Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Na mie uvivu wangu umetoka wapi?

Mtoa post amewakilisha kilichoandikwa kwenye gazeti...not his idea..Sasa kwa vile ni Zitto mnataka isijadiliwe...mbona JK katoka kwenye gazeti anabembea tayari watu wana comment heavily...kwani JK hajajadiliwa huko nyuma?mbona hamsemi agenda zake zisitishwe?....lets be a little bit democratic...kama issue ya Zitto ilijadiliwa kabla si umredirect mtoa thread easily na sio kukashifu watu..pengine ilipojadiliwa alikuwa sio member wa JF....

Tuache jazba na utemi humu....nasi twaweza pia

tafuta forum yako bana hii ilishazungumzwa, we vipi?
Kafulila nini wewe?
 
Kwa habari iliyo andikwa kwenye gazeti la mwanahalisi toleo la leo (9/12/2009) kuhusu yaliyokuwa kwenye mawasiliano kati ya ( Zitto(chadema) na Denis(MWANANCHI)) ni wazi kuwa wanaofikiria kuwa Zitto bado ni mwana-Chadema basi hawajaona mbali.

Maamuzi mazito ya Mweshimiwa Zitto yaatakuwa yameisha fanyika. Tutegemee kumuona Zitto upande wa pili kwa Chadema.

Tutegemee Either kumuona CCM kiwa kada wa chama na karibu sana na Mweshimiwa Makamba au NCCR akiwa karibu na Mkuu Kafulila muda si mrefu.

Kila la kheri Mweshimiwa katika chama kipya, Chadema watakukumbuka kwa changamoto zako.

Chadema imalisheni chama na ikiwezekana chunguzeni wanachama wote kuona kama kweli ni wanachama wenu au ni wapinzani wenu. Malizeni matatizo yaliyopo sasa. Demokrasia bila nidhamu ni fujo(Kafulila)
 
Inaonekana thread yeyote inayomhusu Zitto ni 'upumbavu'' kwa baadhi ya watu hata hapa. Kama tunaweza kumkosoa na kuibua mapungufu ya Rais wa nchi, Zitto kawahonga ni nini kuzuia mijadala juu yake. Nilishaandika huko nyuma kuhusu tetesi za Zitto kununuliwa na akina Rostam. Haikuchukua muda hiyo thread ikafutwa ili wengine wasione. sasa naona watu wanaporomoshewa matusi kwa kuandika mambo yanayomhusu Zitto.Kulikoni? as a public figure he needs to be scrunized like others. kwa mfano, kwa nini tusimuulize Zitto hiyo account ya Braclays wameifunga kwa nini? huo utajiri wa haraka kaupata wapi? kuna tetesi alilipiwa nauli kwenda kuonana na Rostam Canada.Je anasemaje?
 
Slaa na Mbowe wameishiwa..wanaogopa vivuli vyao..shame on them
 

nimeiweka yote kutoka tz daima

Dk. Slaa amvaa Zitto
• Asema CHADEMA ipo tayari kwa uamuzi wowote

na Tamali Vullu




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kipo tayari kupokea maamuzi yoyote yatakayotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, ya kuamua kujiuzulu nyadhifa zote katika chama hicho ama la.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, siku moja baada ya Zitto kukaririwa na vyombo vya habari jana kuwa amekuwa akiandaa barua ya kujiuzulu nyadhifa zote ndani ya chama hicho, ikiwamo na ya ubunge. Zitto pia alituma nakala ya maelezo hayo kwa gazeti hili.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema tangu Zitto aanze kunukuliwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa anamuunga mkono aliyekuwa Ofisa Habari wa chama hicho, David Kafulula, amekuwa kimya licha ya kumtumia barua pepe kutaka kufahamu ukweli juu ya suala hilo.
"Zilipotolewa taarifa hizo kwenye vyombo vya habari mama yake Zitto, Shida Salum, alieleza kuwa mwanawe hausiki kwa kuwa e-mail yake imekuwa ikiingiliwa na watu na kutuma ujumbe huo," alisema.
Mama huyo pia aliwasilisha madai hayo katika kamati kuu iliyokutana Desemba 2 na kwamba kutokana na hali hiyo alilazimika kumtumia taarifa kwa barua pepe (e-mail) Zitto ili ampe ukweli wa suala hilo, lakini tangu wakati huo amekuwa kimya.
"Baada ya kutolewa kwa madai hayo na kuwasilishwa katika kamati kuu, Desemba 2, nilimtumia e-mail Zitto, lakini mpaka leo (jana) hajanijibu," alisema Dk. Slaa.
Alisema kutokana na hali hiyo, ameanza kupata wasiwasi kuwa huenda mama huyo anadanganywa na mtoto wake huyo (Zitto).
Hata hivyo, alisema asipopata majibu kutoka kwa Zitto atajua kuwa maelezo hayo yana ukweli na kusema kwamba CHADEMA ni taasisi, haitayumba kwa kuondoka kwa mtu yeyote. "Wakati ule aliondoka Kabourou (Amani Walid Kabourou) na CHADEMA imeendelea kuwapo…anaweza kuondoka Freeman Mbowe na Dk. Slaa, lakini CHADEMA itabaki," alisema.

Aidha, alisema suala hilo linakuzwa ili chama hicho kiachane na ajenda ya kupigania ufisadi nchini na kujikita katika mizozo ya aina hiyo.
"CHADEMA haitaacha kupiga vita ufisadi na ndiyo maana hivi karibuni tumetoa tamko la kuitaka serikali ijibu hoja kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa (UN) kuichafua Tanzania kuhusu kupeleka silaha kwa kundi la waaasi katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)," alisema Dk. Slaa.
Jana, Zitto alikaririwa na gazeti moja (si Tanzania Daima) kupita barua pepe akieleza kuchukizwa na siasa chafu zinazoendelea ndani ya chama hicho na kwamba yupo tayari kujivua nyadhifa zote ndani ya chama hicho ikiwamo ubunge. Mbunge huyo kijana, alikaririwa akieleza kuwa uamuzi wa kumfukuza Kafulila haukuwa wa haki na kwamba ataendelea kumuunga mkono kama atagombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR - Mageuzi na si mgombea wa CHADEMA. Hivi karibuni, chama hicho kilimtimua Kafulila na Danda Juju, ambao walikuwa wapambe wakuu wa Zitto katika uchaguzi mkuu wa chama hicho, akiwania nafasi ya uenyekiti wa taifa kabla ya kuamua kujitoa badaa ya vikao mbalimbali vya wazee wa chama hicho vilivyomsihi asigombee ili kutokigawa chama katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.

http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=11002
 
Dont argue with a fool, people might not notice the difference ---- sasa who is a fool kati yenu Slaa na Zitto??

Au ni wote wawili?
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kipo tayari kupokea maamuzi yoyote yatakayotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, ya kuamua kujiuzulu nyadhifa zote katika chama hicho ama la.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa

-Tanzania Daima

Zitto,
Kwa maana nyingine ni kuwa uongozi wa juu CHADEMA wanakuambia fungasha uondoke.

Dr. Slaa alishayaongea haya maneno kwenye vyombo vingine vya habari. Lakini naona kaona labda inaonekana kama ni uvumi tu wa vyombo vya habari vinavyoipinga CHADEMA.

Sasa kaamua kwenda kuyanena kwenye gazeti la Mbowe ili pasiwe na utata. Wenzako hawakutaki tena.

Ushauri wangu ni kuwa, usijibu lolote la kwenye vyombo vya habari mpaka wawasiliane na wewe wakifuata taratibu za kiofisi. Jaribu sana ku-avoid vyombo vya habari, watakutega huko. Good lucky.
 
Zitto,
Kwa maana nyingine ni kuwa uongozi wa juu CHADEMA wanakuambia fungasha uondoke.

Dr. Slaa alishayaongea haya maneno kwenye vyombo vingine vya habari. Lakini naona kaona labda inaonekana kama ni uvumi tu wa vyombo vya habari vinavyoipinga CHADEMA.

Sasa kaamua kwenda kuyanena kwenye gazeti la Mbowe ili pasiwe na utata. Wenzako hawakutaki tena.

Ushauri wangu ni kuwa, usijibu lolote la kwenye vyombo vya habari mpaka wawasiliane na wewe wakifuata taratibu za kiofisi. Jaribu sana ku-avoid vyombo vya habari, watakutega huko. Good lucky.

Mkuu this is very sad kwa upinzani, yaani mnapishana lugha ndani halafu mnajibizana mtaani... tena mbele ya watoto

CHADEMA! You have got to put your act together, enough is enough!!!

My advice kwenu, just give media a black-out, hata kwa hilo gazeti lenu!!
 
Mkuu this is very sad kwa upinzani, yaani mnapishana lugha ndani halafu mnajibizana mtaani... tena mbele ya watoto

CHADEMA! You have got to put your act together, enough is enough!!!

My advice kwenu, just give media a black-out, hata kwa hilo gazeti lenu!!


Let their asses be exposed so that we know them better ... what about that!!! Lol!!
 
Zitto,



....

Ushauri wangu ni kuwa, usijibu lolote la kwenye vyombo vya habari mpaka wawasiliane na wewe wakifuata taratibu za kiofisi. Jaribu sana ku-avoid vyombo vya habari, watakutega huko. Good lucky.

Bwa ha ha ha,
 
Kwa aliyoyasema Zitto toka porojo za Wangwe , uchaguzi wa Chadema na jinsi alivyokuwa anajibizana ovyo na kutoa siri za chama, kumtetea Idrisa, Dowans, kuchallenge maamuzi halali ya bosi wake Katibu mkuu wa chama tena hadharani, kutokuwa na uongozi wa pamoja, ubishi usio na maana, dharau kwa viongozi wenzake, kusema aliyoyasema kuhusu kafukulila na kuonyesha immaturity ya hali juu na kusahau kuwa organization will live longer than members na kwamba hakuna aliyejuu ya chama nk.. kamam ningekuwa Chadema ningekuwa nimemfuta kazi zamani sana.
 
Mbona sijakuelewa mkuu, au labda IQ yangu imepungua siku hizi!

Mmoja anatoka kigoma kusini, mwingine kigoma kaskazini, wa kusini aligombea uenyekiti wa vijana, aliposhinda badala ya kutanganzwa mshindi akaitwa sisimizi, wa kaskazini aligombea uenyekiti taifa, wazee wakamwambia achane fomu. huyu wa kusini na wa kaskazini ni marafiki damu damu, ni 'homeboys', wa kaskazini kaapa kumuunga mkono wa kusini kwa gharama yoyote ile. wa kusini kashatafuta hifadhi, wa kaskazini bado (kidichu) IZ T KILIA NAU?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom