Hii ndio Orodha ya makundi ya watu wanaohitaji Katiba Mpya na wasiohitaji

Mengi uliyoyaandika ni ya kweli kabisa.
Ifike mahali tukubaliane kwamba:
1.Katiba mpya ni hitaji mhimu kwa Watanzania
2.Katiba mpya iliyo bora haiwezi kuletwa na wanufaika na Katiba iliyopo.
3.Katiba mpya na iliyobora kwa nchi nyingi za Africa, huwa inapatikana kwa njia mbili tu
a)Kwa utashi wa wenye nguvu ya kimamlaka,na/au

b) Kwa ushindi wa wenye mamlaka ya nguvu.(Hapa tofautisha wenye nguvu ya kimamlaka na wenye mamlaka ya nguvu)
4.Watanzania walio wengi ni mbumbumbu wa kisiasa, hivyo hawajitambui na kimsingi hawawezi kushiriki katika vuguvugu la kudai Katiba mpya japo ina manufaa makubwa kwao.
5.Kutokana na hoja hizo hapo juu, ni wazi kwamba upatikanaji wa katiba iliyo bora kwa Watanzania inategemea tu utashi wa mwenye nguvu ya kimamlaka ambaye, kwa hali ilivyo kwa sasa, ni Rais tu.(Rejea ujio wa Demokrasia ya vyama vingi Tanzania)
Vinginevyo, wenye mamlaka ya nguvu,( jambo ambalo sisi wananchi hatuombei litokee katika nchi yetu na Mungu aepushie mbali) wataleta hiyo katiba mpya.


Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app

Watanzania wengi wanaishi Bora siku ziende
 
..kuna makosa ktk uwasilishaji au uchambuzi wa makundi kuhusu katiba.

..mchambuzi amefanya kosa la kuchanganya kundi linalopinga katiba mpya, na kundi lisilokuwa na uelewa wa katiba.

..mchambuzi au mtoa mada alitakiwa ayabainishe makundi yafuatayo.

1. Kundi linalodai katiba mpya.

2. Kundi linalopenda katiba ya zamani.

3. Kundi lisilokuwa na uelewa wa katiba.

..makundi # 1 na # 2 yanatakiwa kuwaelimisha na kuwashawishi walioko ktk kundi # 3.

..vilevile kuna umuhimu wa KUJIFUNZA toka ktk kundi # 3. Kutokuielewa katiba haimaanishi kutokuihitaji katiba.

Nimewaweka wasio na Uelewa Kama wapinga mchakato wa Katiba mpya Kwa sababu wengi wao wapo upande wa serikali(CCM)
 
Nimewaweka wasio na Uelewa Kama wapinga mchakato wa Katiba mpya Kwa sababu wengi wao wapo upande wa serikali(CCM)

..nadhani hiyo assumption sio sahihi.

..kutokuelewa kuhusu katiba haimaanishi moja kwa moja ni kuipinga.

..walioko ccm wanaelewa katiba mpya ni nini na katiba ya zamani ni nini.

..mwisho, mbona hujaweka kundi lisilotaka katiba kabisa?
 
Nimeipenda hii"wasomi kuanzia stashihada mpaka uzamivu" mimi naongezea na maprofesa. Kenya wanatumia hiki kipengele ndio maana wao hawaangalii makunyanzi.
 
..nadhani hiyo assumption sio sahihi.

..kutokuelewa kuhusu katiba haimaanishi moja kwa moja ni kuipinga.

..walioko ccm wanaelewa katiba mpya ni nini na katiba ya zamani ni nini.

..mwisho, mbona hujaweka kundi lisilotaka katiba kabisa?

Hakuna kundi lisilotaka Katiba mpya kabisa wala hakuna linalotaka Katiba mpya kabisa.

Makundi yote yapo katikati, Kama nilivyosema; Watanzania wengi ni WANAFIKI.

Hivyo, kinachozingatiwa ni upepo tuu unavyovuma
 
Ndio hatikaki iyo katiba ya walioba. Tunahitaji usawa na maendeleo. hatutaki kuji🙋‍♂️tenga. Tunataka universal laws. Sheria mona na usawa
 
Elimu na umasikini hapo ni kigingi
Katiba inazaa institutions lakini institutions siyo mashine. Watu ndo wanatengeneza hizo strong institutions.

Mabadiliko ya kifikra ni ya lazima. Hayaepukiki. Huwezi kuwa na Katiba nzuri. Katiba ya ‘wananchi’, bila ya watu kuiandika, kuifuata, kuilinda, kuihifadhi, na kuitetea ni sawa na zero.

Unaweza kuwa na Katiba mpya, ambayo ni nzuri kabisa, lakini huifuati, huilindi, huitetei, na kadhalika. Hakuna Tume Huru ya Uchaguzi inayojiendesha yenyewe.

Hakuna bunge wala Mahakama zinazojiendesha zenyewe, bali ni watu. Na ukitaka mabadiliko ya kweli kwenye hizo Taasisi, basi ni lazima pia ubadilike kifikra.

Hakuna mabadiliko yoyote yale ya maana pasipo na mabadiliko ya kifikra. Mindset lazima ibadilike. Matendo nayo lazima yabadilike.

Ukibadili Katiba na ukaacha kubadili fikra, hutoenda popote. Utaishia kukwama pale pale ulipo.
 
Mengi uliyoyaandika ni ya kweli kabisa.
Ifike mahali tukubaliane kwamba:
1.Katiba mpya ni hitaji mhimu kwa Watanzania
2.Katiba mpya iliyo bora haiwezi kuletwa na wanufaika na Katiba iliyopo.
3.Katiba mpya na iliyobora kwa nchi nyingi za Africa, huwa inapatikana kwa njia mbili tu
a)Kwa utashi wa wenye nguvu ya kimamlaka,na/au

b) Kwa ushindi wa wenye mamlaka ya nguvu.(Hapa tofautisha wenye nguvu ya kimamlaka na wenye mamlaka ya nguvu)
4.Watanzania walio wengi ni mbumbumbu wa kisiasa, hivyo hawajitambui na kimsingi hawawezi kushiriki katika vuguvugu la kudai Katiba mpya japo ina manufaa makubwa kwao.
5.Kutokana na hoja hizo hapo juu, ni wazi kwamba upatikanaji wa katiba iliyo bora kwa Watanzania inategemea tu utashi wa mwenye nguvu ya kimamlaka ambaye, kwa hali ilivyo kwa sasa, ni Rais tu.(Rejea ujio wa Demokrasia ya vyama vingi Tanzania)
Vinginevyo, wenye mamlaka ya nguvu,( jambo ambalo sisi wananchi hatuombei litokee katika nchi yetu na Mungu aepushie mbali) wataleta hiyo katiba mpya.


Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app

Uliyoandika ni sahihi kabisa tatizo linakuja ni kutoka kwa wale wahafidhina wanaomzunguka rais. Hao jamaa wenye viduku:

IMG_20210704_051559_619.jpg


Uzi huu ulikuwa wajieleza:

 
Back
Top Bottom