Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Awa wakazi wa Gongolamboto ambao at this time wapo Tazara,nna washauri waendelee mojakwamoja mpaka Ikulu.wakomae apo mpaka serikali iwathibitishie kama longolongo za Mbagala azitotokea kwao vinginenvyo wameliwa

Nafikiri huu ni ushauri mzuri sana .........hivi wananchi hatuweziungana na kuupinga uzembe huu?? Tuwawajibishe wahusika.......... (mbona wanachuo wanadare?? ...........ah Tuandamane bana wawajibishwa hawa...........!!
 
Jamani we are praying for you our fellow Tanzanians......may God protect you!
 
This is no longer bearable. This gov has to go. Why did they not learn from mbagala experience? Kuna nchi nyingine uzembe kama huu unatokea?
 
Mabomu bado yanaendelea kulipuka, vikosi vya jeshi vinazuia magari kupita, wanahamasisha watu waondoke huko, na wanaomba watu wasiende huko. Kambini ndiko yanapolipuka mabomu. Barabara zote zimefungwa, kuna nyumba zinawaka moto. Umeme umezimwa eneo lote la Gongo la Mboto. Hakuna anayeweza kusogea ndani ya kambi. Hata vikosi vya polisi na jeshi lenyewe wapo mita 200 kutoka kwenye kambi.

Deogratius Rweyunga Redio one sterio!!
 
Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....

Taarifa zaidi kufuatia.

UPDATES: (by Invisible)

1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!

2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.

3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii

4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari

5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:

"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.

6. Picha ya tukio kwa mbali sana...

obhbd.jpg

shimbo badala ya kufanya kazi za jeshi akaingia kuitetea ccm sasa ajue maana ya kutotawalika kwa nchi ndio huku kama kila baada ya muda mnaua wananchi kwa uzembe hivi habari za kintelejensia ziko wapi kwa hili
 
Mabomu yanalipuka Gongo la Mboto polisi....

Taarifa zaidi kufuatia.

UPDATES: (by Invisible)

1. Hali ni mbaya jijini Dar, nyumba zinabomoka, watu wanakimbia ovyo!

2. Barabara ya Nyerere haitembei (kama unafikiria kwenda uwanja wa ndege ahirisha mapema), magari yameingiliana watu wanakimbia ovyo mitaani na barabarani kulikimbia eneo la maafa.

3. Dalili zinaashiria mabomu ni mengi zaidi na milipuko itaongezeka, kuna uwezekano wa kupoteza raia na watumishi (wanajeshi) wengi kufuatia milipuko hii

4. Watu kadhaa wamekufa kwa kugongwa na magari

5. Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Abdulrahman Shimbo amesema:

"Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi.

6. Picha ya tukio kwa mbali sana...

obhbd.jpg
poleni Sana Mungu awalinde
 
hao wataalamu wa mabomu wanapita wapi kwenda kuchunguza kama si kutegua?
 
Mimi niko mtoni kijichi ninaona miale ya moto na mitikisiko havi nyumba inavibrate, Taarifa za uhakika ni kuwa mabomu yanalipuka kambi ya Jesjhi Gongolamboto.
Shimbo alikemea wakati wa uchaguzi kazi isiyokuwa yake yeye ndie mnadhimu mkuu walijifunza nini mbagala na leo kumetokea nini? Mwamnyange, Shimbo na waziri wenu hii ndio kazi yenu. Mnatakiwa kuachia ofisi za umma mara moja kwa kusababisha Maafa, Hasara na usumbufu kwa watu.
 
badala watume wanajeshi wakaokoe watu, wanawashauri watu wakakae kwenye mabonde, kumbe kukaa mabodeni kuna faida!?[/QUO
mvua zikija ndo watahamishwa huko mabondeni na kulaumiwa kwa nni wameenda kuishi mabondeni-yaani hii nchi hata haieleweki
 
Nawaonea huruma sana Watoto, vikongwe na wenye ulemavu wa viungo. Mungu wasaidie viumbe wako hawa
Usiombe yakakukuta ndugu yangu halafu upo na watoto, unaweza ukakurupuka ukafika hadi buguruni ndio ukakumbuka umemsahau mtoto gongo la mboto, inasikitisha!
 
DESTRUCTION... Hosea 4:6 " Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa "
 
Wanajeshi nao wameamua kufisadi nchi kutokea mezani kwao.

Siamini kabisa kwamba hii ni bahati mbaya. Miripiko hii imeanzishwa kwa makusudi kabisa katika jitihada za kuficha ukweli wa mambo.


Theory number 1-Fedha za kununulia Silaha wametia ndani, au hawakununua kabisa au wamenunua kidogo ili kuficha wizi na ubadhirifu wameamua ku anzisha moto na kuteketeza kila kitu.

Theory number2-Silaha nyingine wameuza huko Congo na South Sudan. Kuua so wameamua kuyaunguza ili kufuta ushahidi.
Jeshi letu JWTZ limejihusisha sana na migogoro inayozunguka Tanzania kwa kufanikisha biashara haramua ya silaha.

Theory number 3- Katika hatua ya kujikita zaidi kwenye ulingo wa Siasa za Kiharamia Edward Lowassa na Rostam Aziz wamechukua sehemu kubwa ya Bunduki, Risasi na Mabomu ili kuimarisha MAFIA yao tayari kutwaa kiti cha Urais mwaka 2015 na kujenga Himaya ya MAFIA Tanzania.

DUDE linazidi kupata nguvu.
 
Yaani ule upuuzi wa Mbagala umejirudia????
Vipi kuhusu INTELIJENSIA YA IGP MWEMA haijaweza kubaini hiyo milipuko???
Vipi kuhusu ULINZI shirikishi???
Yaleyale ya RICHMOND/DOWANS,umeme wa DHARURA. Kila kitu ni dharura kwa Tanzania.

Hapo ndipo tunapozidi kujua UDHAIFU WA SERIKALI YA CCM. Kuwa hawa jamaa hawana akili kabisa na wala huwa hawapendi kufikiri. Kwanini baada ya matukio ya Mbagala hawakuchukua TAHADHARI ya kufanya ukaguzi wa ARMOURY ZOTE KAMA KUNA HATARI MILIPUKO MINGINE KAMA HII??

Safari hii tunataka WATU TUANDAMANE NCHI NZIMA KUSHINIKIZA DR. MWNYI ajiuzulu. Last time Mbagala alikomaa kuwa HAWEZI KUACHIA NGAZI. This time tuseme basi!!!!! You poor Tanzanians wake up please! Acheni kuzubaa,watakaouwawa na hayo mabomu ni ndugu zenu,jamaa zenu na rafiki zenu!!!

ANGALIZO: Nahisi kama vile kuna njama ya kulipua makusudi haya MABOMU ili kuwafanya Watanzania wasahau sakata la DOWANS NA MGAWO. Kwamba wakti watu wanatafakari hayo Maboumu ya G/Mboto MAFISADI WAPATE NAFASI YA KUKAMILISHA MIPANGO YAO YA KULIPA ILE 94b/=kwa DOWANS na wakti huohuo WAKIENDELEA KUWASHA MITAMBO YAO(DOWANS)!!!!!!

inteligensia inapata habari kuhusu maandamano ya chadema lakn si mambo muhmu kama haya! Yaan acha tu. Oh my dear TZ
 
Jamani hizi TV zetu as if hakuna kilichotokea wenyewe ni mamuvi tu na masoap operas, kama hakuna uwezekano wa kupata picha hata sauti tupu inatosha, hakuna mwenye akili timamu anaweza kuenjoy muvi na soap opera saa hizi! we want to know whats going on right now, kucopy na kupaste kumezidi
 
Back
Top Bottom