Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....

Taarifa zaidi kufuatia.

UPDATES: (by Invisible)

1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!

2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.

3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii

4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari

5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:

"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.

6. Picha ya tukio kwa mbali sana...

obhbd.jpg

shimbo badala ya kufanya kazi za jeshi akaingia kuitetea ccm sasa ajue maana ya kutotawalika kwa nchi ndio huku kama kila baada ya muda mnaua wananchi kwa uzembe hivi habari za kintelejensia ziko wapi kwa hili
 
Mie nipo hapa mazimbu mara ya kwanza ni kishindo kiligonga radi c radi lakini milio iliyofuata ni kawaida ndo hapo nika associate na hyo taarifa maana c kawaida may be tusuburi asubuhi watasema nini.

dah,hadi mazmbu?uuwi
 
hivi maji ya kuwasha hayawezi kuzuia mabomu kulipuka ... au ni kwa ajili ya kuwatesa wananchi tuu
 
Ni vigumu hata kwa wataalamu wa kutegua mabomu kusogea eneo la tukio hadi saa kadhaa zipite bila ya kusikika milipuko.
 
MWAMUNYANGE NA MWINYI WASIPOJIUZULU KESHO NITAJUA KWELI VIONGOZI WA AFRIKA HAWAAMBILIKI!

kwa mara ya kwanza nitakiri Kikwete alishinda uchaguzi na ni Rais halali wa Tanzania.

na nitaomba radhi Watanzania kwa kumnyima kura chalii yangu JK katika chaguzi za 2005 na 2010
 
Duh!! Dawa yake ni kupitisha sheria viongozi wote kukaa katk nyumba za serikali na zitajengwa katibu na hizo gara za silaha. Haiwezekana sahizi mtu napiga kikombe cha chai na kutoa komenti upuuzi. Kwanza wananchi wote walitakiwa waelekweze wapi watatakiwa kwenda, uliznzi uwepo, maana kwa jinsi hii ni rahisi watu kubakwa, kuibiwa ,kupoteza watoto, kufa kwa kukosa huduma , wajawazito etc.
 
Haya mabomu yatakuwa ni yale ya enzi za mkoloni, na huenda ni mabaki ya yaliyotumika wakati wa vita ya pili ya dunia!

Hapana mkuu. Ni umaamuma na kutokujali kwa serikali na wakuu wetu jeshini tu. Haijalishi raia tukiuawa na haya mabomu!
 
Tanzania haikaliki tena Mungu wangu.Watanzania lazima tuamke na kusema no to the Freemasons in Tanzania. Whatever is happening is their work by remote control. Kama hatuta amka we are finished.My fellow Tanzanians please, please work up.These people have infiltrated every institution and have vowed to bring mayhem towards 2012.Hizi ni strategy za kizamani sana za ku-enslave.

Yani nina hasira na uzembe wa serikali lakini we jamaa umenifanya nicheke na story zako za Freemasons. Keep on blaming them masons but our enemy is among us...
 
nchi hii ni ya hovyo saana, SIJUI WANAUSALAMA WANAMSALITI MKUBWA WAO AMA?
nimepata adha isiyo kifani leo hii.....AAAH
 
Pengine akifa na mkuu mmoja au wawili wataelewa nini thamani ya Maisha ya Mtanzania Mmoja. Mungu tusaidie
Ndio maana memba mmoja kapendekeza haya maghala ya silaha yawe jirani na ikulu!
 
Jamani imetosha sasa...miundombinu mibovu,huduma duni za kijamii,utendaji mbovu na mengi mengine...kwanini tusione uwajibikaji katika yote haya?
 
Awa wakazi wa Gongolamboto ambao at this time wapo Tazara,nna washauri waendelee mojakwamoja mpaka Ikulu.wakomae apo mpaka serikali iwathibitishie kama longolongo za Mbagala azitotokea kwao vinginenvyo wameliwa
 
wadau naingia jamvini muda huu nikiwa ni muathirika wa mambomu na nilikuwa huko na ndipo napoishi, nimeendesha gari pasipo kujijua na sijui nyumba yangu itasalimika ama la, imenilazimu niingie jamvini niwape hali halisi na si kuhadithiwa, NI HATARI SAANA WADAU.
Sasa rasmi ninailaani serikali hii, ni adha kubwa na nimeiharibu mpaka gari kwa hamaki ya kuinusuru my family.

Poleni sana, Mungu azidi kuwasaidia.
 
wadau naingia jamvini muda huu nikiwa ni muathirika wa mambomu na nilikuwa huko na ndipo napoishi, nimeendesha gari pasipo kujijua na sijui nyumba yangu itasalimika ama la, imenilazimu niingie jamvini niwape hali halisi na si kuhadithiwa, NI HATARI SAANA WADAU.
Sasa rasmi ninailaani serikali hii, ni adha kubwa na nimeiharibu mpaka gari kwa hamaki ya kuinusuru my family.

pole sana
 
Radio One: mabomu yanaripuka, nyumba zina waka moto
 
Back
Top Bottom