Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Naishi Gongo la Mboto mpaka sasa sijaiona familia yangu

Benno Mwitumba
 
Eti msemaji wa jeshi kasema wakae maeneo ya mabondeni, mh! Source: Channel 5

Mimi nilitegemea at the very least basi angalau tungekuwa na timu ya kushughulika na majanga, so ingekwenda sasa angalau kuwaelekeza watu jinsi ya kuhama, wahamie wapi, usalama wa mali wanazoacha, jinsi ya kuwasaidia wazee, watoto , wakina mama wajawazito na logistics zote zinazohusu relocation wakati wa maafa. Hatuna plan, hatujifunzi na hatutataki kukosolewa. Naona hapa ndiyo starting point ya kudai serikali iwajibike kwa hili janga. Hatuwezi kuendelea kutangaza siku za maombolezo, kuvaa vitambaa vyeusi au kutuma salamu za rambi rambi wakati wenye kutakiwa kuwajibika wanaburudika na mvinyo.......
 
obhbd.jpg


Courtesy of J Makamba
 
Jamani, mnakumbuka mwinyi alisema atajiuzulu? Khe khe.... Hafanyi hihyo.... Ni kinyume na maumbile
Kwa serikali ya JK wanavyopena kubebana kujiuzulu wanaona kama vile sio hatua sahihi
 
Yaani ule upuuzi wa Mbagala umejirudia????
Vipi kuhusu INTELIJENSIA YA IGP MWEMA haijaweza kubaini hiyo milipuko???
Vipi kuhusu ULINZI shirikishi???
Yaleyale ya RICHMOND/DOWANS,umeme wa DHARURA. Kila kitu ni dharura kwa Tanzania.

Hapo ndipo tunapozidi kujua UDHAIFU WA SERIKALI YA CCM. Kuwa hawa jamaa hawana akili kabisa na wala huwa hawapendi kufikiri. Kwanini baada ya matukio ya Mbagala hawakuchukua TAHADHARI ya kufanya ukaguzi wa ARMOURY ZOTE KAMA KUNA HATARI MILIPUKO MINGINE KAMA HII??

Safari hii tunataka WATU TUANDAMANE NCHI NZIMA KUSHINIKIZA DR. MWNYI ajiuzulu. Last time Mbagala alikomaa kuwa HAWEZI KUACHIA NGAZI. This time tuseme basi!!!!! You poor Tanzanians wake up please! Acheni kuzubaa,watakaouwawa na hayo mabomu ni ndugu zenu,jamaa zenu na rafiki zenu!!!

ANGALIZO: Nahisi kama vile kuna njama ya kulipua makusudi haya MABOMU ili kuwafanya Watanzania wasahau sakata la DOWANS NA MGAWO. Kwamba wakti watu wanatafakari hayo Maboumu ya G/Mboto MAFISADI WAPATE NAFASI YA KUKAMILISHA MIPANGO YAO YA KULIPA ILE 94b/=kwa DOWANS na wakti huohuo WAKIENDELEA KUWASHA MITAMBO YAO(DOWANS)!!!!!!

Lazima kuna mtu anayachokonoa maksudi au labda mabomu ya ki-expire yanalipuka yenyewe? Manake nashindwa kuelewa miaka yote hio ndio yaje kulipuka mwaka jana na mwaka huu kwa mfululizo?

Hile ripoti ya mbagala ilikuja na sababu gani sijui ,kama mtu anaijua naomba jibu tafadhali.

Maombi yangu yote kwa watanzania wenzangu Mungu hawalinde popote mlipo.
 
Nitashangaa kama baadhi ya watu hawataachia ngazi hata kwa jambo kama hili. Ni maboom yanaendelea kulipuka hadi sasa. Eti wanatushauri tukakae mabondeni wakati hata hawasemi yataisha saa ngapi. Jamani hii ni serious sana wananchi hawana cha kufanya wala hamna directions zozote za maana kutoka kwa wahusika.
Thubutu...waachie ngazi? Hakuna kitu kama hicho! Kibaya zaidi hata hivyo vikosi vya uokoaji sijui kama vinafanya kazi.
 
mimi naishi huko na namshukuru Mungu nimeiokoa familia, WANAJAMII SIJIELEWI NA HALI NI MBAYA SANA, TUWAOMBEENI WENZETU. NIMEENDESHA GARI BILA KUJIELEWA KUIOKOA MY FAMILY,, TUONEENI HURUMA. nchi hii siielwewi kabisa.
am strongly condemning to the current govt of Tanzania kwa adha iliyotufika.
I see, pole sana mkuu!
 
Yaani bado yanalipuka, kwa nini wameweka mabomu mengi hivi mjini kwenye makazi ya watu?
 
wadau naingia jamvini muda huu nikiwa ni muathirika wa mambomu na nilikuwa huko na ndipo napoishi, nimeendesha gari pasipo kujijua na sijui nyumba yangu itasalimika ama la, imenilazimu niingie jamvini niwape hali halisi na si kuhadithiwa, NI HATARI SAANA WADAU.
Sasa rasmi ninailaani serikali hii, ni adha kubwa na nimeiharibu mpaka gari kwa hamaki ya kuinusuru my family.
 
mungu ibariki Tanzania...Zidumu fikra sahihi zinazotuepusha na majanga kama haya ya milipuko ya mabomu, mgao wa umeme, kukosekana kwa maji,madawa mahospitalini, kupanda kwa bei za:- petrol, diesel, mafuta ya taa, nyanya, samaki, kunde, nazi, mapera... Kidumu chama cha mapinduzi kwa kudumisha amani na mshikamano kwa watanzania...
 
Back
Top Bottom