Fursa ya ufugaji wa ng'ombe wa asili kwa ajili ya nyama na maziwa kwa maeneo yaliyokaribu na soko

Wajasilimali wenzangu msije mkasema sijawaambia,iko hivi kama una shamba karibu na Dar,maana ya Mkuranga, Bagamoyo nk fikiria mradi huu unalipa.Nimeiba idea hii kwa jirani yangu kupitia meneja wake nikaone ni FURSA muhimu.

Iko hivi kwa mfano;
Kama una eneo lako hata kama ni ekari moja tu ya shamba na uko eneo ambalo jirani zako wana shamba ambalo hawaliendelezi, basi unaweza kutumia fusra hii kubadili maisha yako.
Mchanganuo wa biashara hii ni kama ifauatvyo

A: INVESTMENT COST
1.Nenda Mikoani nunua mitamba 80,000 kwa 250,000@ = = 20,000,000
2.Nunua madume 4 ya kisasa au Boran ambayo yataanza kupanda baada ya mwaka @ 300,000 = 1,200,000
3.Ujenzi wa Zizi na Nyumba ya mfanyakazi (Lumpsum) = 2,000,000
4.Mabomba ya kuogeshea 2 na Vifaa tiba @ (Lumpusm) = 200,000
JUMLA = 23,400,000
B: RUNNING COST

1.Mishahara ya wachungaji 2 Sh 200,000 X miezi 12 = 2,400,000
2.Walinzi 2 x 200,000 X Miezi 12 = 2,400,000
3.Madawa ya kuogesha na Tiba 50,000 X Miezi 12 = 600,000
4.Chakula wafanyakazi (Sembe +maharage) 100,000 Miezi 12 = 1,200,000
5. Supervisor 300,000 x miezi 12 = 3,600,000
6.Dharula 50,000 X miezi 12 = 600,000
JUMLA 10,800,000
JUMLA KUU A + B 34,200,000


BAADA YA MWAKA MMOJA

-Ngombe 70 watatoa 140 litres X 1000/= Sawa na 140,000/day 4,200,000 /month sawa na Tsh 50,400,000/YR
-Baada ya Miaka 3 utauza ng'ombe 50 X 700,000 35,000,000/YR

NOTE
Hii ina maana baada ya mwaka 1 unarejesha hela yako imerudi na faida ya kutosha. Hakikisha unampata meneja/Supervisor mzuri na umpe motisha ukifika hatua ya kutengeneza faida. Swala la ulinzi na afya ya mifugo lichukulie kwa umakini mkubwa sana. Ninae andika hii hoja ni mtoto wa mfugaji wa ng'ombe wa asili na sasa mfugaji wa ng'ombe wa kisasa..Uzoefu 100%

Hayo ni maoni yangu.

Karibuni kwa maoni.
Huyu Motivation Speaker kama umemlipa hela kamwambie arudishe na mangumi juu.

Kakudanganya sana tu tafuta wafugaji tukueleze siyo huyo motivation atakudanganya utupie mtaji wako wote ujinyonge bure.

Kwanza mtamba wa 250000/=unaupata wapi ?
Zagamba la Boran upate kwa 300000/=?
 
mkuu unaweza kwenda kujifunza ila utalipa, google githunguri dairy farmers, ikom karibu na mji mkuu nairobi kaa chini ya 100km hivi, wakulima toka kenya mzima wanenda hapo kujifunza, all the est mkuu, ningekueleka israel ukajifuze zaidi ila sijui uwezo wako wa fedha
Ada shngap?na wanajifunza kwa mda wa cku ngap,au miez mingap?
 
Ada shngap?na wanajifunza kwa mda wa cku ngap,au miez mingap?
wabongo bhana eeeh, yaani unataka ufanyiwe kila kitu, shida iko wapi ya kugoogle hio kamupuni na mambo yote iko katika website yao, hata nambari za simu, saduku za posta na wengine mengi tuache hii uvivu toka nae, kwa ajili ya kujenga taifa
 
Huyu Motivation Speaker kama umemlipa hela kamwambie arudishe na mangumi juu.

Kakudanganya sana tu tafuta wafugaji tukueleze siyo huyo motivation atakudanganya utupie mtaji wako wote ujinyonge bure.

Kwanza mtamba wa 250000/=unaupata wapi ?
Zagamba la Boran upate kwa 300000/=?
Mkuu tembelea minada ya mikoani utakubaliana na bei hii..kuhusu dume la laki 3 nimeshauri uchukue dogo llliloacha kunyonya..hiyo ndio bei na mimi nimeuza sana wa aina hii
 
Back
Top Bottom