Dr. Isaack Ndodi: Hisia mchanganyiko

Dr. Isaack Ndodi: Hisia mchanganyiko

Huyo jamaa hana lolote, kwanza ni vyema angeeleza CV yake na atuambie huo udokta amesomea chuo gani...Ili mtu awe Dr ni lazima awe amesomea udaktari wa Binadamu au wa wanyama kwa miaka isiyopungua mitano, au mtu mwenye degree ya tatu (phD). Je yeye anaingia kwenye kundi lipi?Anachofanya ni kusoma vitabu vya medicine na kuvitafsiri kwa lugha ya 'kisanii' na kuongeza madoido yake. Na huo mdomo wake unamsaidia sana ili watu wamwimi.Biafsi simkubali Kabsaaaaaaaaaa!
 
Isaac Ndodi....Isaac Ndodiii!....same guy kila siku.../whyyyy?
Hakuna ishuzingine?
Akinenepa mnaulizana,...
Akikonda mnamshangaa..
Give him a break...kweeek!

PJ mbona unamtetea sana huyu jamaa? wewe ni mwanasheria waake, au ni shareholder? maana watu wanayoongea yana ukweli ndani yake ingawa aliyepost hii thread ameandika na kupost pumba.
 
Tatizo letu watz ni wavivu wa kutafuta knowledge.kama tungejaribu kujisomea kidogo tungetambua basic things kuhusu afya zetu.
Kwa kuwa ni wavivu basi tunamuachia dr ndodi,mama teri,shehe yahya,mchungaji lwakatare,lusekelo,kakobe na wengineo wa aina hii kutudanganya.
Inashangaza mtu awe na uwezo wa kusubscribe JF halafu ashindwe kugoogle search njia za kupunguza unene.
Wajinga mtaendelea kuliwa.
 
tatizo letu watz ni wavivu wa kutafuta knowledge.kama tungejaribu kujisomea kidogo tungetambua basic things kuhusu afya zetu.
Kwa kuwa ni wavivu basi tunamuachia dr ndodi,mama teri,shehe yahya,mchungaji lwakatare,lusekelo,kakobe na wengineo wa aina hii kutudanganya.
Inashangaza mtu awe na uwezo wa kusubscribe jf halafu ashindwe kugoogle search njia za kupunguza unene.
Wajinga mtaendelea kuliwa.

nakuunga mkono mkuu.
 
Ni kweli aweke cv's zake hadharani na awaeleze wananchi kama yeye ni Dr amespecialize kwenye nini? maana naona hakuna anachoshindwa
 
Huyo jamaa hana lolote, kwanza ni vyema angeeleza CV yake na atuambie huo udokta amesomea chuo gani...Ili mtu awe Dr ni lazima awe amesomea udaktari wa Binadamu au wa wanyama kwa miaka isiyopungua mitano, au mtu mwenye degree ya tatu (phD). Je yeye anaingia kwenye kundi lipi?Anachofanya ni kusoma vitabu vya medicine na kuvitafsiri kwa lugha ya 'kisanii' na kuongeza madoido yake. Na huo mdomo wake unamsaidia sana ili watu wamwimi.Biafsi simkubali Kabsaaaaaaaaaa!

Dk Dk Dk. Kikwete, Dk Manyau nyau, Prof. Maji Marefu, Sir Juma Nature Kiroboto nk. ni baadhi ya wachache wenye title ambazo hawajazisomea au kuzisotea, kawaida kwa tanzania wala usishangae sana. Huwezi jua labda kapew udok wa heshima nje ya nchi.
 
Watanzania bwana, siku moja niliwahi kumsikiliza huyo Dk. Ndondi akizungumzia kuhusu digestive system ya binadamu, nilicho sikia humo sikuamini masikio yangu - nakajiuliza hivi huyu mtu anajuwa anacho zungumza humu lakini! Je anajuwa kwamba kuna watanzania wengi wanao juwa vizuri maswala hayo vizuri tu na siyo kuleta mambo ya "SANGOMA"

Mwishowe nika-conclude kwamba huyu mtu kitu anachofanya ni kusoma vitabu tu kuhusu vyakula na athali zake lakini uelewa wake kuhusu jinsi ya internal organs za binadamu zinavyo fanya kazi ni mdogo sana, sema Mungu amemjalia kuwa a good orator (mzungumzaji/muhigizaji).

Kama wenzangu walivyo zungumza kwenye forum hii tatizo letu watanzania ni wavivu wa kusoma, matatizo yote kuhusu vyakula, magonjwa, madawa na ushauri wa bure wa kisayansi kutoka kwa watu walio elimika kweli kwenye fani hizo vyote hivyo vinapatikana humu kwenye internet huitaji watu wenye questionable qualification kukupa ushauri.

Chunga sana watu wanao sema dawa ya kutibu ubongo tunayo, yakutibu ini tunayo, yakurudisha uterus hata kama hilitolewa na mdaktari tunayo, kongosho tunayo, enzymes zote tunazo, red/white cells tunayo, serum tunayo; in short take heed of master of all trade it may cost you an arm and leg at the end of the DAY.

Sikatai wasifanye kazi zao lakini wa ache ku-exaggerate huwezo wao wakumbuke watanzania wa sasa hivi siyo wa miaka ya arobaini na SABA, alafu anapo zungumza kwenye radio au television anapashwa kuwa mwangalifu anayo yaongea, nampa ushari huo wa bure, kama yeye ni Mtu wa Mungu anapashwa kuwa mkweli anayo yajuawa/yaweza aseme anayajuwa hasiyo yajuwa vizuri hakili kwamba kusema kweli hayajuhi kiundani, hakuna atakaye mcheka.
 
Jamani huyu dr Ndodi , jana nilimsikia . Anasoma vitabu vya turejee edeni . Tupate CV yake kama ni nutritionist, dietician au....
 
Isaac Ndodi....Isaac Ndodiii!....same guy kila siku.../whyyyy?
Hakuna ishuzingine?
Akinenepa mnaulizana,...
Akikonda mnamshangaa..
Give him a break...kweeek!
Mkuu una interest binafsi nn? nakuona uko vere defensive ikitolewa issue ya huyu bwana.....especially kwenye mambo yake ya tiba.
 
Mie nadhani sio interest binafsi za PJ, ila ni kutofautiana mawazo na misimamo tu na hili ndio msingi muhimu katika kupanua wigo wa mawazo na michango yetu.
 
why listening/watch him, if at all you are not interested? tuachieni siye watz wavivu wa kusoma tumsikilize
 
Tafuta oppurtunity yako, acha kuongelea mwenzako. Tujaribu kuwaheshimu wenzetu wanaojaribu. Siyo rahisi kama unavyofikiria eti kuwadanganya watu na kukulipa pesa, hebu jaribu na wewe. Tujenge utamaduni wa kuwaheshimu WATANZANIA wenzetu wanaojaribu, yule anatoa elimu yake public na watu wanafanya maamuzi wenyewe; kuliko mafisadi wanaotuibia kwa mlango wa DOWANS na kadhalika.
 
Ni kweli aweke cv's zake hadharani na awaeleze wananchi kama yeye ni Dr amespecialize kwenye nini? maana naona hakuna anachoshindwa

Hakuna kitu kibaya sana kama ukosefu wa ufahamu na kunyimwa fikira japo kiduchu, ukazungumza la maana.

Nikuulize ukishawekewa CV yake itakuwa imekusaidia nini?

Hospitalini kote unakoenda kutibiwa unawekewa CV za hao wanaokutibu au ukikuta tu mtu kavaa overcoat jeupe basi ushaamini huyu ndo daktari ili mraidi anafanya kazi muhimbili, au kwingineko. Nafikiri ungeacha ukiritimba wa mawazo.

Pamoja na hayo hulazimwishwi kumwangalia Dk. Ndodi kama anayoongea ni ya uongo na hayana hata faida kwako. Mbona channel ni nyingi tu tena zenye vipindi vya kukuburudisha bila kujifunza la maana ni wewe tu na muda wako. angalia futuhi, super sport, original comed, la maana labda taarifa ya habari kisha kula ugali wako fanya mambo yako mengine.

Tuache siye tunaopenda tusivikose vipindi vyake hata kama anaosoma vitabu vya turejee eden kama mdau hapo juu alivyosema. maanda hata Dk bingwa wa muhimbili ukiingia ofisini kwake hukosi vitabu juu ya meza kukujulisha kuwa soma vitabu upate maarifa. Hoja zingine huwa za kipuuzi.

Weka CV yako tuone kuwa angalau kwa kupitia CV yako watanzania wanaweza wakapata ufahamu na kuacha kuwa wajinga ndo waliwao au shamba la bibi. na pia kwa kupitia CV yako watajitahidi kuepukana na magonjwa ya milipuko kama kipindupindu, kupunguza magonjwa ya moyo au kwa kupitia CV yako angalau namba ya wanaofeli kidato cha nne itapungua na uchumi wa nchi utaimarika aha au pengine dowan hawatalipwa **********n.k. CV, CV, CV, lol!

Jali yako unayoona yanakufaa maana siye wengine tulikuwa hatujui kuwa mkaa wa vifuu vya nazi unaondoa gesi na sumu mwilini mpaka niliposikia kwa dk ndodi. nikajaribu siku moja kutumia nilipokuwa na shida ya gesi nikapata ahueni baada ya muda mfupi, pia sikuwa najua dawa ya meno mpaka siku niliposikia ndulele na jinsi ya kutengeneza nikatengeneza mwenyewe na kutumia mpaka leo meno yangu yako vizuri maana nilikuwa nimeshaamua kwenda kung'oa. So sisi wajinga anatufaa kwa upande mwingine ndo maana tunapenda kumsikiliza maana tunaweza pata tusiyojua tukaepuka kwenda kulipia hizo M3 pale tutakapokuwa wagonjwa. wewe baki na kutaka CV yake hatahivyo nafikiri unawajua wenye CV wafate ukiwa na shida. mwacheni baba wa watu. hamwibii mtu watu wanakwenda wenyewe kwake kwa kuwa wana shida. Sidhani kama mtu hana shida atamfuata ndodi kwanza ukafanye nini. Nafikiri tungeilalamikia serikali yetu ijitahidi kupunguza mlipuko wa bei unaofanya gharama za maisha kuwa juu kila uchao.
 
umelonga mtu wangu, kibaya zaidi anajiita mtumishi wa Mungu lakini bei ya dawa zake ni juu mno.
 
PJ mbona unamtetea sana huyu jamaa? wewe ni mwanasheria waake, au ni shareholder? maana watu wanayoongea yana ukweli ndani yake ingawa aliyepost hii thread ameandika na kupost pumba.

Jambo mkuu me nakuogopa sana hayo majicho.
 
Unajua,kama unaona anachosema ni urongo,acha kufanya!kuna madaktari wengi ambao wanakufa na tb but wanatibu wenye tb so mtu anavyosema yeye ni mnene etc,sio good..fuata moyo wako,ukiona sawa,fanya..its a free world!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom