Dr. Isaack Ndodi: Hisia mchanganyiko

Huyo dk muongo diabetes haiponywi nmna hiyo. Kisukari ni za aina tofauti no.1 na no 2. Sasa kiufupi ni matibabu ya muda mrefu ambayo ni pamoja na kubadilisha tabia ya maisha ikiwa nipamoja na chakula kikichukua nafasi kubwa na dawa kila siku ikizidi sana ni elfu ishirini kwa mwezi. Kipimo cha kisukari kama mgonjwa akinunua cha kwake binafsi ni chini ya laki mbili. hurumia walalahoi, Sasa huu dk ni mwizi hajali maslahi ya umma Tsh. 3m?!/!? Dk fuata maadili ya kazi ufisadi kila kona!!!!
 
kama vipi tumia product za green world unapona mm shosti wangu walienda kwake akiwa na tatizo la sumu nyingi mwilini akamwambia tiba 3 m tukapata ushauri akatumia product za green world imemcost laki 6 amepona haumwi kabisa
 
NILIWAI KUMPELEKA DADA YANGU KWA DR.Ndondi ikiwa mwanza.alikuwa na matatizo ya kivimba miguu,na presha ya kushuka
ALITUAMBIA Ugonjwa huu unaweza kupona kwa wiki 4 kila wiki natakiwa nilipe laki 3.Tulitoa laki 3 za wiki ya kwanza tukapewa dawa.
HATUKURUDI TENA.LAKI 3 ZIMEKWENDA ,DAWA DOZI YAKE HATUKUMALIZA KWA KWA SABABU YA UKATA.

KUNA HAJA YA SELIKARI KUWAMURIKA WATU KAMA HAWA AMBAO WANAIBIA WATU LIVE.
 
Anafidia hizo gharama za dawa ama ?
3m alipie....asipopona zinarejeshwa?

ndodi ana vipindi vingi sana kwenyetv stations...star tv na eatv...unadhani asipochaji hizo 3m atapata wapi hela ya kuendelea kuuza sura pale kwenye tv? huo sio uungwana kabisa kwa watz ambao wengi tuko masikini.
 
Ndg waungwana huu ni mtazamo wangu binafsi kuhusu Ndodi "Dr"

Kwanza kabisa huyu mtu ni mjasiriamali mzuri sana hapa nchini ambaye ameweza kuteka watu wengi sana kwa maneno yake na tiba zake asilia ambazo kwangu mimi nina imani ni nzuri kuliko za hospitali kwani nyingi hazina kemikali na pia hutoa ushauri wa tiba mbadala kama kula right foods, mazoezi sehemu muafaka na vingine vingi.

Huyu mtu ni mjasiriamali na naweza kusema ni genious kwani ameweza kuangalia tatizo liko wapi na akalitumia kutengeneza hela (creativity phenomena) tena kwa kutumia tiba mbadala ambazo ukisikiliza maelezao yake nyingi ni za kweli

Pia mtu huyu ingawa sina uhakika kuhusu taaluma yake ila inaonyesha anajisomea sana hivyo ana ufahamu wa mambo mengi sana yanayohusu kitu anachofanya

Matatizo ya Ndodi

1. Hayuko organised, kama unafualtilia vipindi vyake utaona anachanganya sana mada na mwisho wa siku anashindwa kutoa kwa ufasaha alichodhamiria kukitoa (poor presentation skill)

2. Ana namba nyingi sana za simu (zaidi ya kumi) kitu ambacho kwa mtu ambaye yuko makini na mwenye kujipanga hawezi kuwa hivyo

3. Yuko kibiashara zaidi kuliko kitabibu kwani kama ukifuatilia vipindi vyake utaona anavutia zaidi kuonana nae kuliko kutoa suluhisho kwa ushauri

4. Kitu kingine kinachonishangaza ni kwamba pamoja na umaarufu alionao anakaa hotelini kama sehemu ya kazi, wakati nadhani ingekuwa vizuri kama angeanzisha kituo cha kueleweka maana pale hotelini kama kikinuka anaweza kukimbia kirahisi, mtu makini na mwenye nia ya kazi yake anatakiwa kuwa na kituo maalum (kwa mtizamo wangu)

5. Katika kuongea kwake ana masikhara mengi sana hivyo kipindi chake kimegeuka kuwa kama komedi hivi, wakati anatakiwa kuwa serious kwani suala la utabibu linagusa maisha ya watu

Kwa hayo matano naona ndio matatizo makuu sijui kuhusu customer care kwenye kituo chake maana sijawahi kufika ila kwa jinsi anavyoongea tu kwenye kipindi naona kama hayuko organised yeye binafsi
 
Huyo dk muongo diabetes haiponywi nmna hiyo. Kisukari ni za aina tofauti no.1 na no 2. Sasa kiufupi ni matibabu ya muda mrefu ambayo ni pamoja na kubadilisha tabia ya maisha ikiwa nipamoja na chakula kikichukua nafasi kubwa na dawa kila siku ikizidi sana ni elfu ishirini kwa mwezi. Kipimo cha kisukari kama mgonjwa akinunua cha kwake binafsi ni chini ya laki mbili. hurumia walalahoi, Sasa huu dk ni mwizi hajali maslahi ya umma Tsh. 3m?!/!? Dk fuata maadili ya kazi ufisadi kila kona!!!!
Mhhhhhh! Ninae ndugu yangu mza anajiweza kwa vijisenti alienda wakati ameanza vipindi vyake. Alikua anasumbuliwa Gout akalipia malipo ya awali...hakuenda tena maana hakupona wala hakupata nafuu kabisa. Hadi leo hii hahitaji ahata kumsikia.
Kwani ni mchungaji au dr(profesa) kama profesa Mh:maji marefu?
Maana haeleweki kabisa!
Kweli hii kali.
Walaumiwe Startv kukubali matangazo?
Mbona CDM wakilipia airtime hawakubaliwi?
Vigezo gani wanatumia hawa watu wa marketing?
 
ndodi ana vipindi vingi sana kwenyetv stations...star tv na eatv...unadhani asipochaji hizo 3m atapata wapi hela ya kuendelea kuuza sura pale kwenye tv? huo sio uungwana kabisa kwa watz ambao wengi tuko masikini.

Wanaibiwa ni wengi. Dr gani unahitaji 3m kabla ya huduma? Mbaya zaidi siamini kama anatoa receipt?
Tz kila mtu anakula atakavyo...ukiona anchukuliwa hatua na serikali yetu...itakya alikua hatoi chochote kwa wahusika.
Million tatu????? Kumtibia kisukari mtanzania?
Hivi ni ukweli au mnatupa upupu humu JF?
Imeniuma we acha tu!
 
Sasa huyo ndugu yako anataka kupona au abaki na 3M?
NINACHOJUA NI KWAMBA AKITOA HIYOFEDHA atapona BILA YA SHAKA...
Labda alijisikia duni kwa vile hana hiyo hela...
Mara ingine hata umasikini unasababisha ulalamiishi usiokuwa na sababu!

Paka Jimmy Vp mkuu, mbona unanitisha: au wewe ndy Dr. Ndodi? Kama ndy basi nakuambia wazi kuwa wewe ni MWIZI! na uache kabisa tabia ya kutumia Dr. Nyuma ya jina lako: ni Utapeli. Umeambiwa dr anahesabu dk za kuongea na mgonja: muda ukiisha anagonga kengele mgonjwa aondoke au mpaka aongeze pesa!!!!!!! shame on you

NINACHOJUA NI KWAMBA AKITOA HIYOFEDHA atapona BILA YA SHAKA...You are a great thinker PAKA JIMMY, Usiongee kama layman! Sorry
 
Huyo dk muongo diabetes haiponywi nmna hiyo. Kisukari ni za aina tofauti no.1 na no 2. Sasa kiufupi ni matibabu ya muda mrefu ambayo ni pamoja na kubadilisha tabia ya maisha ikiwa nipamoja na chakula kikichukua nafasi kubwa na dawa kila siku ikizidi sana ni elfu ishirini kwa mwezi. Kipimo cha kisukari kama mgonjwa akinunua cha kwake binafsi ni chini ya laki mbili. hurumia walalahoi, Sasa huu dk ni mwizi hajali maslahi ya umma Tsh. 3m?!/!? Dk fuata maadili ya kazi ufisadi kila kona!!!!
Siyo DR. Bana, acha kudhalilisha fani! lolz
 
Mwalimu , dokta ( mshauri) pia ni mtangazaji.

Ok kwa hiyo hizo zote ni title zake,kazi ipo,wala huwa sipotezi muda wangu kuangalia hicho kipindi chake,
ndugu yangu aliwahi kwenda kumwona alitoka huko amekata tamaa, na hakurudi tena.
 
Ok kwa hiyo hizo zote ni title zake,kazi ipo,wala huwa sipotezi muda wangu kuangalia hicho kipindi chake,
ndugu yangu aliwahi kwenda kumwona alitoka huko amekata tamaa, na hakurudi tena.

Maadili ya udaktari hata kiapo cha udaktari haviruhusu mtu kujitangaza kama anavyofanya huyu bwana, kwanza sio Dr by professional ndo maana ukiomba CV yake anakuwa mkali mithili ya mbogo. Mi naomba medical council of Tanganyika, Medical association of Tanzania na wizara ya Afya viingilie kati na kuweza kuweka utaratibu mzuri kwa watu wanaofanya alternative medicine, otherwise italeta mkanganyiko kwenye jamii.
 
PDIDY...UMETUMIA BUSARA NA HEKIMA KUWAKILISHA UJUMBE WAKO WENYE UCHINGU MWINGI NA MAUMIVU YA NDANI......nakutume kawafundishe vyama fulani kuwakilisha ujumbe bila kuleta madhara


Ukisikia mtu anaitwa mwehu usidhani ni yule anaeokota makopo jalalani au anaetembea uchi tu la hasha, watu kama wewe automaticaly tayari una sifa hiyo.
Wewe mtu anaongelea taarifa za kuuguza ndugu yake wewe unaleta ulevi wako wa ccm! shame on you mentallic slave, to be used like a condoms after use to be dumpped. Rubbish.
 
mhhhhhh! Ninae ndugu yangu mza anajiweza kwa vijisenti alienda wakati ameanza vipindi vyake. Alikua anasumbuliwa gout akalipia malipo ya awali...hakuenda tena maana hakupona wala hakupata nafuu kabisa. Hadi leo hii hahitaji ahata kumsikia.
Kwani ni mchungaji au dr(profesa) kama profesa mh:maji marefu?
Maana haeleweki kabisa!
Kweli hii kali.
Walaumiwe startv kukubali matangazo?
Mbona cdm wakilipia airtime hawakubaliwi?
Vigezo gani wanatumia hawa watu wa marketing?

hawa mwisho wao unasikia wanagombea ubunge mwanza ama dar kwa umaarufu kama majimarefu na wapuuzi watanzania wanampeeleka bungen dem'n
m sisemi
 
Ndg waungwana huu ni mtazamo wangu binafsi kuhusu Ndodi "Dr"

............
Matatizo ya Ndodi

1. Hayuko organised, kama unafualtilia vipindi vyake utaona anachanganya sana mada na mwisho wa siku anashindwa kutoa kwa ufasaha alichodhamiria kukitoa (poor presentation skill).........
.......
wakati anatakiwa kuwa serious kwani suala la utabibu linagusa maisha ya watu
Kwa hayo matano naona ndio matatizo makuu sijui kuhusu customer care kwenye kituo chake maana sijawahi kufika ila kwa jinsi anavyoongea tu kwenye kipindi naona kama hayuko organised yeye binafsi


6. Huwa anakandia wanawake wanene na wenye vitambi, wakati nyumba ndogo yake iko pale Mwanza imejaziana kila sehemu ya mwili including kitambi.
 
Pamoja na yote mazuri na mabaya yanayosemwa na watu kumhusu huyu Dr. Ndodi, mimi nina angalizo;

1. Je nani anyeweza kutujulisha kilichotokea hadi akamwambia huo mgonjwa wa pdiddy alete mil.3? hapo lazima tukubali kwamba kulikuwa na mazungumzo, katika hali ya kawaida kama mgonjwa hakuridhika lazima atafute namna ya kumsema vibaya dk wake na hawezi kusema ya upande wake, kwahiyo sidhani kama ni jambo la busara kuanza kumshambulia mtu wa watu kwa maelezo ya upande mmoja. kama kungekuwa na maelezo ya upande wa pili hapo tungeweza kuwa fair katika mashambulizi tunayoelekeza kwa dr. ndodi.

2.Suala la uhai wa mtu ama kifo chake linabaki kwenye mamlaka ya MUNGU mwenyezi, tusijaribu kumrundikia ndodi tuhuma ambazo hastahili. Hata rais wa zamani wa Yugoslavia,bw.Tito alifariki dunia akiwa amezungukwa na madaktari bingwa wa kila aina lakini kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kutoa na kuchukua uhai alikuwa ameamua tito alifariki dunia akiwa amezungukwa na madaktari bingwa.
Kama kuna mtu katibiwa kwa ndodi na hakupona hilo sio jambo la ajabu kwakuwa yeye ni mwanadamu tu, siye MUNGU, hata huko mahospitalini watu wanakufa tena wakiwa wametumia gharama kubwa. Mwl. Nyerere alipelekwa uingereza kutibiwa lakini alifariki ni sawa na wengine waliokwenda sehemu mbalimbali kutibiwa na hawakupona. Na kuna wengine wengi wanatibiwa kwenye hospitali kubwa hapa nchini ama nje ya nchi, kwa waganga wa kienyeji na kwingineko na hupona ama vinginevyo, jamani tusimnyoshee kidole huyu muungwana kwa suala la kifo, maana tunasahau msururu wa watu waliopona kwa tiba yake na walikuwa wamekata tamaa huko mahospitalini.

3. Kwakuwa anakuwa na vipindi vya television na anatoa namba zake watu wanatuma sms na hata kupiga simu, mbona sijawahi kusikia mtu akituma sms ama kupiga simu kulalamika zaidi ya kusikia watu wakiulizia matatizo yao mbalimbali ili wasaidiwe? Mi nadhani kama kuna tatizo kwenye huduma zake watu wasingekuwa wanamiminika kila siku kwenda kwake, au kama ana customer care mbovu na bado watu wanamiminika kwenda kwake basi tatizo haliko kwake pekee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom