Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

barabara imefungwa-wanajeshi wapo-nyumba zinawaka moto,mabomu bado yanalipuka,umeme umezimwa
source-radio one
 
Kambi 511..............Rweyunga yupo huko.........nyumba zinawaka moto Rweyunga anaripoti akiwa amelala chini. Umeme umezimwa na watu wanatakiwa waondoke
 
Radio One:

bado viazi vinalipuka.

nyumba zinawaka moto.

umeme umezimwa.

walio kwenye magorofa wameagizwa washuke.
 
HIVI WANAUSALAMA WAPO KWA ajili ya nchi AMA NI KWA VIONGOZI TU? iWAJE HAYA YATOKEE? I hate these guys to the extent, yaani nimeshuhudia mambo ya Iraq ndani ya TZ yangu kweli????
 
Hivi askari wanaoishi katika kambi hiyo na familia zao wako vipi hivi sasa!
 
Nawaonea huruma sana Watoto, vikongwe na wenye ulemavu wa viungo. Mungu wasaidie viumbe wako hawa
 
au mubaraka ndio kaamia rasmi bongo kama mkimbizi watu wanahamishwa kiaina ... na kwanini wampeleke gongo la mbototo na siyo oysterbay
 
Si mnaona Libya tayari kinaanza kueleweka bado mkwere tu ye ndo kwaanza anatafuta pozi kuwatuliza kuwa wasijaribu kuiga wenzao wa Tunisia,Algeria,Egypt na Lybia.
 
wanajeshi wanasema uchunguzi ukishafanyika ndo watajua chanzo cha mlipuko
 
badala watume wanajeshi wakaokoe watu, wanawashauri watu wakakae kwenye mabonde, kumbe kukaa mabodeni kuna faida!?
 
kuna kipande cha bomu kimetua ubungo mpaka magari yaelekeayo barabara ya morogoro yalitikisika.watu wa tabata waliliona likipita!MWAMUNYANGE NA MWINYI WASIPOJIUZULU KESHO NITAJUA KWELI VIONGOZI WA AFRIKA HAWAAMBILIKI!

Thubutu! Hawatajiudhuru ng'o. Kwani wananchi wa kawaida wana thamani gani?
 
Tanzania tunaukimbilia umaskini.
1. Umeme mgao , hakuna wawekezaji atakeye thubuti kujenga kiwanda chake ktk mazingira kama haya, labda wezi ndio watakuja.
2. usalama mdogo ( mabomu kama hivi). ni kufukuza wawekezaje pontential ( lukuki ndoo watakuja).
3. utashangaa mkweer atakavyo toa comment zake za kipuuzi na kejeli kwa hili tukio.
4. tusipo chukua hatua ni janga la kitaifa.
 
Ugumu mwingine kwa raia na wadau wengine ni hili giza litokanalo na mgao wa umeme na athari ya mabomu. Wakati ule ilipotokea milipuko ya Mbagala kuna mtu aliniambia: "Sijui ingekuwa usiku kungekuwaje?".
 
Mbona hayaishi jamani, nyumba yangu iko hatarini watoto wanalia. Ni mazito mno

Mungu akulinde mpendwa. Sikia hii,MHE.SPIKA HAWA CDM WAMEZIDI, WAMEONA TUMEWADHIBITI KUCHOCHEA MAANDAMANO YA RAIA, WAMEANZA KUCHOCHEA MAANDAMANO YA MILIPUKO YA MABOM GHALANI! C.C.M wataitikia :kweeeeliiii tuwatenge.
 
hivi maji ya kuwasha hayawezi kuzuia mabomu kulipuka ... au ni kwa ajili ya kuwatesa wananchi tuu

Na inashangaza nchi masikini huduma muhimu kwa wananchi hakuna lakini kwa silaha kama mabomu, rada za kijeshi na maji ya kuwasha kuwatesa wananchi fedha hapo zinapatikana....
 
mi natamani kama yangekuwa yamejengwa karibu na makazi ya rostam,kikwete,lowasa,makamba,mwema,andengenye

sijui nyumba ya jirani yetu pale pugu mh.pinda nayo kama imesalimika.
 
Awa wakazi wa Gongolamboto ambao at this time wapo Tazara,nna washauri waendelee mojakwamoja mpaka Ikulu.wakomae apo mpaka serikali iwathibitishie kama longolongo za Mbagala azitotokea kwao vinginenvyo wameliwa
Ahahahahaaah!! Wazo zuri sana hili
 
Back
Top Bottom