Uongozi mbovu unaupimaje?..mlifungiwa kufanya mikutano ya kisiasa,akawaruhusu kufanya mikutano na maandamano,alikuta mna kesi za kubumba akazifuta,
Mikopo elimu ya juu hadi diploma
Alikuta hakuna ruzuku ya pembejeo,akaweka
Alikuta hakuna kuajiri,akaajiri,akapandisha madaraja na mishahara
Kajenga shule na hospital za kutosha na kutia ruzuku kwenye matibabu
Alikuta bwawa la umeme na sgr vikidema kwa kukosa pesa,kakamilisha
Barabara za lami kajenga na anaendelea
GDP ndani ya muda mfupi kaiongeza pakubwa
Uchumi ukuaji uliporomoka,kaupandisha
Mnachotaka nini toka kwake?!
Kama nyerere alivyosema ujinga hakika ni janga la Taifa.
Ngoja nikupe elimu nikutoe ujinga:
— Kuruhusu mikutano au kufuta kesi ni haki inayotolewa kikatiba wala siyo sifa ya kiongozi bora, na wala siyo achievement ya kupigiwa makofi.
– Kuajiri, kupandisha mishahara, kujenga shule na hospitali ni kazi ya serikali duniani kote zingatia "duniani kote".
– Miradi mikubwa, barabara, SGR, bwawa, GDP kukua… hiyo kila taifa ipo.
Baadhi ya sifa za uongozi mbovu ni hizi hapa:
— Gharama za maisha zinapanda kuliko kipato,
— Taasisi nyingi zinazidi kuwa dhaifu,
— Deni la taifa kuongezeka,
— Maamuzi yanategemea sana mtu mmoja na
— Sauti tofauti zinazopambania hilo huwa zinanyamazishwa kwa jina la “uhalifu”.
Zingatia: Jenga hoja bila kutaja jina kama nifanyavyo mimi
Hapo tunakuwa tunajadili systems za world wide.