Ndg waungwana huu ni mtazamo wangu binafsi kuhusu Ndodi "Dr"
Kwanza kabisa huyu mtu ni mjasiriamali mzuri sana hapa nchini ambaye ameweza kuteka watu wengi sana kwa maneno yake na tiba zake asilia ambazo kwangu mimi nina imani ni nzuri kuliko za hospitali kwani nyingi hazina kemikali na pia hutoa ushauri wa tiba mbadala kama kula right foods, mazoezi sehemu muafaka na vingine vingi.
Huyu mtu ni mjasiriamali na naweza kusema ni genious kwani ameweza kuangalia tatizo liko wapi na akalitumia kutengeneza hela (creativity phenomena) tena kwa kutumia tiba mbadala ambazo ukisikiliza maelezao yake nyingi ni za kweli
Pia mtu huyu ingawa sina uhakika kuhusu taaluma yake ila inaonyesha anajisomea sana hivyo ana ufahamu wa mambo mengi sana yanayohusu kitu anachofanya
Matatizo ya Ndodi
1. Hayuko organised, kama unafualtilia vipindi vyake utaona anachanganya sana mada na mwisho wa siku anashindwa kutoa kwa ufasaha alichodhamiria kukitoa (poor presentation skill)
2. Ana namba nyingi sana za simu (zaidi ya kumi) kitu ambacho kwa mtu ambaye yuko makini na mwenye kujipanga hawezi kuwa hivyo
3. Yuko kibiashara zaidi kuliko kitabibu kwani kama ukifuatilia vipindi vyake utaona anavutia zaidi kuonana nae kuliko kutoa suluhisho kwa ushauri
4. Kitu kingine kinachonishangaza ni kwamba pamoja na umaarufu alionao anakaa hotelini kama sehemu ya kazi, wakati nadhani ingekuwa vizuri kama angeanzisha kituo cha kueleweka maana pale hotelini kama kikinuka anaweza kukimbia kirahisi, mtu makini na mwenye nia ya kazi yake anatakiwa kuwa na kituo maalum (kwa mtizamo wangu)
5. Katika kuongea kwake ana masikhara mengi sana hivyo kipindi chake kimegeuka kuwa kama komedi hivi, wakati anatakiwa kuwa serious kwani suala la utabibu linagusa maisha ya watu
Kwa hayo matano naona ndio matatizo makuu sijui kuhusu customer care kwenye kituo chake maana sijawahi kufika ila kwa jinsi anavyoongea tu kwenye kipindi naona kama hayuko organised yeye binafsi
Maelezo yako nayaunga mkono 100% binafsi ni mpenzi sana wa vipindi vyake na kila kunapokuwa na vipindi vyake huwa najitahidi kuandika yaliyo ya muhimu na kupitia vipindi vyake nami nimeweza kuwasaidia wengine kukawa na matokeo mazuri.
Kwa upande wa matatizo kama ulivyoeleza ni kweli hayuko organised hasa pale anaporuhusu watu kupiga simu live ndipo muingiliano wa mada unapotokea kwa sababu ni kweli unaweza ukawa unaifuatilia mada aliyoanzisha asiimalize kama alivyotarajia hivyo ukawa umeachwa njiani na kipindi kingine akawa na mada nyingine.
Binafsi namwamini na ukisikiliza maelezo yake ukayafata utajiepusha na magonjwa mengi yanayoweza kuepukika. ila walamikaji wengi niliowaona humu kwa kuwa wamezoea vya rahisi (kama vya wachina) bila kujua hasara zake basi wataendelea kulalamika milele.
Dawa zake zote zinatokana na matunda na matunda mengi inabidi ayaagize nje. kuna matunda yanaitwa kiwi, au hata haya olive au almond ni matunda ambayo hata Tanzania hayapo na kuyapata unakuta kilo moja mengine si chini ya Tshs 50,000 sasa unakuta dawa inahitaji mchanganyiko zaidi ya matunda aina tano kwa mfano. atumie kiasi gani kupata dawa origino isiyo feki kama za mchina za kuongeza makalio? na ya watanzania wangapi wanaohitaji huduma hiyo? bado kuna rasirimali watu na vitendea kazi mbali ya muda anaotumia, hivyo gharama lazima ziwepo ingawa ni kweli kwa mtu maskini kama mimi kuzimudu kamwe sitaweza. ninachojitahidi ni kufuata ushauri ili niepuke kuugua then nikashindwa kujitibu kwa kuwa gharama ni kubwa kwa kweli.
Ushauri kwa walamikaji wengi ambao nimewaona humu pengine kabla ya kulalamika tuwe tunachnguza. maana wengine hata afya bora kuifata shida mfano kunywa maji tu glass nane kwa siku shida ambayo ni kitu cha bure. sasa ukiugua gharama huziwezi unaanza kulalamika ufanyweje. Hatukatai magonjwa yapo ya kila aina duniani mengine hayasemeki ukiyaona mwezio kaugua huwezi kuamini dunia hii na hosipitali zipo maana kuna watu waoaamini hospitali ndio mwisho wa matatizo lakini madawa mengi ndio hujaza sumu mwilini mwisho siku ulikuwa unatibu moyo na figo zinaanza kuleta shida maana zimeshinda kuhimili sumu ya muda mrefu. mtu akikwambia tiba mbadala mansema mjasilia mali basi fata hata ushauri ili uepukane na huo ujasilia mali wake. Kupanga ni kuchagua. siku zote nasema ukiwa mzima shukuru Mungu. Kuna watu wanateseka. Tungekuwa na imani ya kuuchangiana kwa wagonjwa kama tunavyochangia harusi pengine tungepunguza malalamiko. Lakini mtu akiumwa mpaka aje achangiwe ugonjwa umekuwa sugu na kupona ni kudra za Muumba.
Kuna mtu kasema majarida ya tiba mbadala yapo kibao je ni wote wanayasoma? Mimi binafsi nina vitabu kama vitatu aina tofauti hivyo vya tiba mbadala kwa kutumia matunda na vyakula lakini nilichokinunua kwa bei ya chini ni Tshs 50,000 sasa wangapi wana-afford hiyo bei na ikiwa waTZ tuna sifa ya kutopenda kujisomea. Wengi wetu wapendacho ni rahisi, mtelemko, kutafuniwa halafu tumeze ndo maana tunaitwa shamba la bibi kwa ajili ya ufahamu wetu mdogo.
Mifano ni mingi ya ujinga tulio nao kama watu kusubiri usiku wakamwage uchafu barabarani mitaro ikiziba, mafuriko uchafu kila kona mwishoe kipindupindu, kuhara n.k ukienda hospitali dawa kanunue hela huna lawama kibao kwa serikali na yeyote atakekutibu kama Ndodi uwezo bado huna lakini chanzo umesahau kama ni wewe uchafu wako uliomwaga kwenye vyanzo vya maji tena usiku watu wasikuone.
Mimi naona tukielimika na ufahamu wetu wa mambo ukawa mkubwa hata akina Dowan wajao tutawaepuka. bila hivyo tutabaki kulalamika ndani ya blanketi hatuchukui hatua.