Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Sababu ni Dr. Slaa anaamini Kikwete alimuibia kura uchaguzi wa 2010 kwa hiyo bado ana beef naye.

Bifu gani wakati anawatambua wasaidizi wa Kikwete? Msikie anavyo-address kwenye video hapo chini. Anaanza kwa kusema "Mheshimiwa Makamu wa Rais". Kama hamtambui Kikwete kama Rais anamaanisha Rais yupi anaposema "Mheshimiwa Makamu wa Rais"?

 
Last edited by a moderator:
huyu pasco ndio Ulanga Ally/Ally Ulanga wa kule Wanabidii...
 
Nafikiri kuna tatizo hapo. Lakin Ukweli unasiama tena kwa sheria zenu wenyewe kuwa Kikwete ni Rais wa Tz mpaka 2015 na ataendelea hivyo kisheria . Kumpinga au hata kummicha kunana nae ni upungufu wa maadili na uvunjifu wa katiba ya nchi yenu siku zote kisheria rais anakuwa mmoja .

Kifungu gani cha sheria ama katiba ya JMT iliyokiukwa kwa Dr. Slaa kutosalimiana na Kikwete shehe.

Nina wasiwasi kwamba huenda unachanganya katiba ya JMT na ya Oman!!

Aliyekwenda kuhani msiba aliwajibika kuwafuata wafiwa pale walipo na kuwapa pole. Sasa kama hakufanya hivyo halafu washabiki maandazi mnakuwa wa kwanza kulalamika, mnakuwa hamueleweki kabisa mnachotafuta kwa Slaa, nadhani ni zaidi ya Salam.
 
Kwenye ili tusitake kumtetea dr slaa ukweli ni kwamba dr slaa amemnunia rais kikwete na sababu ni dr slaa anaamini alishinda urais ila amezulumiwa na rais kikwete,na mwanzoni alishawishi ukawa ni msimamo wa chadema lakini sasa ivi chadema wanamkubali rais kikwete.kwaiyo umebaki kuwa ni msimamo wa dr slaa. Nakwa ili asipoangalia litamuomdolea heshima na iman walio nayo watanzania kwake matokeo yake kupolomoka kisiasa. Aache chuki ajiandae kwa uchaguzi ujao kwa maana asije akaamishia chuki kwa viongozi wenzie wanaomkubali rais kikwete akaja kukivuluga chama


Hilo la kuporomoka kisiasa baadae sana, kama mlivyokuwa mnajinasibu kwamba chadema ni chama cha msimu. Mwaka mmoja tu baada ya uchaguzi hamli, hamlali mnaiwazia chadema, ni dhahiri kwamba hata hilo la kuporomoka ni ndoto zenu ambazo haziwezi kuwa kweli.
Dr. Slaa huyu huyu ndiye amezidi kukipa chama uhai hadi ccm na serikali yake hawalali. Wanapanga na kupangua namna ya kummaliza kisiasa lakini wapi.
 
"Mahali nilipopangiwa kukaa palikuwa kule nyuma na rais alikaa mbele, isingekuwa busara mimi kutoka huko nyuma kuja huku mbele just kusalimia!. Pia Dr. Slaa aliongezea ni kawaida rais akifika mahali huanza kwa kusalimia watu wawili watatu ndipo hukaa!.

Mbona jibu ulishapewa ? mbona mwatafuta chokochoko lakini?
 
Kwenye ili tusitake kumtetea dr slaa ukweli ni kwamba dr slaa amemnunia rais kikwete na sababu ni dr slaa anaamini alishinda urais ila amezulumiwa na rais kikwete,na mwanzoni alishawishi ukawa ni msimamo wa chadema lakini sasa ivi chadema wanamkubali rais kikwete.kwaiyo umebaki kuwa ni msimamo wa dr slaa. Nakwa ili asipoangalia litamuomdolea heshima na iman walio nayo watanzania kwake matokeo yake kupolomoka kisiasa. Aache chuki ajiandae kwa uchaguzi ujao kwa maana asije akaamishia chuki kwa viongozi wenzie wanaomkubali rais kikwete akaja kukivuluga chama

Ni vizuri kupima unachosema na hali ya kisiasa na kiuchumi ilivyo sasa hivi. Serikali ya M**re imefanya lipi kwa Watanzania ukilinganisha na orodha ya ahadi zilizotolewa? Fikiria kwanza•
 
Mkuu Pasco kuna kitu kinachoitwa itifaki...nina shaka km umecheck ratiba ya mazishi na mtiririko mzima wa matukio kwamba nani alistahili kusalimiana na nani na wakati gani...ndio kutofautiana kupo kiitikadi na kimuelekeo (nikimnukuu Hamad Rashid) ila nikiri hatujafikia kiwango hiki...Ni dhahiri km hawakusalimiana perhaps,itifaki ilipangwa hivyo,ama walisalimiana wakati umakini wako ukiwa kando,ama tention za msiba...
 
:A S-cry: nimelia sababu umekimbia mapoint yangu, nilitaka nikupigie siasa za chit chat. Bahati yako, ningekupiga KO.

Chit Chat wazima wanakusalimu.


Kongosho, unielewe usinielewe, you still one of my favs, you make me laugh most of the times.lol

BTW Chit Chat hawajambo?
 
Anaekutendea ubaya, mlipe wema...haya maneno yapo kwenye vitabu vya dini..slaa anamtendea ubaya kikwete na kikwete anamlipa wema.mwisho wa siku dr slaa ataishia kupata aibu.mi namshauri dokta wetu wa ukweli asiwe na mimsimamo mikali kama hii.upinzani si uadui ni kupingana kwa hoja lakini udugu unabaki palepale


mkuu sijakusoma vyema hapo, nani kamtendea mwenzake vibaya kati ya JK aliyepora ushindi wa wazi wa Dr.Slaa, kwangu mimi anayemtendea mema kwa ubaya alofanyiwa na mwenzake ni Dr. slaa kwa kutoingia barabarani kumuondoa huyu kibaraka magogoni.
 
Hapa sasa naona kuna makundi mawili, moja likisema inawezekana ni JK hataki kuonana na Slaa.

Na jingine ni kuwa Slaa bado hataki kuonana na JK.

Na tukirudi nyuma kwenye matukio hayo, "tukachanganya na zetu" basi inawezekana tukapata mweleko flani.

Kuna wanaodai kuwa JK angetaka kuonana na Dr Slaa, basi angeweza muda wowote hata kumwita kwasababu yeye ni Rais, jambo moja wanalosahau ni kwamba JK hawezi kumwita Slaa bila sababu hata kama yeye ni rais.

Na tunachotizama hapa si wao kuitana, rather ni kwanini hawasalimiani hata pale inapotokea nafasi ya kuweza kufanya hivyo?

Kwanza kuna issue ya bungeni kuhusu kumtambua Rais mara baada a uchaguzi mkuu, pia kuna kauli kadhaa wa kadha kuwa uchaguzi haukuwa huru na uchakachuaji ulikuwepo, hilo pekee linapelekea confusions, na speculations kama hizi.

Walikwenda ikulu kuonana na JK, Slaa hakwenda.Mtu yeyote anaweza kuwa na tafsiri yoyote isiyo rasmi kwasababu ofcourse hata Zitto hakwenda na pia kuna watakaodai haikuwa na ulazima yeye Slaa kwenda, na kwamba hilo hali constitute yeye kutokutaka kuonana na JK etc.

Sikubaliani na wale wanaodai kuwa JK ndiyo hataki kuonana na Slaa kwasababu ushahidi wa kimazingira hauonyeshi hivyo.

Mara zote ambazo hawakukutana, ni Slaa ndiye aliyemiss, kwa mfano ikulu na kwenye mazishi na bungeni.

Haya yote si kwamba nina uhakika kuwa mkwepaji hapa ni Slaa, maybe not, or maybe yes...

Its a matter of disscussion.

BTW mimi sina chama na hivyo msishangazwe na neutrality yangu na maswali ambayo simply ni yenye kuleta changamoto zaidi towards finding any truth, if any at all!lol
 
ni ngumu kufahamu nani anamkwepa mwenzake ila JK nae syo wakubeza? anavisasi kweli mnamkumbuka babu seya? kushinei
 
Kwanini kukutana na mbaya wako. je wewe waweza kaa meza na mke\mume mwenzio.
 
Henge, kati ya JK na Dr. nani kafiwa?. Nani alimfuata mwenzie kumpa pole pale Tabata?. Mgeni kafika kutoa pole, mfiwa katoka!.

Nani alijitoa na kwenda mpaka mazikoni kijijini?. Kosa la mtoa pole alitakiwa akifika mazikoni awatafute wafiwa awape pole au aende kwa mfiwa alipo atoe pole!. Yeye kwa vile ni mheshiniwa sana alipofika alikaa alipopangiwa akitegemea mfiwa ndio atoke alikokaa aende kubembelezea pole!.

pasco.
aliyefiwa ni mzee estelatus babake marehemu regia,
wengine ni wapiga kura wake japo kura zao zilichakachuliwa, wengine ni JF,
hoja yako yakulinganisha kati ya JK na Slaa nani kafiwa haina mashiko, mbona mbowe ndo mwenyekiti wa chama km alivyo JK? au JK ni Mkama?
 
Mimi mwenyewe nisingemsalimia Jk mana sitambui kama ni rais halali wa watanzania,najua vituo vingi ambavyo alichakachua matokeo mojawapo kituo nilichokuwa nasimamia mimi.
 
Mimi ninachokijua Raisi wa Nchi ni Kutumikia Walio Hai zaidi!! Ikiwa ni Pamoja na Kuwaandalia mipango bora ya Kuboresha Maisha yao!! Sasa Kitendo Chake Cha kufuatilia Msiba to the Dots sidhani Kama ni Good Idea!! Angeweza Kutuma mwakilishi!!
 
Back
Top Bottom