Jana mimi hawa jamaa wa TV stesheni walinikera sana kutoonyesha habari hizi hata japo picha za tukio.
Please source ya 200 umepata wapi?
SI HAKI KUMUHUKUMU NGIRI KUWA ANACHEKA MUDA WOTE HATA KWENYE MSIBA YEYE ANACHEKA, "JAMANI NGIRI MENO KUWA NJE SI KUCHEKA NI MAUMBILE YAKE TU"TUJIKUMBUSHE MABOMU YA APRILI 2009 MBAGALA
![]()
Picha tu inatosha kuonyesha kuwa huyu prezident sio makini.........Huwezi kuwana na furaha katika mazingira kama hayo hayo, inaonyesha kuwa jamaa ni kama alionekana kutoguswa kabisa na hilo tukio huwezi kutabasamu wakati watu wamepoteza maisha!
Kama madaraka tunapeana kiswahiba mtawajibishana vipi?? Inabidi tuseme ni bahati mbaya ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Hivi kweli JK anaweza kumuwajibisha mtoto wa Mwinyi?? Si Mwinyi naye aliwahi kumpa JK uwaziri na JK kalipa kwa kumpa mtoto wa Mwinyi... Kwanza tujiulize sakata la Mbagala kuna mtu hata mmoja alijiuzuru?? Kama hakuna then nani angechukua taadhari wakati hakuna issue yoyote kubwa nchii hii hata kama watu wanakufa. Kosa lilishafanyika kuruhusu Mkwere achakachue kura na kubakia kuwa rais then tuendelee tu kubeba msalaba manake ndo adhabu zenyewe hizo na laana toka kwa Mungu
Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....
Taarifa zaidi kufuatia.
UPDATES: (by Invisible)
1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!
2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.
3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii
4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari
5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:
"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.
6. Kwa mujibu wa FikraPevu, anga limefungwa kwa muda na ndege hazitaweza kutua uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.
7. Mkono wa mtu (mwanamke), moyo na viatu (na khanga) vimeokotwa... - Radio One
8. Picha ya tukio kwa mbali sana...
![]()
![]()
![]()
VIDEOS:
Unakumbuka Mbagala walisema wangapi wamekufa?
Alafu si walisema haya mabomu yaliyo zeeka wanayaharibu?
Nafikiri haya mabomu yangelipuka IKULU labda watu ndio watawajibishwa lakini hili tutaendelea kusikiliza story tu.