Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,864
- Thread starter
- #121
Mengi uliyoyaandika ni ya kweli kabisa.
Ifike mahali tukubaliane kwamba:
1.Katiba mpya ni hitaji mhimu kwa Watanzania
2.Katiba mpya iliyo bora haiwezi kuletwa na wanufaika na Katiba iliyopo.
3.Katiba mpya na iliyobora kwa nchi nyingi za Africa, huwa inapatikana kwa njia mbili tu
a)Kwa utashi wa wenye nguvu ya kimamlaka,na/au
b) Kwa ushindi wa wenye mamlaka ya nguvu.(Hapa tofautisha wenye nguvu ya kimamlaka na wenye mamlaka ya nguvu)
4.Watanzania walio wengi ni mbumbumbu wa kisiasa, hivyo hawajitambui na kimsingi hawawezi kushiriki katika vuguvugu la kudai Katiba mpya japo ina manufaa makubwa kwao.
5.Kutokana na hoja hizo hapo juu, ni wazi kwamba upatikanaji wa katiba iliyo bora kwa Watanzania inategemea tu utashi wa mwenye nguvu ya kimamlaka ambaye, kwa hali ilivyo kwa sasa, ni Rais tu.(Rejea ujio wa Demokrasia ya vyama vingi Tanzania)
Vinginevyo, wenye mamlaka ya nguvu,( jambo ambalo sisi wananchi hatuombei litokee katika nchi yetu na Mungu aepushie mbali) wataleta hiyo katiba mpya.
Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
Watanzania wengi wanaishi Bora siku ziende