Kuna nafasi hazipaswi kufanyiwa majaribio,mojawapo ni ya Urais.
Kama alivyosema Mwalimu, urais sio nafasi ya mchezo, unapita mitaani na kuona namna wananchi wako walivyo hohehahe, unasoma magazeti na kuona namna watu wanavyoteketea na magonjwa yanayoweza kuzuilika, unaangalia kwenye runinga na kuona namna wananchi wa nchi nyingine zenye nafuu wanavyofaidika na ustawi wa nchi zao. Urais wa nchi masikini ni kazi ya wito
..
Japo bado wapo wabishi sugu wanaoendelea kuamini kuwa JK ni chaguo la Mungu na atapunguza kama sio kumaliza matatizo ya Tanzania, binafsi sioni dalili zozote za kunifanya niamini hivyo. Hakuna udhati kwenye dhamira za JK. Maisha bora kwa kila Mtanzania
..
Pia nilipomsikia JK akitamka bila uoga kuwa anawajua wala rushwa lakini anawapa muda wajirekebishe nikatambua wazi kuwa huyu jamaa hayuko serious na ahadi zake.
Rushwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo, sasa kwa kuwapa muda wala rushwa wajirekebishe inamaanisha kuwapa idhini wamalizie kula rushwa kabla hawajachukuliwa hatua.
Mwaka umepita sasa tangu JK atoe tamko hilo na hajatupa feedback iwapo hao wala rushwa wameshajirekebisha lakini haihitaji certificate ya uchumi kutambua kuwa nchi yetu inatafunwa vibaya mno.
Kasi, ari na nguvu mpya imeshaonekana: kwenye matumizi yanayozidi mapato. Utabiri wangu ni kuwa JK ataamua kutogombea 2010 baada ya kugundua kuwa urais sio jambo la majaribio. Hopefully,and good for him, atayemrithi atakuwa ni chaguo lake la sivyo atakuwa kiongozi wa kwanza TZ kwenda kunyea ndoo Segerea.