni busara kamgogoro haka washindwe kutatua watu ambao tunaamini wanaweza kushika dola!

Kwa migogoro hii Slaa watu wanadharau Upinzani woote , sio chadema tu, wanachama wapya wanaogopa kuingia at its worse kwenye chaguzi watu hawapigi kura na tafiti zinaonyesha wasiopiga kura ni wengi na ndio wenye uwezo wa kubadilisha mambo.

Siamini kama Slaa amegeuka Makamba kiasi hiki, kingeathiri nini ukakaa kimya, mtafute huyo msaidizi wako (for God sake), mjadili muyamalize, pia angalia ni wapi umekosea wewe, you are mediator na kwa cheo chako ungefanyika msaada sana wa kuwaunganisha Mbowe na Zitto.Kinachoonekana hapa ni umechagua side na maamuzi mengi msaidizi wako aidha hayajui au unamruka!

Msiwafanya binadamu kama mbwa you can say and do anthing without reaction, hali kadhalika ama Zitto ana makosa naye asiwafanye nyie mbwa wa kuwafanya chcochote.we need you guys to resolve your issues which are stink right now,however, the authors of all these messy are known
 
Ala!! yaani yaani walitaka mwenyeviti wote watoke Kigoma? Ina maana hao Wachaga walikuja Dar kucheza ngoma? Eeh?? Wmfufue mwalimu wamwuuliza Ed. Mt. ni nani!!
 
Slaa again is making the very same mistake kucheza na magazeti,SLAA nini kimekupata, hivi huwezi kumwita Zitto mkakaa naye chini, mpaka useme na magazeti.Haya magazeti wanawaza kutumia tumbo.Cahdema mnaiua hivi hivi,

Huyu ndiye mlisema anafaa kuwa rais?????

Niliwaelezeni toka mwanzo kufichua ufisadi ni heri, lakini mwangilieni sana mtu anayepata umaarufu kwa kupitia mgongo wa fisadi.

Enzi zile nikatoa mfano.
ya kwamba Juma ana mke Neema ,juma kaenda kuzini na Agnes Musa kaja kamsaidia Neema kumshika ugoni Juma kwa kumpa taarifa mhimu na kwa kuwa Neema bado akili haijakaa sawa na hasira basi Musa anatumia mwanya huo kumshawishi Neema wafanye uzinzi na kweli Musa anafanikisha.
Lakini Musa alichomusshawishi nacho Neema ni kuwa eti yeye Musa ni mwema sana kwa maana amefanikisha ugoni huo, kwa hiyo kama Neema ana akili nzuri bora naye azini na Musa.

Tuwaangalieni sana wa namna hii japo sio wote.
 
Zitto nilisha kushauri usijibu lolote acha kucheza na media hawa watakuharibia mambo yako.

Unadhani anaweza kusimama? Atasimama je kama hayuko tayari kuongea na upande mwingine wa chama? Hili lingekwisha kama angekuwa tayari kama kiongozi wa chama kukutana na viongozi wenzake wakayaongea na kuyamaliza pembeni wakiwa na glass ya juisi na vipaja vya kuku!

Kama hawawezi hili, basi nadhani hakuna njia zaidi ya kila mtu kuchukua zake 50, ili watakaobaki waanze kujenga upya! Siamini kuwa jitahada za usuluhishi kuwa hazijafanyika, ila kinachoonekana wanasema kuwa sote ni vidume na tuuone mwisho wake! Hata Rashidi katika riwaya ya Kuli alisema haya yana Mwisho, ni kweli tungependa kuona mwisho wakati tunaishi, lkn ....

Katika hili tutaendelea kupata fundisho kubwa zaidi kuliko tulivyofahamu jana na juzi. Kweli chama cha siasa ni muuinganiko wa watu wenye nia na sera moja ili hatimaye kushika madaraka ya nchi!
Je, itatokea nini endapo tutakuwa na nia na sera tofauti ndani ya chama kimoja (hususan viongozi)? Utajaza!
 
Labda aje yeye mwenyewe Zitto hapa na asema mambo haya kuliko kubaki na kutazama mambo yote yanakwenda vipi
 
Ni wazi sasa kuwa Chadema kuna mgogolo tena mkubwa tu! Naomba badala ya kuendelea kuwashambulia hawa watu, Tutafute watu wenye ushawishi kwa pande zote mbili zinazogongana ndani ya Chadema waende wakawakalishe chini hawa jamaa wazungumze nao, Wazee wa Chadema ambao wanawaita kisima cha busara vipi mbona mnakaa kimya tu..? huku mkiangalia mambo yanakwenda namna hii..! Kitila na wengine mlioko humu ujumbe huu uwafikie..!
 
Yawezekana kuna ukweli katika taarifa hizi,
Mwnendo wa mheshimiwa kabwe na kauli zake za hadharani katika siku za karibuni zinaonyesha kuwa anamwelekeo wa kuwaacha wenzake katika chadema. Amekuwa akitumia gazeti za mwananchi kupeleka ujumbe kwa umma kwamba anataka kuhama. Hii ni maandalizi ya kisaikolojia kwa watu ili asije akalaumiwa na umma
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom