Ethiopia Wanasiasa Marafuku PhD Za Heshima

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
33,615
Reaction score
40,165
Wizara ya Elimu nchini Ethiopia imetoa Mwongozo mpya unaopiga marufuku Viongozi wa Serikali na viongozi wa Kisiasa nchini humo kutunukiwa Shahada za Heshima (Honorary Doctorate).

Agizo hilo ambalo limetiwa saini na Waziri wa Elimu Nchini Ethiopia Profesa Berhanu Nega kuwasilishwa kwa Vyuo vikuu na taasisi za Elimu nchini humo limezitaka taasisi hizo hususa ni Vyuo ambavyo Wanafunzi wake hawajahitimu angalau awamu nne na havitoi Shahada ya Uzamilivu havitoruhusia kutokoa shahada ya Heshima.
Mwongozo pia unaeleza kuwa Shahada za Heshima zinaweza kutolewa kwa raia wa Ethiopia au Wageni waliotoa mchango wa kipekee katika taaluma au nyanja zao za kazi. Tuzo hiyo inaweza kutolewa kwa mtu mmoja au kikundi kilicho hai au kilichofariki, mradi kimekidhi vigezo vilivyowekwa.

Aidha kuna masharti ya vizuizi Kifungu cha 2 Ibara ya 10 kimeeleza kuwa wafanyakazi wa kudumu wa vyuo vikuu, wajumbe wa Seneti au miundo ya uongozi hawawezi kupokea shahada ya heshima wakati bado wako kazini, isipokuwa pale ambapo uhusiano wao rasmi na chuo hicho umeisha na pia viongozi wa serikali walioko madarakani hawataruhusiwa kuteuliwa kabisa.

Sambamba na hilo kwa mujibu wa masharti ya mwongozo huo chuo kikuu kitakachotoa shahada ya heshima kinapaswa kuwa kimehitimisha angalau wanafunzi wa awamu nane, kinatoa kozi ya PhD, kinakubalika kwa viwango vya kitaifa na kimataifa na kutokana na masharti haya, vyuo vipya kama vile Selale, Dembi Dolo, Mekdela Amba, Raya, na Debarak havitaruhusiwa kwa sasa kutoa shahada za heshima.

Source Millard Ayo
 
Wizara ya Elimu nchini Ethiopia imetoa Mwongozo mpya unaopiga marufuku Viongozi wa Serikali na viongozi wa Kisiasa nchini humo kutunukiwa Shahada za Heshima (Honorary Doctorate).

Agizo hilo ambalo limetiwa saini na Waziri wa Elimu Nchini Ethiopia Profesa Berhanu Nega kuwasilishwa kwa Vyuo vikuu na taasisi za Elimu nchini humo limezitaka taasisi hizo hususa ni Vyuo ambavyo Wanafunzi wake hawajahitimu angalau awamu nne na havitoi Shahada ya Uzamilivu havitoruhusia kutokoa shahada ya Heshima.

Mwongozo pia unaeleza kuwa Shahada za Heshima zinaweza kutolewa kwa raia wa Ethiopia au Wageni waliotoa mchango wa kipekee katika taaluma au nyanja zao za kazi. Tuzo hiyo inaweza kutolewa kwa mtu mmoja au kikundi kilicho hai au kilichofariki, mradi kimekidhi vigezo vilivyowekwa.

Aidha kuna masharti ya vizuizi Kifungu cha 2 Ibara ya 10 kimeeleza kuwa wafanyakazi wa kudumu wa vyuo vikuu, wajumbe wa Seneti au miundo ya uongozi hawawezi kupokea shahada ya heshima wakati bado wako kazini, isipokuwa pale ambapo uhusiano wao rasmi na chuo hicho umeisha na pia viongozi wa serikali walioko madarakani hawataruhusiwa kuteuliwa kabisa.

Sambamba na hilo kwa mujibu wa masharti ya mwongozo huo chuo kikuu kitakachotoa shahada ya heshima kinapaswa kuwa kimehitimisha angalau wanafunzi wa awamu nane, kinatoa kozi ya PhD, kinakubalika kwa viwango vya kitaifa na kimataifa na kutokana na masharti haya, vyuo vipya kama vile Selale, Dembi Dolo, Mekdela Amba, Raya, na Debarak havitaruhusiwa kwa sasa kutoa shahada za heshima.
images (3).jpeg
 
Aim higher FIRST CLASS HONOURS DEGREE wanaangu. PHD ya heshima kwa truly deserving.
 
Nyerere akitaaa huu ujinga kabisa yeye alipenda kuitwa mwalimu kipindi cha Nyerere mwinyi Mkapa Ualimu ulipoteza ushindi ila viongozi wengi walimu akiwemo kasimu majaliwa lakini huwezi kuskia alisema niiteni kasimu majaliwa
 
Nyerere akitaaa huu ujinga kabisa yeye alipenda kuitwa mwalimu kipindi cha Nyerere mwinyi Mkapa Ualimu ulipoteza ushindi ila viongozi wengi walimu akiwemo kasimu majaliwa lakini huwezi kuskia alisema niiteni kasimu majaliwa
We hupendi kulamba asali
 
Tena Hata Kama Ulifeli Form4.
TCU Ukiwashika Madaraka Makubwa Ndani Ya CCM,
Wana Ku-reward Na Li-phd.
Hata kama ulikosa D ukishakuwa na kile cheo lazima wakupe Udaktari
 
Wenye shahada za heshima (Honorary Doctorate) nchini Ethiopia hawataruhusiwa tena kutumia cheo cha “Daktari” nje ya chuo kilichowatunuku shahada hiyo, kwa mujibu wa mwongozo mpya ulioidhinishwa na Wizara ya Elimu.



Mwongozo huo, uliosainiwa na Waziri wa Elimu Berhanu Nega mnamo Julai 2025, pia unakataza viongozi wa serikali waliopo madarakani pamoja na wagombea wa nafasi za kisiasa kuteuliwa kwa shahada za heshima.

Aidha, vyuo vikuu vipya havitaruhusiwa kutoa shahada hizo mpaka vitakapokuwa vimehitimisha angalau makundi nane ya wahitimu na kutoa digrii za juu zaidi, kama vile PhD. Vyuo ambavyo havijafikia viwango hivyo havitaruhusiwa kabisa kutunuku shahada ya heshima. Pia vinatakiwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa kabla ya kufanya hivyo.

Shahada za heshima zitaruhusiwa kutolewa kwa raia wa Ethiopia au wageni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au sekta zao. Zinaweza kutolewa kwa mtu mmoja au kikundi, waliopo hai au marehemu, iwapo tu wanakidhi vigezo vilivyowekwa.

Kifungu cha Pili, Ibara ya 10 cha mwongozo huo kinakataza wafanyakazi wa muda wote wa vyuo vikuu, wajumbe wa Seneti au viongozi wa kiutawala wa taasisi za elimu ya juu kuteuliwa kwa shahada za heshima, isipokuwa pale ambapo uhusiano wao rasmi na chuo husika umekwisha.

====For English Audience ======
Honorary doctorate holders in Ethiopia will no longer be permitted to use the title “Doctor” outside the awarding institution, under a new directive issued by the Ministry of Education.

Signed by Minister of Education Berhanu Nega in July 2025, the rules also bar serving government officials and political candidates from being nominated for honorary doctorates.

The directive further restricts recently established universities from conferring the distinction. Institutions must have graduated at least eight cohorts of students and offer third degrees, such as PhDs, before awarding honorary doctorates.

Universities, which do not meet these criteria, are prohibited from granting the title. Institutions must also comply with both national and international standards before doing so.

Honorary doctorates may be awarded to Ethiopian or foreign nationals who have made significant contributions to their professional fields. They can be granted to individuals or groups, living or deceased, if they meet the stated criteria.

Under Section Two, Article 10, the directive prohibits nominations for full-time employees, Senate members or administrative staff of higher education institutions, unless their direct relationship with the institution has ended.
 
Wizara ya Elimu nchini Ethiopia imepiga marufuku wapokeaji wa shahada za udaktari wa kutumia cheo cha “Daktari” au “Dr” nje ya taasisi walizopewa heshima hiyo.

Aidha, agizo hilo limeweka wazi kuwa viongozi wa serikali waliopo madarakani pamoja na wagombea wa kisiasa hawataruhusiwa kupokea shahada hizo.
 

Attachments

  • Screenshot_20250820-110016.png
    Screenshot_20250820-110016.png
    538.4 KB · Views: 16
Wizara ya Elimu nchini Ethiopia imepiga marufuku wapokeaji wa shahada za udaktari wa kutumia cheo cha “Daktari” au “Dr” nje ya taasisi walizopewa heshima hiyo.

Aidha, agizo hilo limeweka wazi kuwa viongozi wa serikali waliopo madarakani pamoja na wagombea wa kisiasa hawataruhusiwa kupokea shahada hizo.
 

Attachments

  • Screenshot_20250820-110016.png
    Screenshot_20250820-110016.png
    538.4 KB · Views: 16
Back
Top Bottom