Mkandara, kwa heshma zote ningeshukuru kama ungetoa hii hoja siku na wasaa mwingine. Timing yake is very painful to read. Dr Ulimboka ameng'olewa meno na plaizi, ameng'olewa kucha, amevunjwa mbavu, mikono, taya. Unaweza ukawa na muono tofauti kuhusu huu mgomo wa madaktari, lakini kama nilivyosema nimefadhaishwa sana na comment yako kwenye huu uzi unaongelea hali ya Dr Ulimboka kubadilika ghafla! I almost felt kama mtu kanipiga teke la tumbuno.
Mkuu wangu najua sana kwamba nimeandika mambo mazito sana yanayouma lakini Ndivyo Ilivyo! Na tunatakiwa kujifunza ktk kila jambo linalotupata hapa duniani maana kinachoendelea nchini hakina huruma kwa watu wengineo. Tazma picha utaona Dr. wetu kawekewa vifaa vya kila aina kuhakikisha anapata huduma bora ambayo kuna watu 100 hawaipati tena kwa sababu ya mgomo wa Madaktari.
Binafsi yangu naliona somo hapa na hakuna wakati muafaka zaidi ya huu tunapoziona picha hizi hapa JF wakati watu kama Ulimboka wamejaa Mahospitalini mwetu halafu madaktari wanagoma kwa sababu ya mishahara na kusema wao ni binadamu kama wengine wanahitaji kulipwa vema kwa kazi zao wakitolea mfano Wabunge wanaolala bungeni. Leo tunamwona Daktari wetu akiwa ktk hali sawa na wagonjwa wengine hivyo huruma zote tunazozitoa hapa Janvini ni muhimu tukazielekeza kwa wagonjwa wengine wote pia ambao aidha wamegongwa na gari wameingiliwa na majambazi na kadhalika. Dr.Ulimboka ametufungua macho na tuyatazame haya kama karama za Mwenyezi Mungu kwamba hakuna mbora zaidi yetu inapofikia swala la Ugonjwa.
Nachoweza kuwaomba madaktari warudi kazini kutoa huduma kwa wananchi ambao kwa pamoja sote tushirikiane na vyama vya Upinzani kuelekeza mapambano iwe maandamano, bungeni au mahakama za kimataifa kwa kuzihusisha asasi zote za haki za kibinadamu. Ikiwezekana hata migomo iwe sehemu zote isipokuwa sehemu muhimu kama Hospitali na sokoni..Inatakiwa umoja wetu kupambana na dhulma hii na sii kujiona wabora zaidi ya watu wengine.
Nina hakika kabisa madaktari wanaweza tu kufanikiwa ikiwa swala hili litachukua sura tofauti badala ya kuwa madai ya madaktari lile swala la Kitaifa. Nina hakika Chadema, CUF, TLP, NCCR na asasi nyinginezo wapo upande wa madaktari isipokuwa wamekwazwa na njia zilizotumika kutafuta suluhu. Hili sio swala la JK na madaktari au CCM na madaktari ni swala la kitaifa linatuathiri wote, na linatakiwa vyombo vyote vinavyohusika vishirikishwe ktk mazungumzo na hasa bungeni.
Healthcare inapewa kiasi gani cha bajeti.. sidhani kama inafika asilimia 30 lakini ajabu ni kwamba ktk hizo asilimia yake 80 inatumiwa ktk recurrent expenditures yaani matumizi ya ndani sasa bado wanataka kuongeza matumizi ya ndani kuongeza mishahara yao wakati vita yetu kubwa ni kupunguza matumizi ya serikali ili tuelekeze nguvu zetu ktk maendeleo. Ni majuzi tu wabunge wetu wamepitisha bajeti nyingine mbovu kabisa wakijiongezea mishahara madaktari wakashangilia (wengine wabunge) halafu wamejiunga kutaka madaktari pia waongezewe mishahara!. Hawa watu wanajilipa mishahara mikubwa, wanatembelea magari makubwa ni Miungu watu halafu hawataki kupunguza matumizi yao wenyewe ktk anasa zao lakini wapo radhi kukata fungu la maendeleo ili kuonyesha fedha ndio msingi wa maisha yao wao. Hapana jamani hapana..
Nitarudia kusema Dr.Ulimboka awe sababu ya sisi watanzania kuwa na hasira, chuki na hamaki ya kutokubaliana na mfumo mzima wa AFYA nchini. Pengine sio wakati muafaka wa kuyazungumzia haya lakini nijuavyo Wadanganyika wepesi wa kusahau, ukiwawekea kitu hiki usoni mwao kesho hawataweza kubisha wala kusema ungeyasema haya wakati uleee. Hayakutokea kwa bahati mbaya Mwenyezi Mungu anatuonyesha karama zake!