respect wa boda hakuna anayemshambulia
Pasco, tunasema ukweli. Ukweli ambao hata
Pasco amesema kuwa ukiangalia video ya kukaa kwenye kiti, ni "bonafide genuine" Je mkuu hayo maneno ya Pasco unayaelewa maana yake? Hakuna anayemshambulia Pasco tunajadili. Na Pasco hajasema anashambuliwa tunajadili, maana sisi ni sehemu ya Jukwaa la Wafikiriao kwa kichwa na si kwa feeling.
FaizaFoxy ametaja "kila dalili za ugonjwa" hajatuhumu Lowasa kuugua huo ugonjwa, bali kasema kila dalili... wakuthibitisha hayo ni daktari wake na familia yake. Hili liko ndani ya uwezo wa hao tulowataja, na ndo maana mimi msimamo unabaki Lowasa anaumwa, kwa kuwa sina uhakika na ugonjwa anaoumwa sijautaja; tunaelezea dalili za machoni, ambazo zaweza kuwa kweli au si kweli.
Lowasa alisema chama kiandae utaratibu wa kuwapima wagombea wote ikiwamo na yeye, hii ni kauli ya kisisasa maana hata yeye anajua hilo haliwezekani, hata ukiwapima uamuzi wa kutangaza matokeo hautakuwa wa chama bali mgombea binafsi. Na ninadhani hii inaweza kuwa sababu kubwa ya kutoweka afya kama kigezo, chama hakina uwezo kutangaza matokeo ya kiafya ya mgombea yeyote yule. Kwa kwa technicality hii Lowasa na yeye alisema vile out of jazba maana anajua haiwezekani. Sasa sisi ambao haya hatuyajui, tunatokwa mapovu pasi kuruhusu akili zetu kufikiri mara mbili.
Yeye anajijua, anaumwa. Nyinyi ambao mnaamini vimaneno vya niko fit kwa mapambano, haya subirieni, only time will tell na tutakaa pamoja kama waTZ kukubali kumbe alikuwa anaumwa!!!!
Mfungo memo ndugu, kama wafunga weye...