Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Nakumbushwa hapa kuwa sijagusia kupanda ghafla kwa gharama za vitu (MFUMUKO WA BEI) bila udhibiti maalumu, hilo sikutaka lakini niliye naye hapa anadai nigusie.

Vyakula, vinywaji n.k vimepanda bei mara dufu! Haya ndiyo maisha bora ambayo tuyatarajie muungwana?
 
Kwa kweli inasikitisha sana. Sasa yeye kama Rais asipowasikiliza watu na kuwaahidi kuwatatulia matatizo yao si ataonekana siyo mtu wa watu?
 
Kuna nafasi hazipaswi kufanyiwa majaribio,mojawapo ni ya Urais. Sijui kama JK alitafakari kwa makini kuangalia kama kweli ana uwezo wa kuongoza moja ya nchi masikini kabisa duniani. Kama alivyosema Mwalimu, urais sio nafasi ya mchezo, unapita mitaani na kuona namna wananchi wako walivyo hohehahe, unasoma magazeti na kuona namna watu wanavyoteketea na magonjwa yanayoweza kuzuilika, unaangalia kwenye runinga na kuona namna wananchi wa nchi nyingine zenye nafuu wanavyofaidika na ustawi wa nchi zao. Urais wa nchi masikini ni kazi ya wito, kazi inayohitaji ujinyime usingizi kutafakari namna gani utawakwamua unaowatumikia.

Japo bado wapo wabishi sugu wanaoendelea kuamini kuwa JK ni chaguo la Mungu na atapunguza kama sio kumaliza matatizo ya Tanzania, binafsi sioni dalili zozote za kunifanya niamini hivyo. Hakuna udhati kwenye dhamira za JK. Maisha bora kwa kila Mtanzania hayawezekani iwapo ndani ya mwaka mmoja wa utawala tayari kuna maskandali makubwa yanayoashiria ulaji e.g. sakata la Richmond. Pia nilipomsikia JK akitamka bila uoga kuwa anawajua wala rushwa lakini anawapa muda wajirekebishe nikatambua wazi kuwa huyu jamaa hayuko serious na ahadi zake.

Rushwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo, sasa kwa kuwapa muda wala rushwa wajirekebishe inamaanisha kuwapa idhini wamalizie kula rushwa kabla hawajachukuliwa hatua. Basi bora hatua zenyewe zingechukuliwa. Mwaka umepita sasa tangu JK atoe tamko hilo na hajatupa feedback iwapo hao wala rushwa wameshajirekebisha lakini haihitaji certificate ya uchumi kutambua kuwa nchi yetu inatafunwa vibaya mno.

Kasi, ari na nguvu mpya imeshaonekana: kwenye matumizi yanayozidi mapato. Utabiri wangu ni kuwa JK ataamua kutogomea 2010 baada ya kugundua kuwa urais sio jambo la majaribio. Hopefully,and good for him, atayemrithi atakuwa ni chaguo lake la sivyo atakuwa kiongozi wa kwanza TZ kwenda kunyea ndoo Segerea.
 
Tatizo sio wananchi kukimbilia kwa Rais bali tatizo ni watu walioteuliwa na Rais kutowajibika ipasavyo.Unadhani kama matatizo wilayani yangepata ufumbuzi kupitia kwa Mkuu wa Wilaya,hao wananchi wangekuwa vichaa hadi wamtegemee Rais awatafutie ufumbuzi?

Badala ya kulaumu wanaotoa lawama ni vema kujiuliza kwanini wanalaumu in the first place. People do not care who delivers the goods, DC, mwekezaji au Mungu. As long as watu wanapata wanachokihitaji, wao wanaridhika. Wasipokipata wataendelea kulalamika. Matatizo yanayoelekezwa kwa JK yasingeelekezwa kwake iwapo angeteua wawajibikaji ambao pindi wakiboronga wangewajibika kwake badala ya kuwaita tena kwa semina elekezi kila baada ya miezi miwili.

Kutaka wananchi wanyamaze ni kuwanyima haki yao ya kikatiba ya kupatiwa huduma bora na serikali waliyoiweka madarakani. Usipotimiza wajibu lazima utaandamwa, ndio maana timu ikiboronga anayebeba lawama zaidi na pengine kutimuliwa ni kocha/meneja. JK kama kocha wa timu iliyopanda daraja (kuingia Ikulu) alipaswa kununua wachezaji wa kuunda timu ya ushindi (kuchagua watendaji watakaowajibika kwa dhati). Timu inapofanya vibaya mashabiki (wananchi) wanamshikia bango, na hiyo ni haki yao.
 
Kama Mtume alivyo shushiwa maandiko matakatifu ndivyo pia sisi Watanzania Mungu ametuletea Mtume na Mwokozi wa Watanzania JK au mnasemaje ?
 
Mlalahoi,
Si wala rushwa tu. Je wale vigogo waliotajwa kushiriki katika biashara za madawa ya kulevya. Alipelekewa majina lakini kimya kimekuwa cha mshindo.
 
Mlalahoi,
Hilo dua lako naona umekosa pa kulielekeza. Yaani JK aachie hatamu za utamu thubutu! Nakuhakikishia hata 2015 kutakuwa na watu wanapendekeza abadilishe katiba ili aendelee tena.
Ninachoweza kubashiri hapa ni kuwa 2010 atakuja na maneno haya "nipeni tena miaka mitano niweze kumalizia kazi niliyoianzisha"
Wanaoweza kumfanya asigombee ni watoto wake ambao wanafika hapa jambo JF, Tafadhali mwelezeni Pops aitendee haki Tanzania kwa kuachia ngazi 2010. Kama ni hamu ya Urais si imeshaisha?
 
Ni wazi kuwa hii kazi ni kubwa mno kwa huyu ndugu yetu. Tumuombee tu angalau atupeleke kimiujizajiza hadi 2010
 
...na ndiyo maana watu wakiona hamna cha JK wala serikali kwa ujumla, pengine kwa hasira au kwa tafakari, utawasikia wakisema "heri ya mkoloni!"
 
bajeti ya mwaka ujao wa pesa TRILLION 5.2 ..hiyoo inakuja ,sijui hii deficit ya mwaka huu 1.3 trillion projected till june wamejumlishia huko???

wOrM nakupa 5!!!!!!!
 
sasa Rais afanye nini, mimi naona yuko njia panda! Asipoingilia kati watu wata muona hawajali na hatimizi ahadi zake, akiingilia kati wengine watasema anaingilia kazi za watu wengine na anaweza "kususiwa". Sasa kama ungekuwa wewe ndiyo Kikwete ungefanya nini?
 
sasa Rais afanye nini, mimi naona yuko njia panda! Asipoingilia kati watu wata muona hawajali na hatimizi ahadi zake, akiingilia kati wengine watasema anaingilia kazi za watu wengine na anaweza "kususiwa". Sasa kama ungekuwa wewe ndiyo Kikwete ungefanya nini?

Ngoja nijaribu kutoa tafsiri yangu fupi kuhusu kazi ya Rais:

Rais ni kiongozi wa nchi anayesimamia vyombo vyote vya serikali kulinda katiba ya nchi. Jukumu lake ni kutoa sera ya mwelekeo wa nchi kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa mujibu wa katiba; halafu, anateuwa wasaidizi wa kushughulikia utekelezaji wa sera hiyo huku yeye mweyewe akisimamia utekelezaji huo.
 
Tutaendelea kulaumu miaka nenda rudi iwapo mfumo wa utawala hautabadilika. Mfumo wa sasa Rais ni kila kitu. Wakuu wa Mikoa na Wilaya na pia Mameya(wenyeviti wa council) na Wakurugenzi hawana kazi zinazotokana na initiative zao. Kila siku wanapokea maelekzo kutoka Dar es Salaam.

Ni lazima tufikie wakati destiny ya maisha ya watu iwe kwa watu wenyewe. Serikali iweke sera, sheria nzuri na kuhakikishiwa ulinzi na usalama.

Tuwe na mfumo mpya wa utawala utakaotoa uhuru kwa mikoa kujipangia maendeleo kwa kuzingatia sera za kitaifa, malengo ya kitaifa na kulingana na rasilimali zilizopo katika mikoa hiyo. Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji ziwe huru pia kufanya mambo yanaihusu.

Tukifanya hilo tabia ya kumtegemea Rais kufanya kila kitu itakwisha.
 
Kuna wengi humu Jambo Forums walishangilia sana JK alipoibuka mshindi Dodoma. Mimi niliwaonya vikali kabla ya hata moshi mweupe kuonekana kikaoni Dodoma.

JK alipoanza vibaya sana kwa kutangaza baraza la mawaziri 60, nilitabiri kwamba kabla hajamaliza miaka 2 madarakani, kasi ya mfumuko wa bei itazidi 10% kwa mwaka. Nilitabiri vile kwamba kabla hajamaliza miaka 5 ya kwanza, tutafikia kasi ya mfumuko wa bei ya karibu 20% kwa mwaka.

Takwimu alizotoa Waziri wa Fedha wakati huu ni kwamba kasi ya mfumuko wa bei imeshafikia 7.3% (Ilikuwa 4.5% JK alipochukua nchi). Kasi ya kukua kwa pato la taifa ilikuwa 7.2% JK alipochukua nchi na tayari imeshuka hadi 5.8%. This 1.4% decline in GDP growth rate translates into a decline in the rate of growth of the national wealth by some 56bn/- each year.

Waziri Meghji anasingizia ukame na bei ya mafuta. That is rubbish! Mbona Kenya nao walipata ukame kama sisi na hawana mafuta yao wenyewe, na uchumi wao umezidi kuwa mzuri kipindi hiki?

Tutasingizia njaa na mafuta mpaka lini?

Augustine Moshi
 
Eti hakuna deficit, bado serikali inafanya kazi ndani ya bajeti iliyopitishwa Dodoma. Walichofanya ni reallocation tu. Tatizo letu kubwa hatusemi ukweli.
 
sote twajua kuwa rais hawezi kufanya yote ila yeye mwenyewe anajidai anaweza kufanya yote ili apate attention kutoka kwa watu/media na aijengee umaarufu.
hivi kama raisi anaweza kwenda kila msiba?
kila ziara ya nje lazoma yeye?
hata kuzindua barabara ni yeye?
ufunguzi wa GAME supermaket ni yeye?

mameya,wakuu wa mikoa, mawaziri wanafanya nini? Ni lazima wajisikie idle kwa kuwa hata shughuli ndogo tu (ufunguzi wa supermaket) anaenda raisi ndio maana kila jambo litokeapo watu hukmodolea macho yeye. Si kwa sababu tunamtwika shughuli zisizo zake, La ni yeye mwenyewe anarukia majukumu ambayo alipaswa awaachie viongozi wengine.

Kama raisi kikubwa ambacho angefanya ni "Ufuatiliaji wa majukumu ya wale aliowachagua wamuwakilishe" na si kupenda kutoka gazetini
 
Tutaendelea kulaumu miaka nenda rudi iwapo mfumo wa utawala hautabadilika. Mfumo wa sasa Rais ni kila kitu. Wakuu wa Mikoa na Wilaya na pia Mameya(wenyeviti wa council) na Wakurugenzi hawana kazi zinazotokana na initiative zao. Kila siku wanapokea maelekzo kutoka Dar es Salaam.

Ni lazima tufikie wakati destiny ya maisha ya watu iwe kwa watu wenyewe. Serikali iweke sera, sheria nzuri na kuhakikishiwa ulinzi na usalama.

Tuwe na mfumo mpya wa utawala utakaotoa uhuru kwa mikoa kujipangia maendeleo kwa kuzingatia sera za kitaifa, malengo ya kitaifa na kulingana na rasilimali zilizopo katika mikoa hiyo. Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji ziwe huru pia kufanya mambo yanaihusu.

Tukifanya hilo tabia ya kumtegemea Rais kufanya kila kitu itakwisha.


Utawala wa majimbo....lakini hapa ndo kazi kwelikweli maana mwenye nchi ataogopa kugawana madaraka na wengine..Hofu ya kupoteza umaarufu, kutojiamni na wala kutoamini aliowateua, ushamba, ulimbukeni, kutojua mipaka ya madaraka/majukumau..vyote vimo mumo humo..
 
Viongozi wa dini ni watu wa ajabu sana. Ndio walishawishi waumini wao kuwa JK ni chaguo la mungu! Hawakutaka kungalia sera wala uwezo wa mgombea.Matokeo yake wamewatumbukiza waumini wao katika umaskini wa kutisha.

Ni mafarisayo halisi, wamewatwisha mzigo waumini wao ambao wao hawausogelei. Wako kimya wakati waumini wao wanafukarishwa kugharimia anasa za viongozi.

BOT sasa si taasisi ya kitaalaamu, ni chombo cha propoganda.Hakika ni maisha duni kwa kila mtanzania.
 
Viongozi wa dini ni watu wa ajabu sana. Ndio walishawishi waumini wao kuwa JK ni chaguo la mungu! Hawakutaka kungalia sera wala uwezo wa mgombea.Matokeo yake wamewatumbukiza waumini wao katika umaskini wa kutisha.

Ni mafarisayo halisi, wamewatwisha mzigo waumini wao ambao wao hawausogelei. Wako kimya wakati waumini wao wanafukarishwa kugharimia anasa za viongozi.

BOT sasa si taasisi ya kitaalaamu, ni chombo cha propoganda.Hakika ni maisha duni kwa kila mtanzania.
 
Back
Top Bottom