fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....
Taarifa zaidi kufuatia.
UPDATES: (by Invisible)
1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!
2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.
3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii
4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari
5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:
"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.
6. Kwa mujibu wa FikraPevu, anga limefungwa kwa muda na ndege hazitaweza kutua uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.
7. Mkono wa mtu (mwanamke), moyo na viatu (na khanga) vimeokotwa... - Radio One
8. Bunge limeahirishwa kufuatia tukio hili
9. Waziri Mkuu Mizengo Pinda anadai idadi ya waliokwisha kufa ni zaidi ya 19 lakini tunaarifiwa kuwa idadi halisi huenda ni zaidi ya 100.
10. Jeshi la Polisi linawaarifu wale wanaotafuta watoto wao na hawawaoni kwenda kwenye vituo vya polisi jijini kwani kuna watoto wengi wamepelekwa huko.
11. Wananchi wanaombwa kukaa mbali na eneo la tukio kwani hali haijawa shwari.
Picha ya tukio kwa mbali sana...
VIDEOS:
Taarifa zaidi kufuatia.
UPDATES: (by Invisible)
1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!
2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.
3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii
4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari
5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:
"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.
6. Kwa mujibu wa FikraPevu, anga limefungwa kwa muda na ndege hazitaweza kutua uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.
7. Mkono wa mtu (mwanamke), moyo na viatu (na khanga) vimeokotwa... - Radio One
8. Bunge limeahirishwa kufuatia tukio hili
9. Waziri Mkuu Mizengo Pinda anadai idadi ya waliokwisha kufa ni zaidi ya 19 lakini tunaarifiwa kuwa idadi halisi huenda ni zaidi ya 100.
10. Jeshi la Polisi linawaarifu wale wanaotafuta watoto wao na hawawaoni kwenda kwenye vituo vya polisi jijini kwani kuna watoto wengi wamepelekwa huko.
11. Wananchi wanaombwa kukaa mbali na eneo la tukio kwani hali haijawa shwari.
Picha ya tukio kwa mbali sana...
VIDEOS:
Last edited by a moderator: