Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 709
Tatizo lako ndugu unajiona una uwezo mkubwa sana kuliko mtu yeyote hapa Tanzania na hata ukitazama post yako inaonyesha kuwa ni mjivuni. Suala la Urais ni jambo la msingi sana,usipotoshe umma,
ndugu yangu,fikiria kwanza,usipende kupelekwa hisia,au kuangalia wengine wanawaza au wanafanya nini,na usiwe bendera fuata upepo.
Uliyoyasema ni mtazamo wako ingawaje yapo tofauti na nilivyo.Sipendi kuendeshwa kwa mkumbo na ninaamini katika kile nikionacho ni sahihi,sina mob psychology hata siku moja.
Ngoja nikuulize,mleta mada/poll malengo yake ya kuanzisha hii poll ni nini?je hao anaosema sijui Maraisi,je wamepitishwa hata na vyama vyao kuwa wagombea?kwanini amewachagua hao wawili tu wakati wapo wengi tu wanaotajwa kuwania urais?je unafikiri sample ya humu JF inatosha kukupa wewe majibu muafaka?mwisho,hii poll inakusaidia nini wewe binafsi na taifa kwa ujumla?
Nakutakia siku njema.ikiwezekana tupange tuonane ili unijue vizuri ili uone kama naendana na hizo sifa ulizoniambia ninazo.