Gavana Balali Ajiuzulu!

Gavana Balali Ajiuzulu!

Kama kuna nchi inahitaji msaada wa hali ya juu basi ni Tanzania.

Hii nchi inahitaji kuombewa sana kwa watu wanadini.

Pia nchi hii inahitaji msaada wa kuwezesha viongozi kutoa maamuzi yenye kuokoa Taifa.

Mijadala, Mifisadi, Matatizo yaliyopo yanaonesha kumulemea kiongozi mkubwa wa nchi.

Balali Pamoja na mbio zote za kujiokoa lakini siku hizi dunia ni kama ni ndogo mno.

Kujificha Marekani ni sawa na kufichama kwenye nyumba yeye kuta za vioo.
 
Kama kuna nchi inahitaji msaada wa hali ya juu basi ni Tanzania.

Hii nchi inahitaji kuombewa sana kwa watu wanadini.

Pia nchi hii inahitaji msaada wa kuwezesha viongozi kutoa maamuzi yenye kuokoa Taifa.

Mijadala, Mifisadi, Matatizo yaliyopo yanaonesha kumulemea kiongozi mkubwa wa nchi.

Balali Pamoja na mbio zote za kujiokoa lakini siku hizi dunia ni kama ni ndogo mno.

Kujificha Marekani ni sawa na kufichama kwenye nyumba yeye kuta za vioo.

Mimi nilidhani wengine wanaionea gere Tz kutokana na umoja na utulivu! Ukienda haswa West Afrika ukitamka Tz basi watu wanakuassociate na Mwal. na watakupenda!

May be Tz sasa kunajdili mno negative aspects kama za Balali n.k tusione hata moja jema!
 
Jamani Watanzania wenzagu issue ya mafisadi isije ikatotoa kenye wajibu wetu wa kufanya kazi kwa bidii, kwa muda mrefu zaidi na kwa maarifa zaidi, naona hizi hoja za Balali na wengine zinashamiri as if wao tu! ndio wanasabisha uchumi kudorora!Mbona haya yapo South Africa, Kenya lakini kwa kuwa uchumi wao ni mkubw hawaathiriki kiasi kikubwa kama kataifa ketu haka tumaskini, kenye watu wasiopenda kufanya kazi,wanaosubiri serikali iwatengenezee business plan, iraise capital, wakabiziwe tu biasdhara. BMW Alianza kuwapasha Watanzania, ENL anaendelea kuwaambia watu kwamba maisha bora yanaetwa kufanya kazi, ila nasikitika Rais wa sasa bado anaweka mazingira ya kwamba serikali itawafanyia. i'm very disapointed maana hata nchi zilizoendelea wananchi wake wanazalisha kwa kiasi kikubwa hivyo wanalipa kodi kubwa/nyingi, na kodi hii inaimarisha huduma za kiuchumi na kijamii!
 
Mwenye nondo azilete. What was the political or economical circumstances at the time of Rutihinda and Kibona's deaths?
 
Kilitime,
Hili swala la mafisadi kamwe haliwezi kutuondoa ktk wajibu wetu kama litakubalika kuwa ni kinyume cha sheria na hatua kali zitachukuliwa kwa mwenye kuvunja sheria. tatizo la Bongo ni kwamba hawa mafisadi wanaonekana kama ni heroes ambao wameweza kupenya serikalini na kuiba mali za Umma kisha wakapewa immunity na serikali yenyewe.

Swala la kusema haya maswla yapo dunia nzima ni upoteshaji kwani hata Majambazi wapo dunia nzima, Ubakaji na kadhalika ni vitu ambavyo vipo lakini vimetungiwa sheria kuhakikisha kuwa binadamu tunakuwa na control fulani ya madhara haya. lakini tunaposimama hapa na kuyaona ni mambo ya kawaida basi kesho usije kuanza kulalamika kwa nini kila mwananchi anakimbilia siasa ukasahau kuwa hakuna mtu asiyependa Utajiri wa haraka na hasa mahala unapopewa immunity na serikali yenyewe.
South Africa, Kenya na kwingineko kote huwaweka hatiani wahalifu na mpango wa kubebana ndio huzua husda,fitna na kutoelewana matokeo yake sote tutasimama kuzalisha tukitamani kushika nafasi hizo za Utajri wa haraka.
Kumbuka tu kuwa sisi binadamu ni wanyama wenye hisia zote za kinyama isipokuwa tumepewa akili za kuweza kuchagua mabaya na mazuri. Sasa leo tukianza kuhalalisha mabaya na kuyatungia sheria za uhuru tokana na legal obligations, basi mjomba tumekwisha!
 
[B]Ripoti ya Benki Kuu sio Wiki Ijayo sasa imekuwa JANUARI/08,Kwa nini kila siku Tarehe zinapelekwa mbele! Kuna nini kinafichwa hapa,endelea kusoma maneno ya CAG,kama yalivyonukuliwa kwenye gazeti la majira;
[/B
]
*CAG akadhiwa ripoti ya mwisho ya uchunguzi
*Aahidi kutobadili chochote kilichoainishwa
*Asema ataifikisha kwa Rais Kikwete kama ilivyo
* Kukadhiwa wiki ya kwanza Januari mwakani

Na Mwandishi Wetu

WAKATI utata wa kujiuzulu kwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Daudi Balali ukiendelea kutanda, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amepokea ripoti ya mwisho ya uchunguzi wa ubadhirifu ndani ya benki hiyo uliofanywa na Kampuni ya Ennst & Young.

Taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam na kusainiwa na CAG, Bw. Ludovic Utouh, ilieleza kwamba ripoti hiyo imepokelewa baada ya rasimu ya awali ya uchunguzi huo kupokelewa Novemba 27 mwaka huu.

"Kama ilivyoelezwa kwenye taarifa hiyo, ripoti iliyopokelewa ilikuwa ni ripoti ya awali ambayo ilifanyiwa kazi na ofisi yangu na kurudishwa kwa wataalamu walioifanya kazi hii ili kukamilisha ripoti hii. Huu ni utaratibu wa kawaida wa kufanya kazi za ukaguzi hasa ikichukuliwa maanani kuwa Kampuni ya Ernst & Young, imefanya kazi hii kwa niaba yangu," alisema Bw, Utouh.

Katika taarifa hiyo, Bw. Utouh, alisema mbali na uchunguzi wa 'EPA Account'ya Benki ya Tanzania, hadidu za rejea za kazi hiyo ziliwataka wachunguzi kurejea ukaguzi wa hesabu za BoT za mwaka 2005/06, kazi iliyofanywa na Kampuni ya Hesabu ya TAC Associates ikishirikiana na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

Alisema wachunguzi hao wametakiwa kutoa ripoti mbili tofauti moja ikiwa ni ya 'EPA Account' na nyingine ikihusu rejea ya ukaguzi wa hesabu za BoT kwa hesabu za mwaka 2005/06.

" Hivyo basi, napenda kutoa taarifa rasmi kwa Watanzania wenzangu ya kuwa nimepokea kutoka Kampuni ya Ernst & Young taarifa za mwisho za uchunguzi, siku ya Jumapili Desemba 23 (jana ). Kwa sasa nazipitia ripoti hizi mbili ili kujihakikishia usahihi wa yaliyomo kabla ya kuwasilishwa kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete katika juma la kwanza la Januari, 2008 baada ya kumaliza likizo yake, alisema Bw. Utouh.
 
MKJJ,

naelewa concern yako................however, kama amekabidhiwa ripoti ni wajibu wake aipitie ajue kilichomo pengine Ernest & Young wanaweza kuwa wameacha mambo muhimu....................kumbuka ripoti ya kwanza kule MOI iliyopelekwa kwa Prof Mwakyusa..........na hata ikabidi alete tume nyingine ndio angalau waliweza kufanya mambo ya uhakika...

In short unalipa Consultant baada ya kuridhika na kazi yao......hivyo Utouh ni lazima aipitie na kuridhika ndio awalipe final amount
 
Tunasubiri mshangao mkubwa!.. nina hakika hakuna kitu chochote kinachohusiana na madai ya Dr. Slaa kuhusu mafisadi kwani kama JK yumo ktk list haiwezekani akapelekewa yeye report hiyo.
Je, ni lini JK ataweza kuzikosha nyoyo za Watanzania kwa kuwahakikishia kuwa yeye ni SAFI? Kwa nini asiunde tume maalum itakayo chunguza madai ya Dr. Slaa kwani mashirika na watu waliotajwa ktk report ya Dr. Slaa - YAPO/WAPO na kuwepo kwake ni ushahidi tosha kuanzisha uchunguzi.
 
Kilitime,
Hili swala la mafisadi kamwe haliwezi kutuondoa ktk wajibu wetu kama litakubalika kuwa ni kinyume cha sheria na hatua kali zitachukuliwa kwa mwenye kuvunja sheria. tatizo la Bongo ni kwamba hawa mafisadi wanaonekana kama ni heroes ambao wameweza kupenya serikalini na kuiba mali za Umma kisha wakapewa immunity na serikali yenyewe.

Swala la kusema haya maswla yapo dunia nzima ni upoteshaji kwani hata Majambazi wapo dunia nzima, Ubakaji na kadhalika ni vitu ambavyo vipo lakini vimetungiwa sheria kuhakikisha kuwa binadamu tunakuwa na control fulani ya madhara haya. lakini tunaposimama hapa na kuyaona ni mambo ya kawaida basi kesho usije kuanza kulalamika kwa nini kila mwananchi anakimbilia siasa ukasahau kuwa hakuna mtu asiyependa Utajiri wa haraka na hasa mahala unapopewa immunity na serikali yenyewe.
South Africa, Kenya na kwingineko kote huwaweka hatiani wahalifu na mpango wa kubebana ndio huzua husda,fitna na kutoelewana matokeo yake sote tutasimama kuzalisha tukitamani kushika nafasi hizo za Utajri wa haraka.
Kumbuka tu kuwa sisi binadamu ni wanyama wenye hisia zote za kinyama isipokuwa tumepewa akili za kuweza kuchagua mabaya na mazuri. Sasa leo tukianza kuhalalisha mabaya na kuyatungia sheria za uhuru tokana na legal obligations, basi mjomba tumekwisha!

Mkuu Mkandara,

Heshima kwako,,, post yangu haina maana kwamba siwachukii wahujumu uchumi, nawachukia sana tena sana!!! lakini kwa kweli Tatizo la Watanzania wanaweza kujitetea kwamba hao ndio tu wanawarudisha nyuma!!!,,, wakati pia hatufanyi kazi!!! Tanzania Tuwavivu mno Mkandara... hili haliwezi kuondoka kwa kupigia kelele wahujumu uchumi!!!,,, ukombozi wa nchi hii ni kufanya kazi!!!
Kambarage alilijua hili muda mrefu sana uliopita ndio maana akaanzisha slogan "UHURU NA KAZI" akimaanisha uhuru kamili wa taifa hili utaletwa na wananchi kufanya kazi na kupunguza utegemezi kwa wajomba wa IMF na WB.
 
[B]

"Kama ilivyoelezwa kwenye taarifa hiyo, ripoti iliyopokelewa ilikuwa ni ripoti ya awali ambayo ilifanyiwa kazi na ofisi yangu na kurudishwa kwa wataalamu walioifanya kazi hii ili kukamilisha ripoti hii. Huu ni utaratibu wa kawaida wa kufanya kazi za ukaguzi hasa ikichukuliwa maanani kuwa Kampuni ya Ernst & Young, imefanya kazi hii kwa niaba yangu," alisema Bw, Utouh.

.


Mpiga zumari ndiye mchagua wimbo. Tulidhani ni ripoti huru ya uchunguzi ambayo imeagizwa na CAG kwa maana ya kuchukuliwa kama ilivyo kumbe ni ripoti nyingine ya CAG ambayo amemtuma EY kufanya kwa niaba yake! Ndio, ni utaratibu wa kawaida kwa mtu ukimpa kazi kama hiyo kwa niaba yako kuipitia. Na ni utaratibu huo huo unaoweza kumpa maelekezo, hiki weka hiki ondoa, hivi weka hivi ili ripoti iwe na sura hii kwa malengo haya. Sasa ni wakati wa utaaluma wa EY kuwekwa kwenye jaribio- je, watafanya kazi yao kitaaluma na kusimamia utaaluma hata kama anayewalipa ana matakwa tofauti au watakubaliana naye na kufunika kombe mwanaharamu apite? Kupelekwa ripoti ya awali mapema na kuchukua muda mrefu bila kurudishwa kwa ajili ya kutoa ripoti ya mwisho kuna maelezo matatu tu: Ama ofisi ya CAG ni wavivu wanafanya kazi taratibu, au EY ni wabovu walifanya kazi mbaya ambayo ilihitaji maelekezo na maelezo marefu kabla ya kuwarudishia kuleta ripoti ya mwisho au Ripoti ilikuwa na mambo ambayo hayapendezi mbele ya umma kwa hiyo ilibidi CAG atumie muda mrefu kutoa maelekezo ya kuipendezesha ripoti. Nasema hivi kwa kuwa ni CAG mwenyewe na serikali ndio walisema ripoti ingekamilika siku nyingi lakini yani yani zinaendelea mpaka hii leo. Njia pekee ni kuisaka kwa udi na uvumba ripoti origanal ya awali ya EY na kuiweka hadharani kabla au mara baada ya ripoti iliyohaririwa na serikali ya Kikwete ya CCM kuwekwa hadharani

JJ
 
Mpiga zumari ndiye mchagua wimbo. Tulidhani ni ripoti huru ya uchunguzi ambayo imeagizwa na CAG kwa maana ya kuchukuliwa kama ilivyo kumbe ni ripoti nyingine ya CAG ambayo amemtuma EY kufanya kwa niaba yake! Ndio, ni utaratibu wa kawaida kwa mtu ukimpa kazi kama hiyo kwa niaba yako kuipitia. Na ni utaratibu huo huo unaoweza kumpa maelekezo, hiki weka hiki ondoa, hivi weka hivi ili ripoti iwe na sura hii kwa malengo haya. Sasa ni wakati wa utaaluma wa EY kuwekwa kwenye jaribio- je, watafanya kazi yao kitaaluma na kusimamia utaaluma hata kama anayewalipa ana matakwa tofauti au watakubaliana naye na kufunika kombe mwanaharamu apite? Kupelekwa ripoti ya awali mapema na kuchukua muda mrefu bila kurudishwa kwa ajili ya kutoa ripoti ya mwisho kuna maelezo matatu tu: Ama ofisi ya CAG ni wavivu wanafanya kazi taratibu, au EY ni wabovu walifanya kazi mbaya ambayo ilihitaji maelekezo na maelezo marefu kabla ya kuwarudishia kuleta ripoti ya mwisho au Ripoti ilikuwa na mambo ambayo hayapendezi mbele ya umma kwa hiyo ilibidi CAG atumie muda mrefu kutoa maelekezo ya kuipendezesha ripoti. Nasema hivi kwa kuwa ni CAG mwenyewe na serikali ndio walisema ripoti ingekamilika siku nyingi lakini yani yani zinaendelea mpaka hii leo. Njia pekee ni kuisaka kwa udi na uvumba ripoti origanal ya awali ya EY na kuiweka hadharani kabla au mara baada ya ripoti iliyohaririwa na serikali ya Kikwete ya CCM kuwekwa hadharani

JJ

unadhani ni Rahisi?Nachokijua ambacho Muungwana amewaagiza watu wa Usalama Wa taifa,document ambayo imeandikwa SIRI,basi mtu akiivujisha ajue anapoteza kazi na kushughulikiwa kwa sheria za nchi,kuna usiri mkubwa katika kupata ripoti za serikali hasa zilizonadikwa ni siri.
 
Mpiga zumari ndiye mchagua wimbo.

JJ

Mnyika,

Umesahau kidogo. Huwa inasema "He who pays the piper calls the tune!"

Na ndicho kinachotokea hapa. Hawa Ernst and Young si tume ya kitaifa au tume huru au kitu kama hicho. Ni wafanyabiashara waliopewa tenda.
 
unadhani ni Rahisi?Nachokijua ambacho Muungwana amewaagiza watu wa Usalama Wa taifa,document ambayo imeandikwa SIRI,basi mtu akiivujisha ajue anapoteza kazi na kushughulikiwa kwa sheria za nchi,kuna usiri mkubwa katika kupata ripoti za serikali hasa zilizonadikwa ni siri.

Watapoteza mara ngapi, mbona tayari imeshavuja na wakati muafaka ukifika itawekwa hapa. Kinachosubiriwa sasa hivi ni hiyo ambayo serikali itatoa ili zilinganishwe na kama itakuwa tofauti basi kuna mtu si tu atafukuzwa kazi bali pia atapelekwa mafia na kufia huko!
 
Watapoteza mara ngapi, mbona tayari imeshavuja na wakati muafaka ukifika itawekwa hapa. Kinachosubiriwa sasa hivi ni hiyo ambayo serikali itatoa ili zilinganishwe na kama itakuwa tofauti basi kuna mtu si tu atafukuzwa kazi bali pia atapelekwa mafia na kufia huko!

Duh! Wakuu JF haiwezekaniki! Yani siwawezi kabisa! Safi sana hii. Hebu iwekeni hapa tumkome nyani fastafasta, ili hata kama anataka kuifanyia "doctoring" aone aibu mwenyewe.
 
Mwafrika mke na wengine salaam za Noel toka Mwigobero Musoma . Naelekea kuvua samaki sasa . Napenda kuunga mkono kwamba hata mimi nimepata copy ya report siku kama 10 nyuma sasa nangoja kuona watasema nini . Hakuna cha siri watu wamechoka .Tunayo but we cannot pre empty tunangoja .
 
Nadhani walio nayo watatupa zawadi ya Mwaka Mpya. Merry Xmas to you all.
 
Mwafrika mke na wengine salaam za Noel toka Mwigobero Musoma . Naelekea kuvua samaki sasa . Napenda kuunga mkono kwamba hata mimi nimepata copy ya report siku kama 10 nyuma sasa nangoja kuona watasema nini . Hakuna cha siri watu wamechoka .Tunayo but we cannot pre empty tunangoja .

Mhhhh,

Merry chrismas nawe pia.....
kwi kwi kwi kwi, Yaani wewe Lunyungu nimecheka sana kusikia hilo jina Mwigobelo. Hivi umetunga au kuna sehemu hapo Tanzania na huko musoma inaitwa hivyo....kwi kwi kwi kwi kwi...

Haya baba, mimi niko mbali sana na niko limited kwa internet lakini imebidi nirudi tu hapa nikujibu haraka haraka. Hii report ishavuja siku nyingi na Kikwete anazani kuwa bado ni siri!

Endelea kuitunza ili tuwaaibishe wakileta usanii wao..

Asante nawe pia!
 
Nadhani mtandao (Internet) imekuwa mhimili wa nne wa Dola.Pale Mahakama, Bunge na Serikali wanaposhindwa kuwajibika na kuwaelimisha wananchi, basi mtandao unaweza kuchukua nafasi hii.
The report is in wish list. Kudos kwa Father Xmas atakayetupatia zawadi hii nzuri.
 
Back
Top Bottom