Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,891
HII NDIO ORODHA YA MAKUNDI YA WATU WANAOHITAJI KATIBA MPYA
Na, Robert Heriel
Mjadala unaoendelea katika Siasa mitandaoni ni ishu ya Katiba.
Wanaohitaji Katiba Mpya wamegawanyika katika makundi Yafuatayo;
1. Wanasiasa hasa wa vyama vya Upinzani
2. Wanasiasa upande wa Zanzibar.
3. Wanaharakati wa mrengo wa kiliberali.
4. Wasomi wenye elimu kuanzia stashahada mpaka uzamivu. Wenye exposure ya dunia na wenye kutaka mabadiliko kwenye nchi.
Kiuchunguzi makundi hayo ukiyajumlisha ili upate idadi kamili basi ni wazi ni asilimia 20% tu ya Watanzania wote.
Makundi yasiyohitaji Katiba mpya na wala yasiyojishughulisha kama kujua kinachoendelea;
1. Wanawake wengi hapa nchini hawana mpango na ishu za Katiba mpya wala hawalijui Katiba ya zamani.
2. Vijana wa umri chini ya miaka 40 ambao wanaelimu ya chini na Hali zao za kimaisha ni duni. Hawa ukiwakuta kijiweni ukileta mambo ya Katiba mpya ndio utavuruga kila kitu. Kwanza hawatachangia mada. Kundi hili mada zake ni Udaku, mpira, kisha Diamond na Ally Kiba
3. Wana CCM
Kundi hili lipo lipo, hili ni Kama bendera, Inategemea serikali itakapoegemea. Serikali ikisema Katiba mpya ndio, nalo linasema Katiba mpya ndio, serikali ikisema hapana, nalo linasema hapana.
4. WAZEE Hasa wenye miaka kuanzia 60+
Kundi hili litasimama upande serikali ilipo. Kundi hili sio la kulaumiwa Kwa sababu wengi wao elimu Yao ni duni, exposure ya dunia iendavyo pia ni hafifu.
Kundi hili lisilohitaji au kujishughulisha na masuala ya Katiba ndilo kundi lenye watu wengi zaidi, karibu 80% hawana mpango wa Katiba mpya wala hawajihusishi na Siasa.
Uchunguzi wangu unaonyesha kuwa Watanzania wengi wanaamini katika serikali iliyopo madarakani, wanaiheshimu na kuigopa.
Hivyo serikali ikisema No! Basi watu nao watasema No!
Hata hivyo, uchunguzi wangu umebaini kuwa Watanzania wengi ni WANAFIKI, Unafiki wa Watanzania waliowengi unachangiwa kwa kiasi kikubwa cha Umasikini,
Ulimbukeni,
Elimu duni,
Woga na kujikomba Kwa wenye mamlaka.
Aidha Kama nilivyoeleza kwenye andiko langu lililopita ni kuwa, wanaodai Katiba mpya ni Kwa sababu ya mapungufu ya Katiba hii ambayo yanawafanya wasinufaike na Nchi yao.
Na wanaccm wengi wao hasa watawala, hawaoni Upungufu wa Katiba iliyopo hivyo inawanufaisha.
Kundi la mwisho ambalo ni wananchi ambao hawapo upande wowote hawa ni Bora liende, maisha yasonge, mauti ije, kaburini wafukiwe.
Binafsi, ninahitaji Katiba mpya itakayonufaisha makundi yote ya wananchi wa TANZANIA.
Hata hivyo, Siwezi kataa kuwa ndani ya jamii yangu, wananchi wengi hawana habari na Katiba mpya kwani wao ni Bora maisha siku ziende.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Na, Robert Heriel
Mjadala unaoendelea katika Siasa mitandaoni ni ishu ya Katiba.
Wanaohitaji Katiba Mpya wamegawanyika katika makundi Yafuatayo;
1. Wanasiasa hasa wa vyama vya Upinzani
2. Wanasiasa upande wa Zanzibar.
3. Wanaharakati wa mrengo wa kiliberali.
4. Wasomi wenye elimu kuanzia stashahada mpaka uzamivu. Wenye exposure ya dunia na wenye kutaka mabadiliko kwenye nchi.
Kiuchunguzi makundi hayo ukiyajumlisha ili upate idadi kamili basi ni wazi ni asilimia 20% tu ya Watanzania wote.
Makundi yasiyohitaji Katiba mpya na wala yasiyojishughulisha kama kujua kinachoendelea;
1. Wanawake wengi hapa nchini hawana mpango na ishu za Katiba mpya wala hawalijui Katiba ya zamani.
2. Vijana wa umri chini ya miaka 40 ambao wanaelimu ya chini na Hali zao za kimaisha ni duni. Hawa ukiwakuta kijiweni ukileta mambo ya Katiba mpya ndio utavuruga kila kitu. Kwanza hawatachangia mada. Kundi hili mada zake ni Udaku, mpira, kisha Diamond na Ally Kiba
3. Wana CCM
Kundi hili lipo lipo, hili ni Kama bendera, Inategemea serikali itakapoegemea. Serikali ikisema Katiba mpya ndio, nalo linasema Katiba mpya ndio, serikali ikisema hapana, nalo linasema hapana.
4. WAZEE Hasa wenye miaka kuanzia 60+
Kundi hili litasimama upande serikali ilipo. Kundi hili sio la kulaumiwa Kwa sababu wengi wao elimu Yao ni duni, exposure ya dunia iendavyo pia ni hafifu.
Kundi hili lisilohitaji au kujishughulisha na masuala ya Katiba ndilo kundi lenye watu wengi zaidi, karibu 80% hawana mpango wa Katiba mpya wala hawajihusishi na Siasa.
Uchunguzi wangu unaonyesha kuwa Watanzania wengi wanaamini katika serikali iliyopo madarakani, wanaiheshimu na kuigopa.
Hivyo serikali ikisema No! Basi watu nao watasema No!
Hata hivyo, uchunguzi wangu umebaini kuwa Watanzania wengi ni WANAFIKI, Unafiki wa Watanzania waliowengi unachangiwa kwa kiasi kikubwa cha Umasikini,
Ulimbukeni,
Elimu duni,
Woga na kujikomba Kwa wenye mamlaka.
Aidha Kama nilivyoeleza kwenye andiko langu lililopita ni kuwa, wanaodai Katiba mpya ni Kwa sababu ya mapungufu ya Katiba hii ambayo yanawafanya wasinufaike na Nchi yao.
Na wanaccm wengi wao hasa watawala, hawaoni Upungufu wa Katiba iliyopo hivyo inawanufaisha.
Kundi la mwisho ambalo ni wananchi ambao hawapo upande wowote hawa ni Bora liende, maisha yasonge, mauti ije, kaburini wafukiwe.
Binafsi, ninahitaji Katiba mpya itakayonufaisha makundi yote ya wananchi wa TANZANIA.
Hata hivyo, Siwezi kataa kuwa ndani ya jamii yangu, wananchi wengi hawana habari na Katiba mpya kwani wao ni Bora maisha siku ziende.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro