Rutunga M

JF-Expert Member
Mar 16, 2009
1,769
1,382
Sirro.PNG

IGP Simon Sirro leo Agosti 2, 2021 akizungumza kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe


IGP Simon Sirro leo Agost 2,2021 amefanya mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amezungumza mbalimbali kuhusu kukamatwa na Mwenyekiti wa Chadema pamoja na vuguvugu la kutaka kufanya maandamano. Akiwa katika mkutano huo SIrro alisema yafuatayo:

“CHADEMA wanaona Mwenyekiti wao (Mbowe) ameonewa na wanasema hawezi kuwa hivyo wanamuona ni Malaika hawezi kufanya kosa”.

“Kabla ya Uchaguzi nilisema kuna Watu wamepanga kuhakikisha Uchaguzi haufanyiki, nilisema kuna baadhi ya Watu wamepanga kulipua visima vya mafuta na kufanya mauaji ya Viongozi na nilisema tutawakamata kabla hawajafanya hivyo”.

“Tuliwakamata kabla, hayo ya Mwenyekiti wao (Mbowe) sitaki kuzungumzia sana lipo Mahakama ila wajue yeye ni Binadamu kama Binadamu wengine na anaweza kufanya kosa tumempeleka Mahakamani tuache Mahakama itimize wajibu wake”.

“Kama kweli ni mkweli Mwenyekiti wao (Mbowe) na anamuamini Mungu waende wamuulize habari hiyo, kuna mambo unaweza kuyafanya kwamba ni siri lakini ndio mana Vyombo vya Habari vipo, niwaombe Watanzania wenzangu usilolijua ni kama usiku wa giza usiingie kwenye mtego ambao hujui aliyeutega ana jambo gani”.

“Waende wamuulize huyo Mtu tuliyempeleka Mahakamani (Mbowe) kwamba hili jambo unalijua na kama ni ukweli ana Dini yake na anamjua Yesu Kristo aende aaambiwe, tunamuonea kwa lipi?, tupate nini? Tuna ushahidi wa kutosha tuache Mahakama iamue, kafanya Yes hakufanya Yes lakini habari ya kikundi cha Watu kusema tunataka kuandamana wewe ni nani Bro!? hiyo nafasi hauna”.

Awaonya Wanaotaka kuandamana
“Niwaombe Watanzania tuache wale Watu wachache ambao wanataka kupambana na Serikali wapambane nayo labda wana sababu zake lakini Mtu wenye hekima na busara anielewe, lakini kikubwa kama wameandaa kwenda Canada au Marekani wajiandae ila hatuwezi kuruhusu Watu wachache wavuruge Nchi kwasababu wamekosa madaraka”.

“Habari ya kusema mnataka kuandamana mnavunja sheria na ukivunja sheria usilaumu Jeshi, ukivunja sheria umeingia kwenye uhalifu, Sirro hatokuacha na Polisi hawatokuacha na ndio maana wanafanya siasa kwa sababu amani na utulivu upo, Sisi hatufanyi Siasa”.

“Niwaombe Watanzania ambao wameambiwa mkusanyike kutoka Mara kutoka wapi sijui na muelewe Mahakamana ni kituo nyeti ni kama Kituo cha Polisi ukitaka kuvamia utakung’utwa kwa mujibu wa sheria sababu umetaka sasa kama kuna Mtu maisha yamemshinda aje ila asije kulalamika, hii kesi iko Mahakamani tuiachie Mahakama iamue”.
 
Sirro ufahamu kuwa sisi kama watu wenye akili zetu:

1. Tunajua kuwa mwenyekiti Mbowe mmembambikizia kesi
2. Tuko kwenye nafasi za kujua mnambambikizia kesi
3. Tunajua ni haki yetu kuja mahakamani
4. Tunakutaka ujue tutakuwapo mahakamani wala usitutishe
5. Tunakutaka umwogope Mungu wako kwani kushuhudia uongo huku ukilitaja jina lake bure, Mola anakataza
6. Tunakutaka uwashauri wenzio mtafute magereza zaidi ya kutuweka katika mamilioni yetu
7. Tunakutaka uziheshimu haki zetu
8. Tunakutaka uheshimu katiba

Ni hayo tu. Kwako kamanda.
 
Hii nchi wanakoipeleka siyo, kutoka kwenye siasa za hoja kwa hoja mpaka kwenye siasa za kuharibiana maisha, wanatengeneza visasi vitakavyokuja kuleta madhara kwa taifa inaweza isiwe leo wala kesho

Mwendazake ametuachia taifa la ovyo sana katuaribia nchi, hatukua na siasa za hivi na hata kama zilikuepo si kwa kiwango hiki.

Naona ule mkwara wa kuachia watu na kufuta kesi ilikua ni kusafishia njia mashekh wa uamusho
 
Tip muhimu ushahidi

" walishawishi baadhi ya vijana wetu Wenye mafunzo...." kwamba wapo vijana wa Jeshi wanaandaliwa ama,wameandaliwa watumike kutoa ushahidi dhidi mashitaka ugaidi!? Hivi kweli ugaidi unatafutwa kwa tochi? Hisia?

Kuna watu walipanga kuvuruga uchaguzi!?Tulishuhudia kampeni za CHADEMA za wazi wakichangishana cent na kushiriki ngazi nyingi mbali ya vizingiti!

" Hatuingilii ama kujihusisha na Mambo kisiasa..."Kwanini nguvu kubwa ya Jeshi la polisi inatumika kuvuruga makongamano ya CHADEMA kudai Katiba, mbali ya Mboye hata wajumbe wengine wamesafirishwa na kukaguliwa Kama watuhumiwa wa ugaida, wakiwa wamefugwa pingu na vitambaa usoni Gari pickup safari ndefu zaidi saa 10?

Nashauri Jeshi litumie busara, hekima na weledi, mnaharibu amani na umoja wa Watanzania kwa matumizi mabavu, hisia?
 
Mitandao ya kijamii imefurika matusi na kejeli baada ya IGP kutoa press akidai asiyeamini kwamba Mbowe ni Gaidi aende akamuulize. Amekwenda mbali zaid na kudai atakayethubutu kuandamana atapigwa tu.

Hi si ishara nzuri kwa mlinzi wa amani kugeukwa na anaowalinda, naamini Jeshi la Polisi linakila sababu yakujitafakari kuelekea kustaafu kwa huyu Mzee siro ambaye kwa namna yoyote ile awezi Tena kujisafisha.

Ikumbukwe aliyeeleza kwamba Mbowe amekamatwa kwa maelekezo ya Rais alikuwa ni RPC Mwanza na hakuna hatua zilizochukuliwa kupinga kauli hiyo si serikali Wala jeshi lenyewe.

Lakini baadaye tuliambiwa anatuhumiwa kutaka kuua viongozi ila hati ya mashtaka haisemi hivyo na hakuna kiongozi aliyetajwa alitaka kuuwawa.
 
Sirro afahamu kuwa sisi kama watu wenye akili zetu:

1. tunajua kuwa mwenyekiti Mbowe mmembambikizia kesi.
2. tuko kwenye nafasi za kujua mnambambikizia kesi...
IGP amesema kama unaona Mbowe kaonewa nenda kamuulize kama kweli yeye ni mkristu safi atakwambia.

nimeona IGP kaongea kwa kujiamini sana kuwa wanao ushahidi hivyo tusubiri mahakama. huna haja ya kutoka mishipa kwa sasa, Jambo usilo lijua nisawa na usiku wa giza. tusijiingize kwenye mitego ukaja kunasa halafu huna wa kumlaumu.

kwa sasa wacha Mbowe apambane na hali yake.
 
Jeshi la polisi nchini limetoa onyo kwa mtu au kikundi cha watu watakaojaribu kuhamasisha mikusanyiko isiyo rasmi au kuandamana kwa namna yoyote.

Julai 31 Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliwataka wanachama wote ndani na nje ya Mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza katika mahakama ya Kisutu siku ambayo kesi ya Mbowe itatajwa.

Akizungumza na wanahabari leo Jumatatu AgostI 2,2021 Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Sirro amesema tuhuma dhidi ya Mbowe na wenzake ziko chini ya mamlaka ya mahakama.

"Jeshi la polisi halitegemei mtu au kikundi cha watu kwa namna yoyote kutoa shinikizo kwa mamlaka ya mahakama au kwa mtuhumiwa Freeman Mbowe aachiwe au kupewa dhamana,"amesema Sirro.

"Jeshi la polisi linatoa onyo kwa mtu au kikundi cha watu kitakachojaribu kuhamasisha mikusanyiko isiyo rasmi au kuandamana au namna yoyote ile kutoa shinikizo lolote,"amesema.

Ameaema jeshi la polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vimejipanga vizuri na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watu hao.

"Kabla ya uchaguzi nilisema kuna watu wamejipanga kulipua vituo vya mafuta na kuua viongozi wa Serikali hao wanaaopanga kuleta vurugu wajue Mbowe ni binadamu tumempeleka mahakamani tuache mahakama ifanye kazi yake."

Sirro amewataka viongozi wa dini na taasisi nyingine ziache kusema Mbowe anaaonewa na badaala yake wasubiri mahakama iamue.

"Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, yeye kapelekwa mahakamani tusubiri maamuzi, mikoa iliyojipanga kufanya maandamano ni kuvunja sheria."
 
IGP amesema kama unaona Mbowe kaonewa nenda kamuulize kama kweli yeye ni mkristu safi atakwambia.

Nimeona IGP kaongea kwa kujiamini sana kuwa wanao ushahidi hivyo tusubiri mahakama. huna haja ya kutoka mishipa kwa sasa, Jambo usilo lijua nisawa na usiku wa giza. Tusijiingize kwenye mitego ukaja kunasa halafu huna wa kumlaumu.

Kwa sasa wacha Mbowe apambane na hali yake
 
Katibu Mkuu wa chadema Mnyika anapaswa achunge sana kauli zake za kuhamasisha maandamano yenye lengo la kuvunja amani ya nchi.

Asije akalilaumu Jeshi la Polisi endapo atachukuliwa hatua za kisheria.

Huwezi kuhamasisha maandamano ya kushinikiza mahakama itoe haki!! kitendo hiki ni uvunjaji wa sheria.

Mnyika na Mrema wawe makini sana, watanzania hatuko tayari kuona watu.wachache wanajaribu kuchokonoa amani ya nchi yetu, na tunaliomba Jeshi letu kamwe lisivumilie wala kuwachekea.
 
Back
Top Bottom