Finally: Hongereni Wana-CCM Online!!

Status
Not open for further replies.
Samahani kwa hilo Kaka,

Kwanza sikujua kwamba nina uwezo huo; Pili sikujua kumbe mbali ya kutoa hoja, pia wewe ni moderator na unaona mjadala naupeleka kusipo takiwa; Basi nimekuelewa naacha kuchangia kwenye uzi huu, na naomba wale wote ambao nimewaudhi kwa njia moja ya nyingine mnisamehe; Niwie radhi kaka, ila kumbuka - huu ni mgongano tu wa mawazo, na msukumo wangu sio kitu kingine zaidi ya uchungu juu ya jinsi gani chama chetu kinazidi kupotea, huku sisi vijana tukipigia debe malengo ya wazee ambayo ni ya muda mfupi sana, kwani in 10-15 yrs watakuwa hawapo tena katika siasa za nchi hii na watatuachia chama mfu au chenye migogoro mikubwa zaidi ya hii;

Hoja zangu humu hata kama zitakuwa zimekuudhi, naomba uelewe tu kwamba zililenga kujadili jinsi gani tunaweza kukirudishia chama chetu cha CCM hadhi yake ya zamani kwa kuangalia uhalisia wa mambo (sio ignorance and arrogance just because tumekamata dola), and in the process, mgongano wa mawazo ni jambo la kawaida; Nakuachia mjadala wako kwa moyo safi kabisa;

Na kuhusu wewe kuwa kiongozi wa taifa, mimi sijashindwa bali nimekataa kuwa mtumwa; kaulize;

Kila la Kheri;

Alamsiki;

wewe ni kada wa chama gani labda,maana hata mimi sasa umeanza kunichanganya,mwanzoni nilikua nakuona kama unafanya kazi nzuri ya kukikosoa chama chako wewe mwenyewe kwa nia ya kukijenga kwa kujkifanya kijirekebishe badala ya kuwaachia kazi hiyo wapinzani,lakini sasa unakwenda mbali zaidi na kunifanya nianze kukutazama kwa jicho la tahadhari,pengine unatumika kwa malengo maalum,otherwise vua joho la ccm nenda upinzani tuelewe moja kuliko kuuma uma maneno,ccm sio mamako ulikutana nayo barabarani na unaweza kuachana nayo huko huko kuliko kuendelea kuteseka nayo wakati unaamini haiwezi kusimama tena,nenda kajiunge na timu ya ushindi,tena mungu amekujalia una uwezo mkubwa sana wa kuandika,kupanga maneno na kushawishi,upinzani una safu nyembamba ya uongozi nenda kaongeze nguvu kule ili utupe changamoto sisi wafuasi wa chama mfu lakini kinachpendelea kukubalika na watz
 


Hapa nadhani waislam watakujibu, ilikuwaje Mtume Muhamad kuoa mtoto wa miaka 9!
Sio binti mtoto wa miaka tisa.

Miaka ya 1989/90...Mwenyekiti wenu by then alioa binti mwanafunzi wa Jangwani Sec.School. Dar yote iliwasikia mabinti wa Janwani, Kisutu, ZAnaki nk. wakimwita mkuu pale ikulu shemeji yao.

Labda ni sawa, sheria ya ndoa inasemaje. Rais awe mkwale? Mwenye vimada kila kona, kila kabila,kila race?

Hii habari ya mtoto wa jangwani una uhakika nayo lakini?au ulisikia tu watu pale kijijini kwenu wakiisema sema na wewe ikakukaa?je ni mtoto wa nani labda?
 
[h=2]Re: Finally: Hongereni Wana-CCM Online!![/h]Napendekeza kama inwezekana Mods wabadilishe title iwe "HONGERENI WA-TZ WAPIGANIA MABADILIKO & UKOMBOZI WA FIKRA" maana siwaoni hao Wana-CCM wanaopongezwa kwa kujibu hoja online. Au wana mgomo hawajalipwa posho zao nini?
 
- ha! ha! ha! ha! ha! ha! chama chetu hakipotei labda unapotea wewe tu ndugu yangu, sasa ninaanza hata kuelewa unatokea wapi kumbe ni wewe duh!! unajua sana kujificha ficha, ha! ha1 ha!

Le Mutuz!!

William J Malecela, hata siku moja sijaona unamwaga sera za Chama cha Mapinduzi na kuzichambua kama Mchambuzi anavyofanya, ila unakazana na nyimbo zile zile za kusifia na kuiimba CCM huku kwa nguvu zote ukikazania kuwanyoshea vidole viongozi wa Chadema. Uchaguzi Mkuu ujao watakapocast vote wapiga kura watapigia CCM kuimbiwa nyimbo nzuri au sera zake? Unaitangaza Chadema bila kujijua.

Unaweza kubadili kidogo tabia na kuonyesha ukomavu wa kisiasa kwa kuanza kumwaga sera na kuzijadili hapa?
Unaonekana hata mambo yaliyomo ndani ya Katiba huyajui hata wenzako akina Ritz na Chama kwa kuendeleza mipasho tu, kwa sababu hata nukuru moja kwamba "nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko." Rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa." Amini kuna tatizo hapo, haiwezekani wengi hivyo hata waliokuwa best wako wakugeuke, kuna kitu unatakiwa jipime vizuri, CCM ni chama, lakini viongozi ndio tatizo na wewe huko huoni tatizo la kukosoana kama katiba ya chama inavyotaka. Hapo ni tatizo. Kama kuchaguana viongozi CCM ni kupitisha mtu mwenye utetezi na mtazamo wa aina yako kuendelea kushika dola ni ndoto ya kufikirika.
 
".........Wakati huna mke" KWANI Mh SLAA ANA MKE? Wewe kweli umechanganyikiwa.

Wewe ndo nadhan una kichaa cha period...Dr Slaa katoka wapi katika haya mazungumzo..kilichotushtua ni ile kuhamaki baada ya kuona front page ya gazet ikiwa imemwanika akiwa na malaya badala ya kutoa maelezo akakimbilia kusema mie sio shoga jamani, mimi ni bachelor! Inatia mashaka kwa kweli,ikumbukwe ana miaka 51, alikua baharia amesafiri maeneo mbali mbali kama Mombasa, Uturuki,nchi za falme za kiarabu,marekani mashaka yanatuzidia.
 
Makamanda wana-reason kwa kutumia hoja na sio eti wasubiri kuambiwa na mtu wakati wana macho, vichwa ambavyo havifungi nywele bali vinachanganua mambo. Mtu ana miaka hamsini wewe unasema ni kijana eti kisa alikuwa USA, hilo linahitaji kuambiwa kwamba sio kijana. Hapo ndo uone tofauti ya ushabiki wa ki-CCM na wapenda mabadiliko, mmoja anasubiri aambiwe wakati huyu mwingine anachunguza na kutafuta ufumbuzi wa jambo na kutoa hoja ya alichokiona. Bado, hamwoni kuwa hii ni tofauti kubwa, ni kama miaka mitano iliyopita CDM walichunguza wakaona kupunguza gharama za ujenzi inawezekana, na kuandika katiba mpya inawezekana lakni CCM waliona haiwezekana waliona hali iko sawa tu, hili ni kundi linalosubiri kuambiwa, ona sasa karibu miaka mitano baadae CCM ndo wanaona Elimu bure inawezekana, gharama nafuu kwenye vifaa vya ujenzi eti ndo wanaona inawezekana, tatizo la kusubiri uambiwe, akili zimefunikwa na gamba hazioni mbele.

Wewe kama unajitambua bado kijana na Willy anajiona bado kijana tatizo lipo? Usimlazimishe mtu na uzee kuna watu wanaweza kukuona mzee na huo umri wako wa miaka 31; siku akitaka kuwa mzee hatakusubiri wewe umwambie. Tatizo lenu makamanda mna mambo ya kulazimisha sana

Chama
Gongo la mboto DSM

Haya amueni wenyewe na W.J. M wenu na miaka yake hamsini eti kwa sababu alikuwa US, SHAME ON HIS & YOUR HEADS, halafu na yeye lizee lizima eti anajiona kijana...!!!!

"To begin with, youth can begin as early as elementary school and last until the legal age of 21.

During the 1950's, there was a well-known song, "'Twixt Twelve and Twenty," which defined youth as being that age group.

In some cases, 25 may be the demarcation between youth and adulthood because that is the age at which one can run for federal office (House of Representatives or the Senate).

Some people may consider the possession of a driver's license the line of demarcation. This varies from state to state, but generally 16 is the age at which one can get at least a conditonal license.

In most states, the legal drinking age is 21.

One can join the military at 18; however younger persons are allowed to do so with parental permisson.

Anyone below the age of 35 is considered by the U.S. Constitution to be too young to run for President of the United States.

If you want a personal opinion, I'd say that anyone below 11 is a child. Twelve and 13-year-olds are pre-teens. Those between 14 and 25 are the nation's youth. I'd call most people between 26 and 35 "youthful adults." Of course, these ages all assume a normal range of emotional and mental development."
 
wewe ni kada wa chama gani labda,maana hata mimi sasa umeanza kunichanganya,mwanzoni nilikua nakuona kama unafanya kazi nzuri ya kukikosoa chama chako wewe mwenyewe kwa nia ya kukijenga kwa kujkifanya kijirekebishe badala ya kuwaachia kazi hiyo wapinzani,lakini sasa unakwenda mbali zaidi na kunifanya nianze kukutazama kwa jicho la tahadhari,pengine unatumika kwa malengo maalum,otherwise vua joho la ccm nenda upinzani tuelewe moja kuliko kuuma uma maneno,ccm sio mamako ulikutana nayo barabarani na unaweza kuachana nayo huko huko kuliko kuendelea kuteseka nayo wakati unaamini haiwezi kusimama tena,nenda kajiunge na timu ya ushindi,tena mungu amekujalia una uwezo mkubwa sana wa kuandika,kupanga maneno na kushawishi,upinzani una safu nyembamba ya uongozi nenda kaongeze nguvu kule ili utupe changamoto sisi wafuasi wa chama mfu lakini kinachpendelea kukubalika na watz

Nilisha aga mjadala huu kutokana na mtoa mada kuingiwa na jazba kama wewe lakini naomba nirudi kuweka hili sawa; Kwanza ninachofanya hapa hakipingani na kanuni zetu za chama; mimi ni mwanachama wa CCM kwa miaka kumi na nane ninayeamini katika kanuni zote, na kinachoniangusha ni utekelezaji mbovu wa kanuni zetu ambazo laiti tungekuwa tunazingatia, tusingekuwa katika matatizo haya;

Ibara ya (5) ya Mwongozo (1982) Inasema: Kujikosoa na kukosoana ni silaha ya Mapinduzi

58. Kuna mambo mawili tuliyojifunza ambayo ni muhimu pia kuyazingatia. La kwanza linahusu suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana kama njia ya kukijenga na kukiimarisha Chama na wanachama. Ni kweli kuwa katika TUJISAHIHISHE Mwalimu anasisitiza jambo hili na kwamba Katiba ya CCM inatamka waziwazi juu ya umuhimu wake. Lakini ni kweli pia kuwa hatujaijenga tabia hii ipasavyo. Mara nyingi tumependelea kuteteana, kufichiana makosa na hata kutafuta visingizio visivyo na msingi.

59. Suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana lina sura kadhaa. Kwanza linataka wanachama na viongozi kuwa tayari kusema kweli katika vitendo vyao na kukubali kuambizana ukweli. Pili, linataka wanachama na hasa viongozi wawe tayari kukosolewa bila kuhamaki na inapobidi kukubali kujirekebisha. Tatu ni kuwa Chama chenyewe katika vikao vyake vya ngazi mbalimbali kuwa na utaratibu wa kujikosoa.

---
Baina yangu na wewe, nadhani mimi nipo kwenye mstari zaidi kwani sina unafiki tofauti na wewe ambae unasukumwa na ukaribu wako na makada wa chama mnao kunywa pombe pamoja kama unavyotuadithiaga humu;
Kabla ya kunirudia, naomba usome Kitabu cha chama chetu alichotoa mwalimu 'TUJISAHIHISHE' halafu urudi tujadiliane kwa hoja kwani kati yangu na wewe, kuna kila ishara kwamba kwanza haujui maana ya chama cha siasa ni nini, pili haujui maudhui ya kuunda chama hiki (CCM) yalikuwa ni nini, na tatu, unasukumwa na ushabiki kuliko uzalendo kwani hauyumbishwi na tatizo lililopo la CCM kusaliti historia yake yenyewe; Iwapo una tabia ya kupenda kusoma, nakurahisishia kazi, soma maneno ya Mwalimu hapa kisha unirudie kwani anayosema mwalimu yanahusu wanachama na viongozi wa aina yako:

Katika kitabu chake cha ‘TUJISAHIHISHE' (1962). Mwalimu anasema:

["Ukiondoa matatizo wayapatayo binadamu kwa sababu kama mafuriko, nzige, kiangazi, n.k, matatizo yao mengi hutokana na unafsi. Unafsi ni wa aina nyingi. Swali ambalo twalisikia mara kwa mara, "Hali yetu ya baadae itakuwaje?", ni swali ambalo sina shaka kuna wanaouliza kwa nia safi kabisa. Lakini mara nyingi linatokana na unafsi. Mtu anayeuliza anafikiri TANU iliundwa kwa faida yake binafsi. Ni kama kwamba TANU ilipoundwa ilimwahidi kwamba ikiwa atakubali kuwa mwanachama, au kiongozi, basi TANU itamfanyia yeye jambo fulani kama tunzo!

Anasahau kabisa kuwa TANU inajishughulisha na haja za Jumuiya kwa ujumla. Lakini kwa mtu wa aina hiyo, hata kama TANU inatimiza madhumuni yake kwa jumuiya, ataona kuwa ni umoja ambao hauna maana kwa sababu haumtimizii haja zote za nafsi yake. Huu ni unafsi. Kama wanachama wa TANU, na hasa viongozi, hawatakihukumu chama chetu kwa mahitaji na nafsi zao wenyewe, chamaa hakitadumu. Wanachama wa aina hiyo ni ugonjwa katika chama.

Dalili nyingine ya unafsi, na ambayo ni ugonjwa mbaya sana ni fitina. Kanuni moja ya TANU inasema hivi: "Nitasema Ukweli Daima. Fitina Kwangu ni Mwiko." Lakini bado tunao wanachama ambao ni wafitini wakubwa bila kujitambua. Ni wa aina mbali mbali. Wengine humwona mwenzao anafanya kosa. Badala ya kumwambia pale pale kijamaa kwamba atendalo ni kosa, watanyamaza kimya. Lakini hawanyamazi kabisa. Watakwenda kumteta katika vikundi vya siri. Mateto haya si ya kumsaidia mwenzao, ni ya kumdhuru. Hii ni aina moja ya fitina. Wengine hugawa watu katika mafungu. "Fulani" japo kafanya kosa kubwa sana hasemwi. Lakini "Fulani" wa pili akifanya kosa japo dogo, kosa lile hukuzwa likawa kama mlima Kilimanjaro. Hawa hutafuta sababu ya kumtetea "Fulani" wa kwanza, au za kumaulumu "Fulani" wa pili, ambazo hazifanani kabisa na ukweli.

Kwa watu wa aina hii, ukweli ni jambo ambalo hutegemea mtu, si kitu kinachojitegemea chenyewe bila kujali mtu. "Fulani" wa kwanza akisema katika majadiliano kuwa mbili na mbili ni tano, wao watakubali. Lakini "Fulani" wa pili akisema sivyo, mbili na mbili ni nne, watamwona ni mtu mbaya kabisa ambaye hastahili hata kusikilizwa. Hawa hawajali ukweli, hujali nafsi tu. Kwao, ukweli ni maoni yao na matakwa yao. Hatuna budi, hasa katika majadiliano na mazungumzo yanayohusu jumuiya, tujifunze kusikiliza hoja zenyewe zinazotolewa na wenzetu, na kuzijibu zile hoja kwa kuzikubali au kuzikataa, bila kujali kama anaezitoa ni rafiki au si rafiki. Pia wanaopingwa hawana budi wakubali kuwa kinachopingwa ni zile hoja zao, sio wao wenyewe. Bila mazoea haya, mazungumzo hayana maana; yanakuwa ni kupoteza wakati, maana huwa tumekwisha kuzihukumu hoja za mtu hata kabla hajazitamka; kadhalika, hoja zetu zikijibiwa kwa kupingwa halafu tunawakasirikia waliozipinga tunafanya mazungumzo yasiwe na maana, kwa sababu tunapenda hoja zetu zikubaliwe tu hata kama si hoja safi.

Ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo; haujali adui wala rafiki. Kwake, watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwa.

Wakati mwingine, mtu tunayempinga huwa ana makosa kweli lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake. Nikisema mbili na tatu ni sita, nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nafikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha. Ni kweli mbili mara tatu ni sita; lakini mbili na tatu ni tano, siyo sit.a Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema kuwa meno yangu ni machafu, au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana. Huu ni mfano wa upuuzi; lakini mara nyingi hoja tunazotumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda, au kukubali mawazo yetu, huwa hazihusiani kabisa na mambo tunayoyajadili.

Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au unaotuzuia kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua hana makosa. Na msingi wa woga ni unafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine huwa hatuna tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake. Sisi sote tunayo tama hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza kumfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunawaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni unafsi mbaya sana Ni kweli kwamba demokrasi haiwezi kudumu ikiwa wachache watakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo wa wazi.

Kadhalika, matakwa ya wachache hujulikana katika majadiliano na mazungumzo. Bila wachache kusema wazi wazi matakwa yao, majadiliano hayana maana. Wakati mwingine, hata baada ya majadiliano, wachache – japo wamekubali kutii uamuzi wa wengi wanaweza kuendelea kuamini kwamba mawazo yao ni sawa, na ya walio wengi yamepotoka. Demokrasi inawapa haki, na ukweli unawapa wajibu wa kuendeleza mawazo yao mpaka wengi waone kuwa ni ya kweli. Bila hivyo Maendeleo katika mawazo hayawezekani, kwani mara nyingi wazo zuri hutokana na mtu mmoja tu. Mwanzo laweza likapingwa, pengine kwa nguvu kabisa, na walio wengi, lakini hatimaye wengi hulikubali. Huu ndio msingi wa Maendeleo katika mawazo ya binadamu.

Makosa ni makosa na dhuluma ni dhuluma, japo watendao makosa hayo au dhuluma ile ni wakubwa au ni wengi. Chama kinachopenda ukweli na haki hakina budi kiwape wanachama wake uhuru na nafasi ya kusahihisha makosa na kuondoa dhuluma. Wanachama hawana budi waone kuwa ni wajibu wao kuutumia uhuru huo, na nafasi hiyo. Wanachama wasiotumia uhuru huo na nafasi hiyo, kwa sababu ya kuogopa kuchukiwa au kupoteza nafasi zao, wanafanya kosa kubwa la unafsi, ambalo ni adui wa haki na ukweli.

Kosa jingine linalotokana na unafsi tunalifanya wakati wa kuchagua viongozi. Wakati mwingine hufanywa na wanachama; wakati mwingine hufanywa na viongozi wenyewe, au wale wanaotaka uongozi. Nimesema mahali pengine kwamba viongozi wetu hawana budi watokane na WATU. Viongozi wa TANU hawana budi watokane na wanachama wa TANU wenyewe, bila hila, vitisho, rushwa, au ujanja wa aina yoyote. Lakini mara nyingi wanachama huchagua viongozi bila kufikiri kwa makini kama viongozi hao wanaiweza, au hawaiwezi, kazi wanayochaguliwa kufanya.

Wanachama wetu watafanya makosa makuwa sana ikiwa watachagua viongozi wa ovyo tu. Hii ni jambo la hatari kwa demokrasi na chama chetu, na maadui wa TANU wanaweza kusema kwamba demokrasi haina maana kwa sababu haizai viongozi wanaoweza kazi zao. Hii ni kweli, maana wote twajua kwamba demokrasi inaweza kuchagua viongozi wazuri. Lakini ni wajibu wetu katika kuhifadhi demokrasi kuona inachagua viongozi ambao wanaziweza kazi zao. Kazi za kuchagua viongozi ni kazi ya wanachama wetu; lakini viongozi wetu wanaweza kusaidia kwa kuelezea wanachama wetu kwamba jambo la kuchagua viongozi ni kubwa sana. Haifai kuchagua kiongozi kwa sababu ni mjomba, au binamu au ana sauti au sura nzuri. Wala haifai kuacha kumchagua mtu kuwa kiongozi kwa sababu kama hizo. Jambo kubwa ni kuchagua kiongozi mwenye tabia nzuri na anayeiweza kazi. Hatuna budi tutii kanuni hii katika kuajiri wafanya kazi katika TANU au Serikalini. Hawa pia hawana budi wachaguliwe kwa sababu wanaiweza kazi wanayoajiriwa kufanya, na ni watu wenye tabia nzuri.

Kosa jingine ni kutojielimisha. Kanuni yetu moja inasema: "Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu wote na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote". Wengi wetu hufikiri kuwa kujielimisha ni kwenda Kivukoni, au kupata nafasi kwenda kusoma katika nchi za nje. Wengine hufikiri kuwa kujielimisha ni kujua kusoma na kuandika. Hilo ni kosa, lakini sio kubwa kama la pili. Wengi wetu, hasa baadhi ya viongozi, hufikiri kuwa tunajua kila kitu na hatuna haja ya kujifunza jambo lolote zaidi. Mtaalamu mmoja wa zamani alisema kuwa "mwanzo wa elimu ni kutambua kuwa haujui kitu."]

Unirudie kwa hoja ukifikia tamati ya Maneno haya ya Mwalimu;


 
wewe ni kada wa chama gani labda,maana hata mimi sasa umeanza kunichanganya,mwanzoni nilikua nakuona kama unafanya kazi nzuri ya kukikosoa chama chako wewe mwenyewe kwa nia ya kukijenga kwa kujkifanya kijirekebishe badala ya kuwaachia kazi hiyo wapinzani,lakini sasa unakwenda mbali zaidi na kunifanya nianze kukutazama kwa jicho la tahadhari,pengine unatumika kwa malengo maalum,otherwise vua joho la ccm nenda upinzani tuelewe moja kuliko kuuma uma maneno,ccm sio mamako ulikutana nayo barabarani na unaweza kuachana nayo huko huko kuliko kuendelea kuteseka nayo wakati unaamini haiwezi kusimama tena,nenda kajiunge na timu ya ushindi,tena mungu amekujalia una uwezo mkubwa sana wa kuandika,kupanga maneno na kushawishi,upinzani una safu nyembamba ya uongozi nenda kaongeze nguvu kule ili utupe changamoto sisi wafuasi wa chama mfu lakini kinachpendelea kukubalika na watz

sasa hii dhahiri ni jazba, mbona Mchambuzi anakosoa chama chake in bonafide ila wewe unatoa layman solution jumla jumla namna hii??
hebu punguza jazba mkuu.

Hatari:
Weka Mbali na Tembo.
 
Last edited by a moderator:
- ha! ha! ha! ha! ha!ETi least wananchi hapa wana uhakika kwamba mimi kiongozi wao wa Taifa sio shoga, maana siku hizi Dunia imeharibika sana mnachagua kiongozi wa taifa kumbe shoga! ha! ha! ha!

- But in me what you see is what you get, kudadeki yaani Kiongozi Rijali! ha1 ha! ha! ha!

Le Mutuz!!

Hizi ni hoja za mtu aliyepata kura 800 za CCM!! kweli kuna umbwe la uongozi huko
 
- Ahsante sana, ila ndugu yangu dalili za mvua huwa ni mawingu, uchaguzi wa udiwani majuzi ni ujumbe tosha kuhusu what to expect 2015 the budern is on the otherside sio kwetu CCM tena!!

Le Mutuz!!

Le Mutuz;CHADEMA viti vyao 2 vyote wamevitetea,CCM ktk viti 27 wao wamepoteza 5 bado mnajisifia kuwa mmefanya vyema?

Mmepoteza viti iweje muendelee kujisifu kama mmefanya vyema?Upo kwenye kamati ya propaganda za Mzee Tambwe?
 
mkuu Mchambuzi huyu @W.J. Malecela ni mmoja kati ya wanachama wa ccm anayekitia aibu chama chenu.

Hatari:
Weka Mbali na Tembo.

Pengine ndio tiketi yake ya kutafuta madaraka kwani humu anajisifia eti "hawezi kujibizana na wanachama ambao sio viongozi wa kitaifa kama yeye"; Hicho chama kwani kinatumikia nani, viongozi au wanachama wasio kuwa na uongozi kama yeye? Kwa mtazamo wake huu, ni dhahiri yeye na wengine wengi huingia CCM Kutafuta:

  • Social Status
  • Wealth
  • Prestige

Hawapo ndani ya chama kutumikia wananchi, hivyo ni vigumu sana kuelewana na watu wa namna hii kwa hoja;

Isitoshe, tumeshaona kwamba watawala huko CCM huwapa watu kazi au kuwapandisha vyeo kwa vigezo vifuatavyo:


  • Ignorance (hata kwa makusudi);
  • Irrationality;
  • Stubbornness (hasa kuwavunjia heshima wapinzani na wananchi wanaowaunga mkono);
  • Dishonesty;

Hizi ndio prefered features wanazoangalia watawala kabla hawajasema wewe ni mwenzao na unafaa; Kama hauna hizi sifa, sahau uongozi ndani ya CCM;

Tusije kushangaa Kaka yetu anateuliwa kuwa Mjumbe wa kamati kuu (CCM) kwani katika majibu yake kwangu katika bandiko moja, ameonekana kutukuza sana ukubwa alionao, na kwa sifa hizo hapo juu, hakika ataenda mbali sana ndani ya chama;
 
Very well said brother! You really are a great thinker!


Hivi Kaka William,

Unajua kwamba chama chetu kimesha meguka ndani kwa ndani siku nyingi na tuna vyama zaidi ya viwili kimtazamo na kimalengo ndani ya CCM? Kinacho kosekana ni usajili wa tendwa; Isitoshe, viongozi wengi ndani ya CCM hawafanya kazi tena kwa mapenzi ya CCM, na hii ni hatari kwani wanasukumwa zaidi na UWOGA, UBINAFSI na UNAFIKI, masuala ambayo mwalimu aliyajadili sana jinsi gani ni tishio kwa uhai wa Chama;

Mimi ni Mwana CCM lakini kwa akili zangu timamu, naelewa kwamba kwa sasa CCM bado ni moja kwa sababu ya System tu, hakuna lingine; Chama kinacholindwa na system ni chama dhaifu;

Ni muhimu tukai sambaratisha CCM sasahivi kama nia yetu ni kuijenga upya, kuliko kusubiri kuja kusambaratishwa na Upinzani, kwani siku hiyo haipo mbali;

Hoja yako ya kutetea Chama chenye kansa ya kiungo ni hoja mfu kwani unachofanya ni kutetea na kuwa mtiifu kwa chama kwa mujibu wa katiba, sio kwa mujibu wa uhalisia wa soko la Siasa; Kaka, Kansa imesha sambaa, tukate tu hicho kiungo na tuanze maisha mapya
 
W. J Malecela, akili ndogo iliyojengwa kwa jitu nene!! Utafiti mdogo tu wa chekechea unakushinda wewe na kundi kuubwa la ccm? Tangu general election 2010, kati ya ccm na CDM, who is the looser? Viti kwenu vimeongezeka? Au vimepungua? Hata hii ya viti 29, ccm ilikuwa inavitetea viti 26, CDM 2, Tlp 1 na Cuf 0. Matekeo ccm ilitetea 22 ikapoteza 4, CDM ilitetea 2 na kuongeza 3, Tlp ilitetea 1 na cuf iliongeza 1. Umeelewa? Kubwa jinga wewe!!
 
Re: Finally: Hongereni Wana-CCM Online!!

Napendekeza kama inwezekana Mods wabadilishe title iwe "HONGERENI WA-TZ WAPIGANIA MABADILIKO & UKOMBOZI WA FIKRA" maana siwaoni hao Wana-CCM wanaopongezwa kwa kujibu hoja online. Au wana mgomo hawajalipwa posho zao nini?

Si kila utumbo utaujibu mnauliza maswali yaleyale; kazi yenu ni kubadili ID; hapa tunafanya kazi kwa mapenzi yetu na CCM nyie wengi ndio mnaotegemea posho na kujipendekeza pale mtaa Togo. Hamna hoja ya kujibu wengi mnataka kulazimisha mambo kwasababu hoja hamna tunawaangalia macho; na isitoshe hii thread sio yenu tuwaachieni wenyewe wanaCCM kama mnatatizo na ujana wa Le Mutuz fungeni thread tuone kama hamtakimbia na kubadili ID zenu.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
- Nimeshindwa kusoma yote maana it is toolong daamn! however naomba kusema hivi kama unaaamini CCM itameguka basi wahi Chadema, kama unaamini CCM imemeguka tayari basi wahi Chadema, CCM ni treni inaondoka haiwezi kusimama, ninasema CCM itshinda mwaka 2015, hakuna atakayemeguka wala kutoka, Chadema best net ilikuwa Sitta labda angetoka, lakini Slaa amemkorofisha na kusema sana now hakuna hope tena!!

-
Le Mutuz!!

Ni mvivu wa kufiki peke yake anayeshindwa kusoma post iliyochambuliwa kama ile na haiyumkini, umejibu kitu usichokielewa sababu hukusoma post yote. Rudi kaisome kuanzia ulipoishia then uje uijibu upya
 
Pengine ndio tiketi yake ya kutafuta madaraka kwani humu anajisifia eti "hawezi kujibizana na wanachama ambao sio viongozi wa kitaifa kama yeye"; Hicho chama kwani kinatumikia nani, viongozi au wanachama wasio kuwa na uongozi kama yeye? Kwa mtazamo wake huu, ni dhahiri yeye na wengine wengi huingia CCM Kutafuta:

  • Social Status
  • Wealth
  • Prestige

Hawapo ndani ya chama kutumikia wananchi, hivyo ni vigumu sana kuelewana na watu wa namna hii kwa hoja;

Isitoshe, tumeshaona kwamba watawala huko CCM huwapa watu kazi au kuwapandisha vyeo kwa vigezo vifuatavyo:


  • Ignorance (hata kwa makusudi);
  • Irrationality;
  • Stubbornness (hasa kuwavunjia heshima wapinzani na wananchi wanaowaunga mkono);
  • Dishonesty;

Hizi ndio prefered features wanazoangalia watawala kabla hawajasema wewe ni mwenzao na unafaa; Kama hauna hizi sifa, sahau uongozi ndani ya CCM;

Tusije kushangaa Kaka yetu anateuliwa kuwa Mjumbe wa kamati kuu (CCM) kwani katika majibu yake kwangu katika bandiko moja, ameonekana kutukuza sana ukubwa alionao, na kwa sifa hizo hapo juu, hakika ataenda mbali sana ndani ya chama;
Mchambuzi;
Haya unayongea ni matusi kwa viongozi wetu; na sijui unatumia vigezo labda ningeshauri uje na mifano halisi; naona umeandika kijazba; CCM ni chama kinachojiendesha kidemokrasia si lazima ukubaliane na kila jambo linalofanywa na viongozi wa CCM; hizi tuhuma unazozitoa dhidi ya Le Mutuz ni character assassination ambazo hazina maana yoyote ile. Hapana hata mahali pamoja Le Mutuz ameonyesha eti anajikomba ili apate cheo kama hiyo ingekuwa tija Le Mutuz asingejitosa kwenye chaguzi mbalimbali pamoja na kwamba alishindwa kwenye baadhi ya chaguzi hakukata tamaa aliendelea kugombea na hatimaye kushinda; mtu anayetegemea vyeo vya kupewa hagombei; sina haja ya kukupa mifano ya vyeo vya kupeana Chadema ila nina hakika unayo na unaijua. Wapo makamanda wengi tu wanaitumia JF kama nguzo ya kujikomba na kina Dr. Slaa ili wapewe nafasi za uongozi kwani wameona siasa ndio njia pekee ya kujikwamua kimaisha; naheshimu sana michango yako ila kuwa mtafiti nilikuambia humu JF wengi hawapo kujifunza ni washabiki wanaotumiwa na Dr. Slaa na kukuthibitishia hilo wengi walijaribu kupindisha maneno ya kitabu kitakatifu Biblia wakidai Dr. Slaa hafanyi ZINAA wakati anaishi na mwanamke bila ndoa.

Chama
Gongo la mboto DSM
CC: Ritz, william
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom