Hii ndio Orodha ya makundi ya watu wanaohitaji Katiba Mpya na wasiohitaji

Kenya wana katiba tunayoambiwa ni bora sana lakini ufisadi na umasikini kwa raia umekita mizizi!

Ndio kusema kwamba katiba ya Kenya ni nzuri kwa wanasiasa tu!

Katiba nzuri na huku una njaa ni sawa na unyani
Unaweza kuthibitisha kauli yako?
Tunahitaji Katiba ya Wananchi itakayotokana na mawazo yao na siyo Katiba nzuri.Kama Katiba ya Kenya haijatatua changamoto zao za kiuchumi,kijamii,kisiasa,usawa ama haitoi Haki sawa kwa wananchi,ni jukumu lao kuiboresha na isiwe sababu ya Watanzania kutokuandika Katiba yao.
Sidhani kama ni sahihi kuwatisha Wananchi, ujenzi wa uchumi hauwezi kuwa mbadala wa Katiba Bali Katiba Bora ni msingi wa kujenga uchumi endelevu.
Tusiwapotoshe Watanzania. Kwenye madaraka hawastahili kuwazibia Wananchi kujipatia Katiba waitakayo.
 
Sihitaji Katiba wala nini nachotaka ni ugali mezani na kulipa ada za wanangu bila shida.
Nakubaliana na wewe. Naamini wewe na mm ni wale ambao hatujui kilichopo kwenye katiba ya sasa. Mimi naongezea hitaji la moyo wangu la kuwa na viongozi waadilifu na hodari wa kusimamia haki kwa kutumia busara. Wabunge wasimamie maendeleo ya wapiga kura wao na wazikane nafsi zao wasikubali Kula kabla wananchi wao hawajashiba.
 
Ukiwa an Average Tanzanian
Wala huna maslahi na Katiba mpya wala ya zamani
Maadam unachunga mdomo wako na kufuata sheria za nchi.,
 
solution yetu nafikiri ipo kwenye mda na matukio, otherwise kwa sasa hv wananchi ni kama hamna power, mmefinywa na ikitokea kuna mtu au kundi linataka kufanya mapinduzi basi linazimishwa fasta, au wananchi wapumbavu wasioelewa kinachoendelea kwenye siasa/duniani wanatumika, na hili group la wajinga ndo group hatari sana, imagine una nchi yenye watu asilimia kubwa hawajui kinachoendelea duniani, wamefocus sana kwenye story za mpira na wasanii, hivi unategemea group kama hili wewe ukiwa kama mwana harakati lina kusaidia nn Zaidi ya kukuona kama jambazi unaetaka kupindua nchi, ujinga ni tatizo kubwa sana mkuu ambalo watu wengi hawalioni, watu wanafocus kwenye usimba na yanga, na Tanzania watu wanachukulia siasa kama sehemu ya entertainment, so usitegemee kuna mtuanaweza kua serious na kitu chochote kinachohusiana na siasa au maendelea
usikimbilie kuwalaumu hilo kundi. Hata hawaviongozi wanaharakati nao sometimes ni kikwazo. Hebu fikilia kiongozi anatumia miaka zaidi ya 8 kuhubiri kuwa Fulani ni mwizi. Fisadi cha ajabu kwenye uchaguzi huyo wanayemwita fisadi ndo wanampa apeperushe bendera ya chama kugombea. Unategemea vijana wamwamini tena?
 
Kenya wana katiba tunayoambiwa ni bora sana lakini ufisadi na umasikini kwa raia umekita mizizi!

Ndio kusema kwamba katiba ya Kenya ni nzuri kwa wanasiasa tu!

Katiba nzuri na huku una njaa ni sawa na unyani

Pamoja na mapungufu yote hayo uliyosema, bado katiba ya Kenya ni nzuri na madhubuti kuliko yetu. Na uchumi wa Kenya ni bora kuliko wetu. Hapa unachosema ni sawa ww umepata kwenye masomo F, anasifiwa mwenzako mwenye C+, ww unasema huyo mwenye C+ pamoja na kusifiwa, lakini hajapata A!
 
Ukimuonyesha mtanzania uhusiano wa wazi na moja kwa moja jinsi gani katiba imefanya tuwe na hali mbaya ya kiuchumi au jinsi gani katiba itaboresha need ya chini kabisa ya kila mwananchi kama ilivyo kwenye Maslow's hierarchy basi hata hilo kundi ambalo halina muda na katiba litaanza kufikiri zaid,
,, msiwahukumu kuwa hawataki katiba wakat mnajua dhahiri kuwa hayo yooote ya kutaka au kutokutaka katiba ni for your own interests za kisiasa

CCM wanatumia advantage ya kutuweka kwenye hali duni for more than 60 years kutufanya tusifikirie vitu vikubwa,,,,siwezi kutaka burger wakati mlo wa siku ni shida kuupata( simple personality calculation) siwezi kuwaza self esteem au self actualization level wakati physical and security needs sijazipata bado

CHADEMA wana hoja nzuri za kutaka mabadiliko ya kiutawala ( na sio kikatiba kama wanavyo claim wao) najua kama CHADEMA wangekuwa wenye nchi sasa hv hoja ya katiba isingekuwa kipaumbele kwao,, ( wenye fikra finyu watakataa)

Makundi hayo hayawezi kuwasikiliza kwa sababu hamjagusa sehemu ambayo wao wanaona ina umuhimu pesa, mlo, mavazi na uhakika wa kuingiza kipato kila siku,,,, sio CCM au CDM hakuna mwenye maelezo ya moja kwa moja ubadilishwaji wa katiba utaleta uhakika wa kupata angalau pesa ya matumizi ( nazungumzia kazi)

Mnasahau kuwa kundi la hao ambao hawataki katiba ndio kubwa zaidi tanzania wajuzeni hao ambao mnaona ni washenzi,,, kuhusu umuhimu wa katiba ambao unagusa maisha yao ya kila siku moja kwa moja (ukiwatoa CCM ) hapo mtafanikiwa
Twitter na mitandao ya jamii isiwadanganye kuwa each citizens of this doomed county anataka katiba


#politiciansarefiltyliers

Kwa taarifa yao hao wengi unaosema hawataki katiba mpya, kwa wingi wao huo huo hata ikija kwao ni sawa. Hilo kundi kubwa ni lile linaloburuzwa kwa chochote. Kwahiyo usitake kuonyesha kuwa hawaitaki kwa maana ya uelewa. Kwa maneno marahisi hilo kundi kubwa hawajui chochote, kwao kizuri au kibaya ni sawa tu.
 
Kwakuwa wana CCM ni wengi. Kwakuwa vijana chini ya miaka 40 na wenye kipato duni ni wengi. Kwakuwa wazee wa miaka zaidi ya 60 ni wengi na kwakuwa akina mama ni wengi, basi mjumuisho wao inaonesha wasiotaka Katiba Mpya ni WENGI SANA! Hivyo basi, wanaodai Katiba Mpya ni wahuni wachache ambao hawatakiwi kuyumbusha mawazo ya wengi!

Sio kwamba hawataki, hao bado wako usingizini. Hili kundi ni la kuswaga tu kama ng'ombe. Maana hata ikija hiyo katiba mpya kwao ni poa, isipokuja ni sawa tu. Sasa kama watu wanakunywa maji ya tope na wanyama, huku viongozi wakitembea na maVX ya 500m na hawajui lolote wanaona sawa tu, hao unawaambia kuhusu katiba mpya ili iweje? Hayo ni ya kuburuza tu.
 
Kwanza kuna swali moja la kuuliza. Unapokuwa madarakani unaweza ukawa unakuja kwa nia njema kabisa ya kupigania haki za wananchi na sio maslahi binafsi na kulinda serikali hata kama inakosea.

Kwa maneno hayo sasa. Tujiulize, ni wangapi ambao wanaweza kuweka kipaumbele shida za wananchi na kuweza ku sacrifice hata uhai wake. Tunajua kupigania haki ni jambo linalohitaji ujasiri sana. Ili uwe kiongozi bora katika hili ni lazima pia usiwe mlafi wa pesa na uroho wa madaraka, pia unahitaji kua na mindset ya mwanafalsafa.

Kwa mfano tunawalaumu sana viongozi/wanasiasa juu ya uwajibikaji. Lakini ukweli mchungu kwa dunia ya sasa viongozi ni wafanyabiashara. Na siku zote mfanya biashara atafanya chochote hata kudiriki kudanganya wananchi ilimradi lengo lake litimie. Hawa huwa hawana uchungu na jamii wanazotoka, huwa ni waoga wa kupoteza mali na pesa kwa ajili ya kupambana dhidi ya matatizo ya nchi.

Kiongozi wa aina hii, huwa anahakikisha anacheza karata yake kwa umakini sana akiwa madarakani au nyazfa yoyote ya uongozi.
Sisi wananchi tunabaki kulia mara ooh mbona mbunge fulani anajua tuna matatizo fulani wilayani lakini haongei. Anaweza asiongee kwa sababu kwake ni rahisi kuishi vizuri aki defend serikali kuliko ku defend wananchi. So wanachofanya wanaaangalia sehemu yenye influence ya power. Kama kusifia raisi kutamfanya maisha yake yawe mazuri na salama atasifia sana hata kama ni ujinga.

Ndo maana tunasema kwa dunia ya sasa 2021 tuna wafanya biashara wengi sana kwenye nyazifa za uongozi kuliko wazalendo na viongozi wa kweli. Sifa kuu ya mfanyabiashara ni kufanya chochote kinachomwezesha kupata hela na usalama wa maisha yake sio ya wananchi.

Sasa solution ya hii mambo ni nn wakuu? South afrika imetuonesha ni kiasi gani kuna wafanya biashara wengi kuliko viongozi. Kuna swala la kujifunza hapa kama nchi.
Uko sahihi viongozi wengi ni wafanyabiasha ndio maana wanataka katiba inayowalinda. Wenzetu wenye mfumo mzuri biashara na uongozi ni tofauti Cc. Trump administration ilishindwa kwa sababu mfumo wa wenzetu haukumpa nafasi kufanya ujinga na nchi kwa ajili ya biashara zake na ndio tunataka katiba ya aina hiyo
 
Back
Top Bottom