Gerson Msigwa: Tozo kwenye Miamala ya kutoa pesa bado ipo

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa, leo Julai 8, 2023 amesema kuwa tozo kwenye miamala ya kutoa pesa haijafutwa.

"Tozo imefutwa kwenye utumaji ama usafirishaji wa fedha kupitia kwenye mifumo, ukituma wewe fedha kupitia kwenye simu yako kwenda kwenye simu nyingine, ile tozo tuliyokuwa tunaipigia kelele imefutwa, lakini ukienda kutoa fedha kwenye ATM ama kwa wakala ipo" amesema Msigwa.

Pia, amebainisha kuwa lengo la Serikali ni kuhamasisha uchumi usiotumia fedha taslimu ambao dunia ya sasa inahama huko pamoja na kupunguza gharama za uchapishaji wa noti ambapo serikali hutumia fedha nyingi.

Awali, JamiiForums kupitia jukwaa lake la Jamii Check, Julai 6, 2023, ilitoa pia ufafanuzi huu ulioungwa mkono na msemaji wa Serikali hii leo.

Tozo za miamala ya kieletroniki zilizofutwa ni;
  1. Unapomtumia mtu muamala kutoka simu yako kwenda simu ya mtu mwingine.
  2. Unapohamisha fedha kutoka akaunti yako ya Benki kwenda akaunti nyingine.
  3. Unapohamisha fedha kutoka akaunti yako ya Benki kwenda kwenye simu yako.
Pia soma: KWELI - Tozo za kutoa pesa kwa wakala na ATM bado hazijafutwa
 
Sabato Njema

Mshangao wangu ni kuwa, ilipowekwa watu walifurahia, imefutwa watu wale wale wamefurahia
Waliofurahia ni hawa 👇👇👇 usijumuishe na wengine!

IMG_20220330_194603.jpg
 
Nadhani wameona idadi ya watu wanaotuma kutoka kwenye akaunti zao imepungua.

Wengi tulikua tunamtumia wakala kudeposit moja kwa moja.
 
Imesaidia kwa KIASI kikubwa kwa sababu mtumaji ALIKUWA anakatwa tozo na mpokeaji pia anakatwa tozo imesaidia kwa KIASI fulani
 
Et,"..ile tozo TULIYOKUWA tunaipigia kelele imefutwa".-Msigwa.

Mrema Lyatonga akihama CCM alidai kilichomtoa huko ni unafiki kwamba yeye kama Mrema,Kitwana Kondo hafai kuwa Mayor wa jiji la DSM ila yeye Mrema kama mwanaCCM, Kitwana Kondo anafaa.
 
Ni ujanja tu. Yaani mtumuaji pesa hatozwi lakini mpokeaji pesa hiyo anatozwa au siyo?

Halafu mshahara unakatwa PAYE halafu unaapekelwa benki. Huko benki ukenda kuchukua unatozwa. Yaani mshahara mmoja unatozwa kodi mara mbili, au siyo?

Tuwe wakweli badala ya kubabaisha
 
Back
Top Bottom