Hivi udini wa Samia Suluhu uko wapi? Tuzungumze ukweli

Hivi udini wa Samia Suluhu uko wapi? Tuzungumze ukweli

Humu jukwaa kuna tuhuma ambazo Samia Suluhu anatupiwa ya kwamba ni mdini na amejaza waislamu katika wateule wake sasa najiuliza udini wa Samia uko wapi? Au udini wa Samia anaufanyia wapi?

Mbona nikiangalia kati wateule wake kati ya wakristo na Waislamu naona wakristo ni wengi sana kwa maana kuna idadi kubwa ya wakristo Kati wateule wake kuliko waislamu?

Je, udini wa Samia uko wapi? Na mbona kiongozi akiwa muislamu hizi kelele za udini ni nyingi sana kuliko akiwa wa dini nyingine?

Mimi nauliza tu wala sina maana mbaya uzi uachwe.
Swali lako lingekuwa na maana kama ungeuliza hivi uislaam wa Samia uko wapi?? ni kile kilemba au eneo analotoka? Mpaka mashekhe wengi wafikie kusimama na kumtetea? Kwataalifa yako kwenye udini watu walishatoka huko waislam wanaemtetea ni mashekhe tu na kwa maslahi yao.
 
Siku ukielewa maana ya STRATEGIC PLANNING hutakuja Tena kuuliza swali kama hili.
 
Awamu ya kwanza ya Samia, tatizo siyo wafuatiliaji,kuna askofu akadhihaki ushungi kuwa rais anakua kama muuza vitumbua,akapewa na jina bi ushungi
Haya yote ni maoni yako. Weka ushahidi.
Kuhusu ushungi. Nilitegemea muwe proud hata akiambiwa ni Bi ushungi. Maana ni kweli anavaa ushungi. Kwani hamtaki tusema anavaa? Na kuna shida gani akiambiwa kavaa ushungi au akiitwa Bi Ushungi?
 
Mkuu, unaweza kuleta uthibitisho wa hao wanaosema ni mdini?

Au na wewe ni miongoni watanzania wajinga wachache wanaotaka viongozi watetewe kutokana na dini zao, naona kama kuna ajenda unaisukuma.

Binafsi sijawahi kuona mtu anasema huyo kiongozi ni mdini bali nimewahi kuona wajinga wachache wanaotaka tutetee maovu kwasababu kiongozi aliyepo anatoka katika dini yetu.
Mfuatilie mtu anayeitwa Lwiva
 
Mtu mwenye hofu ya Mungu na mshika dini asingeruhusu watu wauliwe kinyama na baadhi miili yao kuzikwa kwenye makaburi ya halaiki…

Hivi nyie Waislamu mnaomtetea kwa vigezo vya dini, ndio dini inavyosema hivi?

Uislamu unasemaje kuhusu kusitiri miili ya watu waliotangulia mbele ya haki?

Wanatakiwa kulundikwa kwenye stretchers kama digidigi?
Wapi nimemtetea chizi wewe mimi nimeuliza
 
Kwanza hongera kwa swali hili, pili jf ya sasa imebadilika sana, mtu unatoa hoja, badala ya watu kujibu hoja kwa hoja au kwa hoja mbadala, watu wanajibu hoja kwa viroja!.

Kwenye hizi hoja za Udini, Tanzania tuna tatizo la mazoea ya kitu kinachoitwa Mfumo Kristu, unaoshikiliwa na Kanisa Katoliki Tanzania kupitia TEC, ambapo it's is systematic rais wa Tanzania akiwa Mkristo, ni lazima awe Mkatoliki!. Hii haijaandikwa popote ila ndio hivyo!. Juliasi ni Mkatoliki, Benyamin ni Mkatoliki, Yohana ni Mkatoliki, anayefuata ni Emanueli!.

Hii imewafanya Wakatoliki kujisikia kuwa na an upper hand kwenye utawala wa nchi hii!.

Kwa sababu pia ni ukweli usiofichika, idadi ya wasomi Wakristo ni kubwa zaidi ya wasomi Waislamu, automatically kwenye teuzi nyingi lazima kutajaa Wakristo, hii ikapelekea Wakristo kujiona wao ni deserving kutawala idadi ya teuzi zote.

Tuhuma za Udini zikaanzia kwa Mwalimu Nyerere kuwa amejaza Wakatoliki kwenye serikali yake, Waislamu wakaanza kuita ni Mfumo Kristo, Father Sivalon ameandika kitabu kuhusu Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania.

Wakati wa Nyerere, kuwapata Waislamu wenye sifa za kuteuliwa ilikuwa ni wa kutafuta kwa tochi.

Mfano Benki Kuu ya Tanzania, ilihitaji kuwa na Naibu kutoka Zanzibar, sifa ni awe na Ph.D ya uchumi +10 years experience post Ph.D, mtu huyo hakuwapo, hivyo wa kwanza kupatikana ni enzi za JK.

Tanzania tuna ma CDF 8, kati ya hao mwenye jina la Kiislamu ni mmoja tuu, Abdullah Twalipo tena usikute ni jina tuu kama Jaji Mkuu Saidi au Jaji Ramadhani, majina ya Kiislamu, wenyewe Wakristo.

Samia akiteua CDF Muislamu sasa hivi utasikia kelele jeshini!, hii ndio mara ya kwanza Mnadhimu Mkuu ni kutoka Zanzibar!, kelele!.

Hakuna rais alukuwa na mkabila, mdini na nepotism kama JPM, kwa vile alikuwa Mkatoliki, hakuna kelele, sio tuu aliteua kabila lake tuu, ndugu zake, rafiki zake hadi something zake!, watu kimya.

Samia kateua tuu mtoto na mkwe, kelele!. Kiukweli Samia hana udini wowote, tatizo ni
1. Ni Mwanamke
2. Muislamu
3. Mzazibari mwenye nywele za singa

Enzi za Mwinyi hakukuwa na kelele hivi, hivyo huyu Mama wanamuonea tuu kwa uanamke wake!, dini yake na asili yake.

Tusiruhusu

P
Enzi za mwinyi palikua na kelele,sema hapakua na internet
Kwa nyerere waislam wa kushika wizara ya mambo ya ndani walikuwepo,ila wa kushika wizara ya elimu hata unaibu hawakuwepo
Nyerere alishutumiwa kwa ukatoliki, hapakua na wakristo wasomi madhehebu mengine ya kikristo au ndiyo alikua akisimika mfumo katoliki na sasa wanataka kumlipa kwa kumpa utakatifu?
 
Haya yote ni maoni yako. Weka ushahidi.
Kuhusu ushungi. Nilitegemea muwe proud hata akiambiwa ni Bi ushungi. Maana ni kweli anavaa ushungi. Kwani hamtaki tusema anavaa? Na kuna shida gani akiambiwa kavaa ushungi au akiitwa Bi Ushungi?
Bi ushungi,vibaraghashia,kobazi..hayasemwi haya kwa upendo bali kinyume chake
 
Litajibu vipi? Nyerere aliteua viongozi wengi wa kikristu lakini kwa matendo yake hakuwa mdini. Kama unadhani proportions hizo zitasaidia kwa nini usizilete wewe ili ujihakikishie kuwa ziko sahihi? Huu ni mjadala wa kipuuzi.

Amandla...
Nyerere alikua mdini kwa matendo,na ndiye mfumaji mkuu wa udini tz
Rejea kuvunja eamws alivyoingia ground mwenyewe,kuhodhi wizara ya elimu wakristo bila kuteua waziri muislam wizara hiyo kwa robo Karne aliyotawala Ili asimike ukatoliki serikalini
 
Kwanza hongera kwa swali hili, pili jf ya sasa imebadilika sana, mtu unatoa hoja, badala ya watu kujibu hoja kwa hoja au kwa hoja mbadala, watu wanajibu hoja kwa viroja!.

Kwenye hizi hoja za Udini, Tanzania tuna tatizo la mazoea ya kitu kinachoitwa Mfumo Kristu, unaoshikiliwa na Kanisa Katoliki Tanzania kupitia TEC, ambapo it's is systematic rais wa Tanzania akiwa Mkristo, ni lazima awe Mkatoliki!. Hii haijaandikwa popote ila ndio hivyo!. Juliasi ni Mkatoliki, Benyamin ni Mkatoliki, Yohana ni Mkatoliki, anayefuata ni Emanueli!.

Hii imewafanya Wakatoliki kujisikia kuwa na an upper hand kwenye utawala wa nchi hii!.

Kwa sababu pia ni ukweli usiofichika, idadi ya wasomi Wakristo ni kubwa zaidi ya wasomi Waislamu, automatically kwenye teuzi nyingi lazima kutajaa Wakristo, hii ikapelekea Wakristo kujiona wao ni deserving kutawala idadi ya teuzi zote.

Tuhuma za Udini zikaanzia kwa Mwalimu Nyerere kuwa amejaza Wakatoliki kwenye serikali yake, Waislamu wakaanza kuita ni Mfumo Kristo, Father Sivalon ameandika kitabu kuhusu Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania.

Wakati wa Nyerere, kuwapata Waislamu wenye sifa za kuteuliwa ilikuwa ni wa kutafuta kwa tochi.

Mfano Benki Kuu ya Tanzania, ilihitaji kuwa na Naibu kutoka Zanzibar, sifa ni awe na Ph.D ya uchumi +10 years experience post Ph.D, mtu huyo hakuwapo, hivyo wa kwanza kupatikana ni enzi za JK.

Tanzania tuna ma CDF 8, kati ya hao mwenye jina la Kiislamu ni mmoja tuu, Abdullah Twalipo tena usikute ni jina tuu kama Jaji Mkuu Saidi au Jaji Ramadhani, majina ya Kiislamu, wenyewe Wakristo.

Samia akiteua CDF Muislamu sasa hivi utasikia kelele jeshini!, hii ndio mara ya kwanza Mnadhimu Mkuu ni kutoka Zanzibar!, kelele!.

Hakuna rais alukuwa na mkabila, mdini na nepotism kama JPM, kwa vile alikuwa Mkatoliki, hakuna kelele, sio tuu aliteua kabila lake tuu, ndugu zake, rafiki zake hadi something zake!, watu kimya.

Samia kateua tuu mtoto na mkwe, kelele!. Kiukweli Samia hana udini wowote, tatizo ni
1. Ni Mwanamke
2. Muislamu
3. Mzazibari mwenye nywele za singa

Enzi za Mwinyi hakukuwa na kelele hivi, hivyo huyu Mama wanamuonea tuu kwa uanamke wake!, dini yake na asili yake.

Tusiruhusu

P
Wee Mzee P Pa1 na kuwa chawa au kiroboto ila bado hauuziki na hauhitajiki kwao. Hujistukiii? Hujishangaiii??

Acha kujipendekeza, hawakutakiiiiii.
 
Enzi za mwinyi palikua na kelele,sema hapakua na internet
Ndio palikuwa na kelele. Kelele hizo zilichangiwa na baadhi ya watu kutamba kuwa ni wakati wa waislamu.
Kwa nyerere waislam wa kushika wizara ya mambo ya ndani walikuwepo,ila wa kushika wizara ya elimu hata unaibu hawakuwepo
Kwako wewe wizara ya mambo ya ndani sio wizara? Na huyo mkatoliki Nyerere ndie aliyetaifisha shule za taasisi za kidini ambazo nyingi mno zilikuwa za kikristu. Shule za kiismailia zikitaifishwa lakini waliachiwa hosteli zao.
Nyerere alishutumiwa kwa ukatoliki, hapakua na wakristo wasomi madhehebu mengine ya kikristo au ndiyo alikua akisimika mfumo katoliki na sasa wanataka kumlipa kwa kumpa utakatifu?
Sema anashutumiwa, sio alishutumiwa. Wakati wake hakuna aliona hayo ya Vatican. Hakuna mkristu alikuwa na tatizo nae kwa sababu ni mkatoliki. Hata Kambona hakuwahi kuzungumzia hilo la Vatican. Ni nyie ndio mnalizusha.

Amandla...
 
Back
Top Bottom