Gavana Balali Ajiuzulu!

Gavana Balali Ajiuzulu!

hata mimi tayari ninayo, nilichosubiri ni huo ubabaishaji wa serikali.
 
Mnyika,

Umesahau kidogo. Huwa inasema "He who pays the piper calls the tune!"

Na ndicho kinachotokea hapa. Hawa Ernst and Young si tume ya kitaifa au tume huru au kitu kama hicho. Ni wafanyabiashara waliopewa tenda.

Kithuku

Nashukuru...

Kweli aiseee, nimesahau maneno- tafsiri sahihi: Alimpae mpiga zumari ndiye mchagua wimbo!

JJ
 
hacheni kuimba nyimbo za father chrismas,mnasubiri nini mtakuja kuta mtoto sio wenu, eti kulinganisha kwani mnacomper price,wekeni vitu wao ndio waje walinganishe hapa.
 
Yaani, kama kuna kitu kilicho tangulia furaha yangu ya sikukuu hii, ni pamoja na kupata tetesi hizi kwamba tayari original document iko mikononi mwa wapiganaji!

Sasa ole wao walete ambayo ndiyo siyo!! Patakuwa hapatoshi! hata mawe yatasema.

Yaani nimefurahi mno!
 
Kithuku

Nashukuru...

Kweli aiseee, nimesahau maneno- tafsiri sahihi: Alimpae mpiga zumari ndiye mchagua wimbo!

JJ


bado hujapatia amlipae sio alimpae, pupa ya nn mkuu, taratibu ktk uandishi unaharaka utadhan i unaiba!!
 
unadhani ni Rahisi?Nachokijua ambacho Muungwana amewaagiza watu wa Usalama Wa taifa,document ambayo imeandikwa SIRI,basi mtu akiivujisha ajue anapoteza kazi na kushughulikiwa kwa sheria za nchi,kuna usiri mkubwa katika kupata ripoti za serikali hasa zilizonadikwa ni siri.

Huwezi kuficha siri ya wizi! Any plot that is against national interest does not qualify to be a national secret. Hao usalama waulizwe, kwa nini mkataba wa Buzwagi, Richmond nk nayo ilikuwa siri lakini tulipoitoa hawajatukamata? Kwani nyaraka za BOT alizoanza kuanika Dr Slaa nyingine si siri, mbona usalama wa taifa hawamkamati hususani kwa kuwa na ripoti yao ya usalama wa taifa waliyompelekea Lowassa ambayo imeandikwa SIRI kwa herufi kubwa? Siri inaweza kuwa kati ya wezi na wezi, lakini hakuwezi kuwa na siri kati ya wezi na wenye mali! Binafsi sijaipata hiyo ripoti, ila nimepata shauku zaidi ya kuitafuta.

Nami nawatakia wote Noeli na Mwaka mpya wenye upendo, furaha, jitihada na mafanikio.

JJ
 
mie nnaona hakuna alie nayo maneno tu.

kwa kimbele mbele cha jamvi hili utadhani mimba ingekuwa ishwekwa dahari.

hayo majigambo tu hamna lolote
 
Imwageni hapa sasa kumbe kila Tom, Dick and Harry (at least within the esteemed JF Community) anayo mnasubiri nini?
 
Vuteni subira kuna haja ya kuilinganisha na nyingine kwani kuna ripoti mbili moja kutoka kwa E&Y na nyingine kutoka kwa mdhibiti mkuu wa serikali , mambo yatakuwa hadharani muda sio mrefu sana .
 
mie nnaona hakuna alie nayo maneno tu.kwa kimbele mbele cha jamvi hili utadhani mimba ingekuwa ishwekwa dahari.

hayo majigambo tu hamna lolote

Mtu wa Pwani, mdhalau mwiba..
Hapa JF mwisho wa Lami.. Yaani ni kukoma nyani mchana kweupeeeeee!! Ole wenu mafisadi siku zenu zinahesabika, kila aliye mwema kawachoka, ndo maana sirizenu za wizi nje nje!
 
mnyika ukweli hakuna alie nayo hiyo ripoti hadi sasa kama ingekuwepo ingeshawekwa zamani.

barua ya balali iliwekwa mapema kabla hata tetesi hazijaenea.

ingeekwa kwa mbwembwe na majitapo ila mkuu debe tupu tu hilo wacha lipige kelele.


nnakupongeza kwa kuwa mkweli.

nnawatakia Xmas njema nyote
 
Back
Top Bottom