Mkuu Jasusi,
Heshima mbele, nakumbuka kule nyuma ulimwambia Masanja, kuwa when the time is right ukweli utajitokeza na kumsafisha gavana, na mimi siku zote nilisema kwamba lets give it a time kujua ukweli wote kabla ya kumhukumu gavana, nakumbuka Mwafrika wa Kike alivyonitwanga, lakini nika-maintain kuwa gavana apewe time, now here comes this news za yeye kujiuzulu kama ilivyotabiriwa, tena akiwa nje ya nchi!
Sina wasi wasi na ukweli wa barua ya Mzee MMJ, kwa sababu najua ameipata wapi, mkuu kwa kweli ninasubiri what you have to say na this topic kwa ujumla!
Mkulu FMES,
Heshima mbele mkuu, nimekuwa alerted na system kuwa unataka nikupe jibu la niliyosema hapa last time. Sitakuwa na muda mwingi sana wa kujibu maana matumizi ya internet nilipo sasa hivi yako very limited. Mengine zaidi nitajaribu kukujibu jumatatu au baada ya krismams.
Nilikubaliana nawe kuwa Balali anaweza kuwa na pesa zake za kutoka na ajira yake ya WB. Nilipingana nawe kuwa, mshahara wa Balali wa WB hautoshi kumfanya jamaa amiliki majumba kibao na biashara kibao anazomiliki ndani na nje ya nchi. Document zipo na achive yangu na ya Mzee Mwanakijiji inazidi kupokea nyingi zaidi.
Balali sasa hivi ni bilionea ile mbaya, swali je hizi pesa zote ametoa wapi? Unajua kwa nini Balali ameshindwa kufanya alichofanya yule Githongo wa Kenya?
Inawezekana Balali hakupata mgawo mkubwa kwenye skendo ya Meremeta na zingine zilizomweka Kikwete madarakani ila naye ana skendo zake kibao tu ambazo kama akiwasema kina Kikwete basi RO na vijana wa usalama watamwaga file la Balali (wameanza kumwaga sasa hivi ndio maana watu kama sisi tunapata vitu kibao vya balali) ili naye apoteze.
Balali sio safi, anahusika moja kwa moja na ule wizi wa BOT kama Dr Slaa alivyosema kwenye report yake. Kama angekuwa safi angekataa (kumbuka Rutihinda na Kibona) au angefanya chochote kuwazuia Kikwete na the company wasichote mabilioni na kutumia kwenye uchaguzi.
Alternative nyingine aliyonayo ingekuwa ni kufika tu marekani na kuwapigia simu waandishi wa washington post au 60 minutes (ambao so far wanaaminika kwa kutunza siri) ili aseme story yake na baada ya hapo hata mafia hao wa bongo wangeogopa kummaliza.
Mimi na memba fulani hapa JF tumemtafuta Balali tuongee naye na ikiwezekana tumuunganishe na waandishi wa habari hapa US lakini jamaa hataki na anaogopa kila mtanzania aliyeko marekani. Kuna mawili hapa, Balali ni mwizi na anaogopa kuwataja wezi wenzake au Balali anaogopa kila mtu wakiwemo waaandishi wa habari.
So far, hakuna uthibitisho wowote ambao barua yake ya kujiuzulu itaonyesha kuwa Balali ni msafi, labda kama unao mkuu uuutoe..
Otherwise uwe na sikukuu njema na mwaka mpya wenye mafanikio..
Samahani kama sitajibu haraka hoja zako niko mbali sana na ulimwengu wa fast life ya marekani sasa hivi!