Dr. Ulimboka: Hali ya afya (Updates)

Dr. Ulimboka: Hali ya afya (Updates)

Kesho anafanyiwa operation na nani?kwani si bado wamegoma?kama wamerudi kazini na mimi mgonjwa wangu niliyemrudisha nyumbani nimpeleke kesho akafanyiwe operation.

Madakatari wamewnunua wenyewe vifaa vinavyohitajika ili kumfanyia operesheni kumbuka katika bajeti hii inayojadiliwa bungeni wizara ya afya iliomba Bilioni 198 kununulia masawa kwa ajili ya hospitali hapa nchini lakin i wkatengewa Bilioni 78 tu pungufu ikiwa ni Bilioni 120; ilihali fedha za posho na safari zimeongezeka kufikia bilioni 500
 
Mkuu tupac umenena yaliyo sahihi.Jina la Ulimboka litabaki kwenye historia ya nchi hii

Akumbukwe kwa kitu gani alichofanya? ndio wananchi waliopoteza ndugu zao watamkumbua kwa kuwa sababu ya wao kuwapotezea maisha ndugu zao kwa kugoma kuwapa huduma za matibabu. Wanajamii fikirini kwa kutumia vinchwa vyenu sio makalio yenu.
 
Kesho anafanyiwa operation na nani?kwani si bado wamegoma?kama wamerudi kazini na mimi mgonjwa wangu niliyemrudisha nyumbani nimpeleke kesho akafanyiwe operation.

Vipi mgonjwa wako nae alipigwa na wale wale wahusika? kichwa kikiwa kama kibuyu maana yake kiko wazi kichwani.
 
Wabongo bana, so ndugu zetu wanaondelea kufa kutokana na mgomo wa akina Ulimboka hawana haki ya kuishi ama, mimi simuonei huruma huyu jamaa honestly, mgomo wao unawaumiza ndugu zetu sana, na simuombei kupona.
Hivi wewe kiumbe... Wa kulaumiwa ni serikali yako dhaifu au Dr. Ulimboka!! Kama huridhiki si uende mahakamani!!??

 
Mimi chicheme kama mambo ni haya ndio maana watu huwa rebels ndio nimeekewa hali halisi kuwbe duniani heri simba kuliko kukutana na binadamu mubaya ukweli swala la ulimboka ni sawa na kusema mtoto kamufyonya halafu we baba unachukua panga unamukata mkono jamani najiuliya je madaktari wakijipanga wakarudi kazini halafu wakaanza kutumia sindano ya kuua mtu kimya kimya jamani tutafika wapi mungu nusuru nchi ya nyerere mi naanza kuogopa kuishi Tanzania
 
Tuko pamoja Dr Steven Ulimboka bwana yuko nawe na atakuponya muda mchache kwani bado ana makusudi na wewe ndio maana walishindwa kukuua.
 
Kesho anafanyiwa operation na nani?kwani si bado wamegoma?kama wamerudi kazini na mimi mgonjwa wangu niliyemrudisha nyumbani nimpeleke kesho akafanyiwe operation.

Mpeleke tu afanyiwe operation ya kichwa na tumbo then awekewe damu yenye ukimwi ndo utajua hawa madr wako serious
 
Duniani sheria itapindishwa lakin mbinguni haki itadhihirika wazi,hao waliompiga na kumtesa dr je mungu watamtoa meno? Watamtoa kucha? Mungu ni mwema ndio maan amezuia roho yake ili awaumbue waliofanya umafia huo
 
KTK MATENDO HAYA YOTE MAOVU ALOTENDEWA DR ULIMBOKA, JK NA CCM HAWAWEZI KUKWEPA NA KWAKWELI WAMEFANIKIWA.

Je, Kuna tofauti gani ya haya yanayotokea Tz na yale ya Kule SYRIA? Hivi bado kuna wendawazimu wataendelea Kudai Tanzania Kuna AMANI?

Damu ya Daktari huyo isiyo na hatia itaendelea kulia na kuitia LAANA nchi hii, believe it or NOT!!
Yanayotendeka Syria ni maswlaa ya kisiasa na hatari ya Udikteta ambao CCM wanautumia. Lakini pia wale wanajeshi wa upande wa pili wanapotumia raia hasa wanawake na watoto kama human shield nao wanawajibika kuelewa makosa yao. Hiki ndicho nachopinga mimi, Madaktari wana kila haki ya kuendeleza madai yao, vyama vya Upinzani na wananchi sote tuna madai yetu makubwa tu..lakini ktk kupambana na hali hiyo hatutakiwi kuwaadhibu wananchi wenyewe ili ujumbe wetu ufike.

I believe in diplomacy, ikishindikana kupitia njia hiyo basi madaktari na wananchi tuungane pamoja na kufanya waloyafanya Tunisia au Egypt sio tuchukue mkondo wa Syria ambao hauna suluhu zaidi ya kufa watu wasikokuwa na hatia zaidi na zaidi. Ombi langu linabakia pale pale ktk maandalizi na decision making. Madaktari na wananchi waungane pamoja kuiadhibu serikali na sii kuondoa nguvu ya uamsho kwa wananchi - It's the method we chose..

Kwa Dr. Ulimboka tunamwomba Mungu amlinde, ampe nguvu na uzima ktk mapambano haya japokuwa nilijua fika haya yangetokea na tulishindwa kumlinda ipaswapo. Bado nasema hivi sisi ni Wanafiki tu maneno mengi JF na magazetini lakini inapofikia kuungana kufanya kweli kila mtu atajikata kivyake na kwa maslahi yake. Bro, asilimia 80 ya watanzania hatuaminiani! hivi tunadanganyana nini hapa JF wakati tunajuana vizuri?. Manyapala na makada wa system wapo ndani ya Union ya Madaktari wanachota Info na kuzipeleka upande wa pili wakikatiwa kitu kidogo tu na kinachodaiwa hapa ni maslahi ya watu fulani tu - Tuna skip the big picture!
- Umaskini jamani kilema!
 
Dr. Ulimboka usijali mwana ww hujamkosea Mungu, kwa kudai haki, utapona tu, siku zote Mungu ni wa wanyonge na waonewa, wafanye wanalotaka utapona tu, aliyekuokoa katika mikono fidhuli atakuokoa tu; waseme wanaleta waganga wasiwalete serikali ni ya raia, na raia daima watashinda tu wataonewa lakini Mungu kamwe hataonewa anasimama na wanyonge, poleni madaktari wetu! hao wanasiasa uchwara wanaofikiri wanaweza kuonea wataona hatima yao ikiishia pabaya.:flypig::flypig::flypig:
 
hi serikali ya nani? Je madaktari hawana haki kusema katika mazingira hayo magumu, je kuwafukuza ni dawa swali kwako je wanasiasa wanalipwa kiasi gani na ukilinganisa wao na madaktari wetu ni nani wana kazi ngumu?:deadhorse:
 
dr%20ulimboka.jpg

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka


Hali ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, aliyelazwa nchini Afrika Kusini, imeendelea kuimarika, ingawa bado yuko chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Edwin Chitage, alisema pamoja na kwamba bado Dk. Ulimboka yuko ICU, lakini hali yake inaendelea kuimarika.

"Tunasubiri ripoti kutoka kwa daktari anayemtibu Dk. Ulimboka ili tufahamu ni kitu gani kinachomsumbua... ingawa daktari wake amesema hajapata ridhaa kutoka kwa mgonjwa wake ya kutoa ripoti hiyo kwa jumuiya yetu," alisema Dk. Chitage.

Mapema wiki iliyopita, baadhi ya vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii, viliripoti kuwa hali yake ni mbaya na kwamba amelazwa ICU.

Kutokana na taarifa hizo kutofautiana, NIPASHE lilikwenda nyumba kwa wazazi wa Dk. Ulimboka eneo la Ubungo Kibangu, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupata taarifa za hali yake.

Hata hivyo, mama mzazi wa Dk. Ulimboka, alipoulizwa kuhusu hali ya mwanaye aliyepelekwa Afrika Kusini, hakuwa tayari kusema chochote kwa kudai kuwa tukio lililompata mwanaye hawezi kulizungumzia.

Mama huyo ambaye alikataa kutaja jina lake, alikuwa na hali ya wasiwasi hasa anapokwenda mtu yeyote ambaye familia haimfahamu.

Usiku wa kuamkia Juni 25, mwaka huu, Dk. Ulimboka alitekwa na watu wasiojulikana wakiwa na silaha za moto, ambao walimjeruhi vibaya ikiwemo kumng’oa meno na kucha.

Kufuatia tukio hilo, madaktari wenzake walichangishana fedha, ambapo Jumamosi ya wiki iliyopita, waliamua kumpeleka nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.






CHANZO: NIPASH

 
Back
Top Bottom