Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, akijibu swali la Mwandishi leo Juni 10, 2026 kuhusu taarifa ambazo chama hicho zimeeleza kuwa kufuatia kusikilizwa kwa kesi ya Tundu Lissu kesho Polisi inajiandaa kushambulia wanachama na viongozi wa CHADEMA kwa kisingizio za taarifa za uongo kwamba CHADEMA wanajaribu kumuokoa Lissu
"Umeuliza sasa hizi taarifa za kiintelijensia, huu mpango huu ni ni polisi ngazi ipi? Ni je ni Jeshi la Polisi lote? Au ni baadhi?
Katika hatua hii wakati tunafuatilia taarifa zaidi, tunabebesha hili zigo la huo udhalimu na hiyo haramu inayopangwa kufanyika kesho kwa kanda maalumu Dar es Salaam na na mkoa wa kipolisi wa Ilala na na wilaya zake zinazohusika na eneo hilo la la mahakama hizi mbili; mahakama, Mahakama ya Rufaa ambayo iko pale Kivukoni, na Mahakama Kuu ambayo iko na yenyewe Kivukoni lakini zikiwa zimetenganishwa katikati na na hoteli ya Kilimanjaro, Kempinski pale.
Kwa hiyo wale ambao wanalitawala lile eneo kipolisi ndio ambao kwa sasa ah tunatuhumu kuhusika na njama za; kwanza kuna njama za kutengenezwa kwa vurugu pale, lakini pili kuna njama za polisi kujiandaa kutumia silaha na nguvu kwa kisingizio cha kudhibiti vurugu zilizotengenezwa, lakini target ikiwa ni kushughulikia viongozi na wanachama wa CHADEMA."
Katika hatua hii wakati tunafuatilia taarifa zaidi, tunabebesha hili zigo la huo udhalimu na hiyo haramu inayopangwa kufanyika kesho kwa kanda maalumu Dar es Salaam na na mkoa wa kipolisi wa Ilala na na wilaya zake zinazohusika na eneo hilo la la mahakama hizi mbili; mahakama, Mahakama ya Rufaa ambayo iko pale Kivukoni, na Mahakama Kuu ambayo iko na yenyewe Kivukoni lakini zikiwa zimetenganishwa katikati na na hoteli ya Kilimanjaro, Kempinski pale.
Kwa hiyo wale ambao wanalitawala lile eneo kipolisi ndio ambao kwa sasa ah tunatuhumu kuhusika na njama za; kwanza kuna njama za kutengenezwa kwa vurugu pale, lakini pili kuna njama za polisi kujiandaa kutumia silaha na nguvu kwa kisingizio cha kudhibiti vurugu zilizotengenezwa, lakini target ikiwa ni kushughulikia viongozi na wanachama wa CHADEMA."