Hivi kuna hoja gani ambazo CCM wamejibu zaidi ya kuleta vioja vya udini na ukabila tu?
-Watu wanapenda kujifariji kweli kweli.
Comrade.....
Ukweli ni kwamba siasa za Tanzania sasa hivi zimeingiliwa na hazina maana yoyote......Vyama (ikiwa ni pamoja na chama tawala, CDM na vingine) vimekuwa vikundi vya mipasho, havina tofauti na enzi zile za TOT Taarab (Khadija Kopa) na Muungano Cultural Troupe(Bi Nasma Khamis Kidogo - RIP)......Siku hizi vyama badala ya kueleza nini watawafanyia watanzania, vyenyewe ni kutupiana maneno ya kejeli, kutukanana na kila aina ya upuuzi.....Ni ajabu kuona CCM badala ya kueleza ni wamewafanyia watanzania katika miaka 50 ya Uhuru (ambavyo vipo na vinaonekana) wao wanakaa na kuisakama CHADEMA na viongozi wake......
Inashangaza pia kuona CHADEMA kama chama mbadala katika siasa za Tanzania badala ya kuutumia muda huu wa kuelekea mwaka 2015 badala ya kuwaeleza watanzania nini watawafanyia mara watakapochaguliwa wao nao kila uchao wamekuwa wakiisakama CCM na viongozi wao kila uchao.....Imekuwa ni mipasho tu kila kukicha.....
Ni ajabu kuona viongozi wa vyama vya kisiasa (hasa wa CCM na CHADEMA) wakitumia muda mwingi kukashifiana na kukashifu vyama vyao badala ya kuwaeleza wananchi sera na nini wamewafanyia/watawafanyia wananchi hao wa taifa hili maskini.....Hu si wakati wa viongozi wa CHADEMA kutumia muda mwingi kuelezea udhaifu wa sekretarieti mpya ya CCM, huu ni muda wa wao kujipanga na kwenda kwa wananchi na kuwaeleza nini watawafanyia mara watakapowachagua(kumwaga sera), huu ni wakati wa kwenda kuwatongoza wananchi, huu ni wakati wa kuwashawishi wananchi kujenga imani na chama hicho, kuisakama sekretarieti ya CCM na agenda isiyochuja ya ufisadi hakutakisaidia CHADEMA kuingia madarakani, CCM imekuwa dhaifu tangu mwaka 2005 baada ya mgawanyiko uliotokana na mtandao lakini bado imeendelea kushinda uchaguzi( wa Urais, wabunge na madiwani) na kuendelea kushika dola... Agenda ya ufisadi imeanza kuzungumzwa majukwaani tangu mwaka 2006 pamoja na kuwaingia watanzania bado haijawasaidia CHADEMA kisiasa......CHADEMA wanapaswa kuutumia muda huu(ambao kimsingi ilitakiwa ianze tangu baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010) kujiimarisha kisiasa na kujenga imani kwa watanzania kwa kuwaeleza nini watawafanyia pamoja na kujenga mtandano ulio imara kuanzia ngazi ya shina mpaka Taifa badala ya kutegemea ofisi na viongozi wa kujitolea kama ilivyo sasa......CHADEMA wanapaswa kutafuta ofisi na viongozi katika kila eneo la nchi hii (bara na visiwani) kuanzia katika ngazi ya Tawi mpaka mikoani na si kutegemea Operesheni Sangara, M4C n.k.....Kwa kufanya hivyo watakuwa karibu zaidi na wananchi......Kutumia muda mwingi kuelezea ufisadi wa viongozi wa CCM na serikali na kuiponda sekretarieti mpya ya CCM hakutakisaidia CHADEMA....Kama sekretarieti hiyo ni dhaifu ni bora CHADEMA wakatumia mbinu za kisiasa kuutumia udhaifu huo kujinufaisha kisiasa, kuisakama na kuiponda majukwaani ni dalili za KUIOGOPA..
Kwa chama changu CCM, kwa kweli sitofautiani na ndugu yangu Comrade
Mchambuzi .....Niko naye ukurasa mmoja kabisa, chama chetu kina matatizo mengi sana kiasi kwamba kwa walio karibu na siasa za ndani za CCM wanaweza kudhani kuna vyama zaidi ya vinne ndani ya CCM, kinachosababisha hali hii si kingine, ni makundi ya waroho wa madaraka (wanaoutaka urais) , rushwa pamoja na kulindana ndani ya chama... Makundi ndani ya chama ndiyo imekuwa kansa inayokitafuna chama kuanzia mwaka 2005 na kadri siku zinavyokwenda kansa hii imezidi kuwa sugu na sasa makundi zaidi yanaundwa kwa ajili ya kujipanga kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, hii ni hatari sana, haya tunayoyasikia ya Membe na Bashe ni manynyu tu, mvua kamili itaanza kuonekana/kunyesha mwaka 2014....Makundi haya yasipodhibitiwa(japo ni too late) yatakifanya chama kiwe na hali mbaya katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015...Hali hii ya makundi ipo hata katika ngazi ya Ubunge na Udiwani......
Kuhusu Rushwa ndani ya chama kwa sasa; ni miujiza pekee ndiyo inayoweza kutenganisha rushwa na uongozi ndani ya chama chetu hiki....Rushwa nayo imekuwa kansa ambayo tiba yake ni ngumu kupatikana......Sijajua ni mbinu zipi hasa mzee wangu mpiganaji na muadilifu Philip Mangula atazitumia katika kupambana na rushwa na wala rushwa ndani ya chama maana karibu asilimia 90 ya viongozi wa chama na wawakilishi(wabunge,wjumbe wa baraza la wawakilishi,madiwani,masheha n.k) wameingia madarakani kwa rushwa.....Nasubiria hiyo miujiza ya kuwaondoa waliopata uongozi kwa rushwa ndani ya miezi 6......Ila kiukweli nina imani sana na sekretarieti mpya ya CCM na nimefurahishwa na utaratibu unaotumiwa na Katibu Mkuu wa CCM Kanali(mstaafu) Abdulrahman Kinana kuzunguka na viongozi wa serikali katika mikutano yake na kuwabana mbele ya wananchi.....Hii inadhihirisha kwamba sekretarieti hiyo imekuja kikazi zaidi na si porojo.....
Ni matumaini yangu kwamba mzee Mangula kama Kiongozi wa maadili ndani ya chama atasaidia katika kuondoa tatizo la kulindana na kuwashughulikia viongozi na wanachama wasio waadilifu ndani ya CCM, na kwa kuanzia waanze na makatibu wa CCM wa wilaya na mikoa na baadae kwa wale wote wenye uroho wa madaraka ambao wanatumia muda mwingi kukidhoofisha chama kwa kuendekeza makundi ndani ya chama na kuzua mpasuko ambao unakigharimu chama na utazidi kukigharimu siku za usoni.......
Siasa si uadui.......Japo ni mchezo mchafu
Tutabanana humuhumu ndani ya CCM.....
Bala.