Hakuna namna yoyote ya kutetea Uzembe huu uliotokea Ukonga,Ni kweli tukio zima ni ajali,lakini ni ajali ambayo ingeweza kuzuilika...Haiwezekani katika kipindi kisichozidi mwaka kutokee ajali zinazofanana,ina maana next month likitokea tukio kama hili Lugalo bado tutasema ni bahati mbaya?Inabidi Viongozi wetu wajifunze kutoa majibu sahihi kwa maswali magumu.Waziri Wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa inabidi atoa maelezo ya kina kwa Umma wa watanzania na kutafuta suluhu ya kuyaangamiza mabomu chakavu...kwa kutumia ujuzi na uwezo ndani ya jeshi lake au kuomba msaada nje ya nchi...Hatuwezi kuona Raia wasio na hatia wanapoteza maisha yao,na sababu inayotolewa na serikali ni ya kizembe eti "ni ajali tu".....hali ya joto kali imesababisha mabomu kulipuka,majibu hayo ni dharau na matusi kwa waathirika na raia wa Tanzania,imefika wakati sasa Viongozi wetu wajifunze kujiuzulu,ikitokea kashfa ndani ya mamlaka yao...Waziri Mwinyi jiteteee!Utetezi wako uandamane na KUJIUZULU!