Huyu aliyeelekeza magari ya serikali kupaki saa kumi na mbili ana maana gani?

Sasa kama muda wa kazi umekwisha na huna dharula yoyote ya kikazi kwanini usipaki gari la serikali.......kuna ugumu gani kulielewa hili......??

Hebu jenga kama ni gari lako....baadae ya muda wa kazi kuisha utamuachia tu dereva azurure nalo tu bila kuwa na sababu za msingi.......mimi sioni haja ya malalamiko ukizingatia hayo magari ndio yanayokamatwa kwenye mambo haramu
 
Yupo sahihi ingawa madereva wamecharuka, muda wa ofisi za serikali ukiondoa baadhi ya taasisi Kama Tra ni saa 9.30 na ulienda baada ya muda huo hawakupi huduma.
Kama gari linakuwa nje ya saa kumi na mbili linapaswa liwe na kibali maalumu.
Nafikiri angeoogezea hata kutumia siku za mapumziko kuwe.na kibali maalumu kudhibiti matumizi mabaya ikiwemo matumizi mabaya ya mafuta.
 
Nyie watoto mliomaliza kunywa maziwa ya mama majuzi tu, hamjui kuwa kupaki magari saa 12, ni kanuni ya matumizi wa hayo magari toka enzi ya mkoloni.
Isipokuwa kwa kazi maalum au kwa sababu maalum inayofahamika !
Wahenga tunaifahamu hiyo Amri !
 
Hivi kama jiji la dar ,mpaka gari limpeleke boss tegeta jioni na dereva kuja kulipaki Gongo la mboto anapoishi si saa tano usiku, na bado aamke saa kumi usiku.tuache uroboti wa sheria za zamani wakati Mama kafungua nchi masaa 24, hizo ni sheria enzi za nyerere.

Au boss asitoe huduma baada ya kazi akiwaza gari lake linatakiwa likapaki.😂😂huku tunasema wananchi wahudumiwe usiku na mchana huku gari zote za serikali zipaki saa 12 jioni. Futuhi.kila wizara na idara ina ma transport officers wawajibike kufuatiia matumizi ya magari ya umma yatumike kwa shughuli kusudiwa, kama kuna dereva mtovu awajibishwe siyo kutoa tamko la jumla
Serikali ina masaa ya kazi Acha hizo .Muda wa kazi ukiisha nenda kwenu au kalale na gari kapaki
 
Leo imetolewa hoja kwamba magari ya serikali yapaki saa kumi na mbili. Unajiuliza hawa watu wanapotoa haya matamko wanashindwaga nini kufanya tathimini?

Nchi hii inawaza kuendesha shughuli zake masaa ishirini na nne; Mama anawaza kuona soko la Kariakoo linafanya kazi masaa ishirini na nne kuendana na ratiba ya vyombo vya usafiri.

Tunaelewa kwamba kadri muda wakutoa huduma unavyoongezeka ndivyo serikali inapanua muda wa usimamizi. Leo walevi kipaki magari bar imekuwa ni agenda inayopelekea mteule wa Rais kusema magari yapaki saa kumi na mbili?

Huyu Mbunge aliyetoa hoja alishindwa kupiga picha gari husika akamtumia waziri Dreva au bosi akawajibishwa tukasonga mbele?

Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.

Mnapotoa matamko na makatazo someni sera ya nchi kwanza. Mimi ningesema tumelipokea na tutalifanyia kazi then you go back to the office and communicate.

Ulaya nidhamu imejengwa kwenye uwajibishaji wa watovu wa nidhamu. Tuangaike na tatizo na siyo kufanya vitu jumla.

Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?
Tuambie nani huyo na kasema hayo wapi
 
Leo imetolewa hoja kwamba magari ya serikali yapaki saa kumi na mbili. Unajiuliza hawa watu wanapotoa haya matamko wanashindwaga nini kufanya tathimini?

Nchi hii inawaza kuendesha shughuli zake masaa ishirini na nne; Mama anawaza kuona soko la Kariakoo linafanya kazi masaa ishirini na nne kuendana na ratiba ya vyombo vya usafiri.

Tunaelewa kwamba kadri muda wakutoa huduma unavyoongezeka ndivyo serikali inapanua muda wa usimamizi. Leo walevi kipaki magari bar imekuwa ni agenda inayopelekea mteule wa Rais kusema magari yapaki saa kumi na mbili?

Huyu Mbunge aliyetoa hoja alishindwa kupiga picha gari husika akamtumia waziri Dreva au bosi akawajibishwa tukasonga mbele?

Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.

Mnapotoa matamko na makatazo someni sera ya nchi kwanza. Mimi ningesema tumelipokea na tutalifanyia kazi then you go back to the office and communicate.

Ulaya nidhamu imejengwa kwenye uwajibishaji wa watovu wa nidhamu. Tuangaike na tatizo na siyo kufanya vitu jumla.

Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?
Kwahyo wakuache utumie hadi usiku ili uendelee kubebea mikaa na abiria
 
Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.
Usipanic, hii nchi ni matamko tu hakuna utekelezaji
 
Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?
Yes, utahojiwa unaenda wapi saa hii na gari la serikali kama kuna kazi maalum itajulikana tu, tena ilitakiwa hiyo kazi ya kukamata hayo magari baada ya saa za kazi wapewe polisi wa doria, askari anapoona gari la serikali mahali ambapo sio sahihi awe na uhalali wa kuhoji, dereva akishindwa kutoa maelezo gari linaperekwa kituoni.
 
Yes, utahojiwa unaenda wapi saa hii na gari la serikali kama kuna kazi maalum itajulikana tu, tena ilitakiwa hiyo kazi ya kukamata hayo magari baada ya saa za kazi wapewe polisi wa doria, askari anapoona gari la serikali mahali ambapo sio sahihi awe na uhalali wa kuhoji, dereva akishindwa kutoa maelezo gari linaperekwa kituoni.
Kwani gari ya serikali unaloliongelea ni ipi? Make naona unaondoa gari ya polisi kwenye list ya magari ya serikali. Inaonekana mtoa mada hajaeleweka vizuri.
Mtoa mada yeye shida yake ni huyo Mbunge kutoa kauli jumuishi kwa magari ya serikali bila kuangalia kuwa kuna magari mengine yanafanya kazi katika mazingira yanayosababisha masaa ya usiku yafike kabla hawajafika sehemu yao ya kupaki magari.
 
Watakachofanya sasa watakuwa wanabandua namba za serikali wanaweka za kiraia na bata wanakula mpk asubuhi na hakuna kitu mnacheweza kuwafanya
 
Kuna mdau alishauri magari yote ya Serikali yawekwe alama kuonyesha taasisi husika. Nakubaliana na wazo la mdau maana kuna baadhi ya taasisi za Serikali inaonyesha zina usimamizi mbovu sana wa magari yake. Unakuta gari imepaki bar usiku dereva na wapambe wake wanapiga vilevi tu.
Kenya wana sheria kari sana za Magari ya Serikali na nahisi yote yana GPS hivyo yanafuatiliwa, Tanzania gari la Serikali ni mali ya Dereva
 
Tanzania wajinga ni wengi hivyo hawawezi kuwajibishana.Anayetakiwa kuwajibisha naye anafanya mambo yale yale anayofanya anayetakiwa kuwajibishwa.Unakuta kitu bila aibu limebeba nyasi za ng'ombe mchana kweupe but nobody cares.polisi wanaona,ras yupo na dada wake yupo.ukimwona RPC ni kama DC,ras,das,nk
 
Leo imetolewa hoja kwamba magari ya serikali yapaki saa kumi na mbili. Unajiuliza hawa watu wanapotoa haya matamko wanashindwaga nini kufanya tathimini?

Nchi hii inawaza kuendesha shughuli zake masaa ishirini na nne; Mama anawaza kuona soko la Kariakoo linafanya kazi masaa ishirini na nne kuendana na ratiba ya vyombo vya usafiri.

Tunaelewa kwamba kadri muda wakutoa huduma unavyoongezeka ndivyo serikali inapanua muda wa usimamizi. Leo walevi kipaki magari bar imekuwa ni agenda inayopelekea mteule wa Rais kusema magari yapaki saa kumi na mbili?

Huyu Mbunge aliyetoa hoja alishindwa kupiga picha gari husika akamtumia waziri Dreva au bosi akawajibishwa tukasonga mbele?

Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.

Mnapotoa matamko na makatazo someni sera ya nchi kwanza. Mimi ningesema tumelipokea na tutalifanyia kazi then you go back to the office and communicate.

Ulaya nidhamu imejengwa kwenye uwajibishaji wa watovu wa nidhamu. Tuangaike na tatizo na siyo kufanya vitu jumla.

Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?
Hapo wameipu tatizo la wizi wa mafuta kwa sababu dereva hatakubali kuliacha gari lina dizeli wakati wanapewa na serikal
 
Hivi najiuliza hii nchi kuna shida gani? Majuzi tu naona mkwara kuwa magari ya serikali baada ya saa 12 jioni hayaruhusiwi kuwepo nje. Cha kushangaza, madereva kama kawaida wapo wanakula nayo bata na hawaogopi.

Alafu ghafla unaona tena eti serikali inaagiza magari mengine ya sijui wakuu wa wilaya blah blah. Hivi mpaka watanzania wafanye nini ndio hawa wezi waelewe watu wamechoka na mambo ya hovyo?
 
Siku utakapomkuta Dereva wa Serikali ameegesha gari kwenye eneo la starehe kwa muda ambao unakatazwa nakushauri jiridhishe kwa nini yupo maeneo hayo kwa wakati huo naamini utapata jibu zuri la swali lako.Pia ni vizuri ukafahamu kwamba baadhi ya Watumishi wa Umma wanawajibika kufutilia sehemu za starehe kwa wakati wanaona ni sahihi ili kutimiza wajibu wao.

Aidha, kuna baadhi ya Watumishi ambao huwa wanakuwa safarini mbali na vituo vyao vya kazi na kulazimika kupitia maeneo haya kwa ajili ya kupata chakula hasa nyakati ambazo migahawa ya kawaida huwa imefungwa.
 
Back
Top Bottom