Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....

Taarifa zaidi kufuatia.

UPDATES: (by Invisible)

1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!

2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.

3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii

Tanzania haikaliki tena Mungu wangu.Watanzania lazima tuamke na kusema no to the Freemasons in Tanzania. Whatever is happening is their work by remote control. Kama hatuta amka we are finished.My fellow Tanzanians please, please work up.These people have infiltrated every institution and have vowed to bring mayhem towards 2012.Hizi ni strategy za kizamani sana za ku-enslave.
 
milipuko bado inaendelea nipo kariakoo msimbazi anga yote mwanga wa moto, nadhani nyumba nyingi zatakuwa zimebomoka kwa milipuko mikubwa ya mabomu bora ya mbagala kuliko ya leo

bado yanalipuka.
 
Msemaji wa jeshi la polisi, anasema mabomu yanayolipuka hayajulikani yataisha saa ngapi , source eatv
 
Poleni sana ndugu zetu uko.hao wezi sasa uko leo!mh!mana hawanaga uoga wala huruma!
 
mabomu yanalipuka gongo la mboto polisi....

Taarifa zaidi kufuatia.

updates: (by invisible)

1. Hali ni mbaya jijini dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!

2. Barabara ya nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.

3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii


hivi hapa tbc1 wanaposema wananchi waondoke mbona hawasemi wameandaa kambi ya dharura wapi? .hivi mtu aondoke sasa hivi jamnai aende kulala wapi wakati hata hela ya gesti au kuchukua atm card hawezi kutokana na kukimbia. Hivi tunawapeleka wapi watanzania? Jamani.

Usishangae ndio kwanza jk anavuta shuka huku akimtuma mwinyi akaangalie ili aje kuzungumza kwenye hotuba ya kufunga mwaka 2011
 
milipuko bado inaendelea nipo kariakoo msimbazi anga yote mwanga wa moto, nadhani nyumba nyingi zatakuwa zimebomoka kwa milipuko mikubwa ya mabomu bora ya mbagala kuliko ya leo
Hii ni hatari kwa kweli, sipati picha wakazi wa gongo la mboto hali yao ikoje?
 
mimi nahisi hii mvua ya ghafla ndiyo iliyosababisha mabomu ku detonate ...labda paa la ghala la mabomu linavuja
 
Hivi mpaka wafe wangapi ndio wataacha kuhifadhi mabomu karibu na nyumba za watu???? Kutenda kosa sio kosa lakini kurudia kosa ni kosa. Lazima watu wawajibike safari hii.

Hii siyo serikali, ni genge la vijana wa wahuni.
 
Nilikuwa naulizia link ya kuhamasisha Vijana na wazee kwenye maanadamano ya Uhuru au ukombozi Ipo wapi? kama ipo tunaomba link:msela: Muda wakujiandaa umefika sio kila siku tunawaona waaraabu wakijipatia Uhuru katika nchi zao na kuwasifia

Intelijensia haikufanya kazi hapo kuepusha milipuko hiiii.....CHADEMA INAHUSIKA LABDA ITASEMEKANA KIITELIJENSIA....kwangu nilitaka yaelekee usawa wa whitehouse...uko vipi Tujuuzeni mliopo karibu...Ureeeeeeeeeeeeeeeeee...!!
 
Msemaji wa jeshi la polisi, anasema mabomu yanayolipuka hayajulikani yataisha saa ngapi , source eatv

hapo ni ile hadisi ya samaki moja akioza yote naoza.


hapa kuomba mungu tu asife mtu.

lakini lazima viazi vyote viwive.
 
fungueni radio free africa nao wanatoa updates vizuri,wanahoji wahanga live
 
Oooooi my God....nina jamaa zangu walikua K.I.U campus ya Gongolamboto nawaflash hawapatikani sasa...its so sad!
Dears I'm at Kinyerezi here it is really scarely. Hali ni mbaya, hakuna mtu kwa nyumba wote tuko njiani hatujui tunakokwenda. Tunamwamini Mungu atatutokea.
 
Eti msemaji wa jeshi kasema wakae maeneo ya mabondeni, mh! Source: Channel 5

Hao wanajeshi wa taaluma hiyo wote ni vihiyo wakubwa. Hakuna wanachojua! Vinginevyo wangejifunza kutokana na tukio la Mbagala. Mpaka wafe wangapi?
 
Tanzania haikaliki tena Mungu wangu.Watanzania lazima tuamke na kusema no to the Freemasons in Tanzania. Whatever is happening is their work by remote control. Kama hatuta amka we are finished.My fellow Tanzanians please, please work up.These people have infiltrated every institution and have vowed to bring mayhem towards 2012.
Ni kazi ya freemasons! Lete stori zaidi mkuu.
 
Tulianza na serikali na sasa sina imani n jeshi letu wananchi yaan JeiWii au JWTZ. Siamini kabisa kama hawa watu wanaoshindwa kuntrolsiraha kama wana uwezo wa kutulinda sisi wananchi!

Xuma....ninaanza kuona ile nuru ya "NAjivunia kuwa Mtanzania" ikififia.................. hatukujifunza na yaliyotokea Mbagala?? Hebu Waziri husika awajibishwe kama wafanyavyo wenzetu tuone ....tumuwajibishe. Ninaamini kabisa wananchi tunao uwezo wa kushinikiza hilo halafu tuone kama wengine watatuchezea...tumechoka kufanywa wajinga ilhali tunaona. Walianza na Mod tajiri (Richmond) wakaja na Do once (Dowans) tumewakalia kimya...ilipokuja ya Mbagala tukasema ni bahati mbaya wengine tulipoteza ndugu zetu tunasamehe sasa imerudia tena??
 
Mjomba wangu mdogo ana miaka minne alianza kuniabia uncle radi hiyo,nikamwambia uncle hakuna radi ,akaniambia tena uncle radi nikambishia kumbe ni mabomu yanalipuka nipo Sinza lakini muungurumo ni mkubwa.Leo nimejifunza kutoka kwa uncle wangu wa miaka 4 kuwa usidharau unapoambiwa kitu ati kwa kuwa anayesema ni mtoto mdogo au ni mtu unayemuona hana maana,kwani naamini ningemsikiliza uncle wangu na kumtilia maanani ningebaini kuwa kuna jambo lisilo la kawaida linatokea NA SASA KAMA KAWAIDA WAKUBWA WETU WATAUNDA TENA TUME YA KUCHUNGUZA CHANZO CHA KULIPUKA MABOMU GONGO LA MBOTO,SIJUI ILE YA MWANZO YA MBAGALA IMELETA TIJA GANI AU NDIO WATU WATACHUKUA PA DIEMU NA KUISHIA ZAO
 
Hii ni hatari kwa kweli, sipati picha wakazi wa gongo la mboto hali yao ikoje?

Khali yao itabidi tumuulize mzee Rais wa kuchakachua yeye na viongozi wake wa kiitelijensia kama hapo kulikuwa na cdm wakiandamana au laa...
 
Back
Top Bottom