Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Lazima kuna mtu anayachokonoa maksudi au labda mabomu ya ki-expire yanalipuka yenyewe? Manake nashindwa kuelewa miaka yote hio ndio yaje kulipuka mwaka jana na mwaka huu kwa mfululizo?

Hile ripoti ya mbagala ilikuja na sababu gani sijui ,kama mtu anaijua naomba jibu tafadhali.

Maombi yangu yote kwa watanzania wenzangu Mungu hawalinde popote mlipo.
ni kweli lazima kuna mtu atakuwa anayachokonoa tuu ina maana mwaka jana na mwaka huu ndio ywameanza kuoza
 
Mimi nipo Mbezi Luguruni bado naona mabomu yanaendelea kulipuka. Na Jamaa zangu siwapati wanaokaa maeneo ya Gongo la Mboto. Tumwombe MUNGU awanusuru Ndg. Zetu
 
Haya mabomu yatakuwa ni yale ya enzi za mkoloni, na huenda ni mabaki ya yaliyotumika wakati wa vita ya pili ya dunia!
 
Huyu mtoto wa mwinyi sasa imefika wakati wake wa kutuachia wizara yatu

Hivi mnajua kwa nini hakuna Mkuu wa Majeshi wa kutoka Zanzibar tangu nchi hii ijinyakulie uhuru? Ni kuhofu kwamba mtu huyo asije akawa kumbe ni mse***!
 
Ahsante kwa kuwajuza wadau, mimi ni muathirika na naingia hapa walau nikiwa nimeinusuru family yangu, NI HATARI HATARI HATARI SAANA.
Siipendi tanzania yangu
 
Mungu ashukuliwe kwa kuwaokoa. Tuombe aokoe na wengine. Nadhani inabidi tuandamane majeshi yahamishiwe mbali na miji




wadau naingia jamvini muda huu nikiwa ni muathirika wa mambomu na nilikuwa huko na ndipo napoishi, nimeendesha gari pasipo kujijua na sijui nyumba yangu itasalimika ama la, imenilazimu niingie jamvini niwape hali halisi na si kuhadithiwa, NI HATARI SAANA WADAU.
Sasa rasmi ninailaani serikali hii, ni adha kubwa na nimeiharibu mpaka gari kwa hamaki ya kuinusuru my family.
 
Pengine akifa na mkuu mmoja au wawili wataelewa nini thamani ya Maisha ya Mtanzania Mmoja. Mungu tusaidie
 
Kwa kweli ni vigumu kutabiri chochote ingawa sauti za milipuko hazifululizi kwa sasa km ilivyokuwa hapo mwanzoni, hasa ikizingatiwa kuwa kutakuwa na mabomu yaliyotua sehemu kadhaa ambayo bado hayajalipuka.
 
Tanzania haikaliki tena Mungu wangu.Watanzania lazima tuamke na kusema no to the Freemasons in Tanzania. Whatever is happening is their work by remote control. Kama hatuta amka we are finished.My fellow Tanzanians please, please work up.These people have infiltrated every institution and have vowed to bring mayhem towards 2012.Hizi ni strategy za kizamani sana za ku-enslave.

Sijaelewa hapo kwenye red na matatizo yetu inawezekana tunapigana vita moja lakini wengine hatuwajui vizuri adui zetu, ebu fafanua, unaruhusiwa kuni-PM
 
Hivi Kikwete yupo Dar au yupo ziarani? Ilitakiwa awepo eneo la tukio.
 
kuna kipande cha bomu kimetua ubungo mpaka magari yaelekeayo barabara ya morogoro yalitikisika.watu wa tabata waliliona likipita!MWAMUNYANGE NA MWINYI WASIPOJIUZULU KESHO NITAJUA KWELI VIONGOZI WA AFRIKA HAWAAMBILIKI!
 
Milipuko ya Mbagala Serikali walisema RAIA WALIJENGA KARIBU NA MAENEO YA JESHI KWA NGUVU NA WAKASHAURIWA WAHAME.
  1. Je,kwako Mhe. Dr. Mwinyi Waziri wa Ulinzi HAWA RAIA WA GONGO LA MBOTO NAO WAMEHAMA KUYAFUATA MABOMU AU MABOMU YAMEWAFUATA RAIA?????
  2. Kama milipuko ya Mbagala mliona TATIZO NI RAIA KUWA KARIBU NA MAENEO YA JESHI KWANINI HAMKUWAHAMISHA RAIA WOTE WALIOKARIBU NA MAENEO YA JESHI HASA MAGHALA YA JESHI(ARMOURY)?
Tunataka KESHO ASUBUHI UTANGAZE KUJIUZULU KAZI YA JESHI IMEKUSHINDAAAAAAAAAAAAAAAAAA!
Tunakuomba kwa heshima na taaadhima ujiuzulu kufuata nyayo za Babako mzee Mwinyi aliyejiuzulu miaka ile ya 70s kuwajibika alipokuwa Waziri wa Mambo ya NDANI. Itakujengea heshima kama babako na pengine ukaukwaa Urahisi wa Zanzibar na baadaye Bara kama babako.

Kazi kwako.




Kujiuzulu haitoshi inabidi tuwachukulie na hatua za kisheria wale wote wanao husika na hili suala direct or indirect,yan mkuu wa majeshi,usalama wa taifa,mkuu wa kambi,waziri, naibu wake etc
 
dah,rafiki yangu amekimbia toka ukonga hadi BUGURUNI,ndo anamuomba konda apande daladala aje mwananyamala,ana pensi tu,anasema mosh una washa sana,
JE WAFUNGWA WA GEREZA LA UKONGA WANAENDA WAPI?
 
Sijaelewa hapo kwenye red na matatizo yetu inawezekana tunapigana vita moja lakini wengine hatuwajui vizuri adui zetu, ebu fafanua, unaruhusiwa kuni-PM
Kweli inabidi ufafanuzi hapa namna freemasons walivyo/wanavyo husika na tukio hili.
 
Back
Top Bottom