Dkt. Leonard Akwilipo: Wanafunzi waliopata mimba Tanzania kurejea masomoni kupitia vyuo vya maendeleo ya wananchi

ni sahihi kabisa maana ukiangalia nchi jirani kenya.. wao haijalishi mtoto wa shule ya msingi au sekondari.. haijalishi amepata mimba ndani au nje ya shule.. wanaendelea na masomo yao kama kawaida na ndoto zao zinatimika na bado wanatuzidi kimaendeleo.. ko haina haja wanafunzi waliopata mimba kusimamishwa masomo.

tuamkeni..
yawezekan one among the reasons that forces these female creatures to engage in love relationship and become pregnant may be their weak background economic status... and they engage in.. and later on accidentally they perceive..

kwahiyo kupata mimba kwa mwanafunzi ni ajali tu kama ajali nyingine.. na hakuna binadamu yeyote ambaye yupo tayari kuharibu maisha yake even if he/she ignorant to what extent. tuamkeni mama aangalie swala hili..
 
Sote tumetokana na mimba!

Sielewi kwa nini iwe stigmatized kiasi hicho!
Well, mimba kwa jamii za kiafrika ni kukosa maadili maana umeanza mambo kabla ya ndoa as you know huku kwetu jamii bado zinaamini mtoto akiwa mkubwa basi aolewe ndio azae kwenye mji wake sio anazalia nyumbani kwa babake.

There is a lot behind this, mtoto wa kike anaheshimika, kama anaheshimika basi asianze kutembea na wanaume wakati anaishi kwao maana inakuwa anadhalilisha ukoo, wanaume wanaomdharau babako ndio maana wanakubeba na wanakurudisha uzalie kwenu.

Story ni nyingi, lakini stigma inatokana na jamii zenyewe zinavyochukulia mtoto au binti kuanza mapenzi mpaka kuzaa ingali yupo kwao.

Stigma pia ni kama detterance kwa wengine wasifanye hayo lakini sasa bahati mbaya ndio inakuwa inamuaffect aliyepata mimba na mtoto anayezaliwa ambaye ni innocent.

Ila wakati mwingine mabinti bila kuwaweka sawa utapata shida watakuzalia hapo nyumbani utalea kila mtoto wa mtu na itamuathiri zaidi mwanao.

So better the lesser harm than the bigger one although zote ni athari.
 
Bado haijakaa poa. Wanatakiwa warudi shule na kuendelea masomo yao. Hao wa ufundi labda watake wao.
 
Well, mimba kwa jamii za kiafrika ni kukosa maadili maana umeanza mambo kabla ya ndoa as you know huku kwetu jamii bado zinaamini mtoto akiwa mkubwa basi aolewe ndio azae kwenye mji wake sio anazalia nyumbani kwa babake.

There is a lot behind this, mtoto wa kike anaheshimika, kama anaheshimika basi asianze kutembea na wanaume wakati anaishi kwao maana inakuwa anadhalilisha ukoo, wanaume wanaomdharau babako ndio maana wanakubeba na wanakurudisha uzalie kwenu.

Story ni nyingi, lakini stigma inatokana na jamii zenyewe zinavyochukulia mtoto au binti kuanza mapenzi mpaka kuzaa ingali yupo kwao.

Stigma pia ni kama detterance kwa wengine wasifanye hayo lakini sasa bahati mbaya ndio inakuwa inamuaffect aliyepata mimba na mtoto anayezaliwa ambaye ni innocent.

Ila wakati mwingine mabinti bila kuwaweka sawa utapata shida watakuzalia hapo nyumbani utalea kila mtoto wa mtu na itamuathiri zaidi mwanao.

So better the lesser harm than the bigger one although zote ni athari.
Kwa nini umtwike mzigo wote binti ambae tumemfundisha kuwaheshimu na kuwapigia magoti wanaume badala ya hao wanaume watu wazima ambao kusudi lao kubwa ni kuwalaghai kwa kutumia nafasi walizokuwa nazo katika jamii? Hatutaki kuwapa elimu kuhusu mambo yao kwa kusema kuwa tutawafundisha umalaya halafu tunashangaa anapopata mimba? Hawa watoto kosa lao ni kuzaliwa kwenye jinsia hiyo na si lingine. Ni unafik mkubwa kuwaweka watoto wetu kwenye pedestal wakati tunafanya kila jitihada kuharibu watoto ambao sio wetu. Na, ndio, hata mabinti wanaofanya kazi kwenye mabaa wanastahili heshima kama ile tunayotaka wake na mabinti zetu wapewe. Ovyo kabisa.

Amandla...
 
Kunyanyapaa aliyepata mimba ni jambo la ajabu sana. Kinachofanya mtihani ni kichwa na mikono sio viungo vya uzazi!
 
Kwa nini umtwike mzigo wote binti ambae tumemfundisha kuwaheshimu na kuwapigia magoti wanaume badala ya hao wanaume watu wazima ambao kusudi lao kubwa ni kuwalaghai kwa kutumia nafasi walizokuwa nazo katika jamii? Hatutaki kuwapa elimu kuhusu mambo yao kwa kusema kuwa tutawafundisha umalaya halafu tunashangaa anapopata mimba? Hawa watoto kosa lao ni kuzaliwa kwenye jinsia hiyo na si lingine. Ni unafik mkubwa kuwaweka watoto wetu kwenye pedestal wakati tunafanya kila jitihada kuharibu watoto ambao sio wetu. Na, ndio, hata mabinti wanaofanya kazi kwenye mabaa wanastahili heshima kama ile tunayotaka wake na mabinti zetu wapewe. Ovyo kabisa.

Amandla...
Wote waadhibiwe lakini tuwakanye nao sio kuwaambia jibebishe lipanue tu. NO, turudishe kampeni zile za FATAKI na SAY NO.
 
Wote waadhibiwe lakini tuwakanye nao sio kuwaambia jibebishe lipanue tu. NO, turudishe kampeni zile za FATAKI na SAY NO.
Hazijawahi kusaidia. Unadhani mabinti wameanza kupata mimba hivi karibuni tu? Wazee wetu walijua yote hayo ndio maana kulikuwa na vyuo vinavyoitwa jando na unyago. Watoto walipewa elimu tosha kuhusu mabadiliko katika miili yao. Na sio tamaduni yetu kuwanyanyapaa watoto waliopata mimba maana katika jamii zetu watoto walienziwa.

Kwa nini hatujiulizi inakuwaje huko ambako tunasema wanawapa mno uhuru binti zao hawana tatizo kubwa la mimba za utotoni wakati sisi ambao tunajifanya wakali kila siku watoto wanazaa watoto. Inabidi tuache unafik.

Amandla...
 
Hazijawahi kusaidia. Unadhani mabinti wameanza kupata mimba hivi karibuni tu? Wazee wetu walijua yote hayo ndio maana kulikuwa na vyuo vinavyoitwa jando na unyago. Watoto walipewa elimu tosha kuhusu mabadiliko katika miili yao. Na sio tamaduni yetu kuwanyanyapaa watoto waliopata mimba maana katika jamii zetu watoto walienziwa.

Kwa nini hatujiulizi inakuwaje huko ambako tunasema wanawapa mno uhuru binti zao hawana tatizo kubwa la mimba za utotoni wakati sisi ambao tunajifanya wakali kila siku watoto wanazaa watoto. Inabidi tuache unafik.

Amandla...
Hii kitu ya unyanyaoaa wa mabinti waliopata mimba inaweza kufaa kuwa thesis aisee kama haijafanyiwa bado although unaweza kuitwist namna nyingine tu .
 
Hii kitu ya unyanyaoaa wa mabinti waliopata mimba inaweza kufaa kuwa thesis aisee kama haijafanyiwa bado although unaweza kuitwist namna nyingine tu .
Kweli kabisa Mkuu. Mara nyingi tunahusisha mimba na promiscuity, kwamba wanaopata mimba ni wale wanaotembea na wanaume wengi. Tunajisahaulisha kuwa mtu anaweza kushika mimba hata kama ametenda kitendo hicho mara moja tu. Unaweza kukuta wale ambao ni promiscuous hawapati mimba bali wale ambao ni naive au ambao walishikwa kwa nguvu ndio wanapata mimba. Hili zoezi ni la uonevu uliopitiliza, Mkuu. Hatupaswi kutumia kitu arbitrary kama miamba kumuharibia maisha mama na mtoto wake.

Amandla...
 
Hii ni kumnyima mtoto wa kike elimu tu. Na jamii inayotoa adhabu ya namna hiyo Kwa yoyote kwenye Karne ya 21, achilia mbali mtoto, ni jamii backward.
 
Mbna unadharau kaz yangu????
Si vyuo kitu. Na hii ina maana msichana yeyote atakaesoma kwenye "vyuo" hivyo siku zote atatambulika kama ni mmoja wa wale waliopata mimba wakiwa wanafunzi. Hii ni fig leaf tu. Binti aliyekuwa akiongoza darasani na ambae kweli ni potential ataishia kujifunza ufundi cherehani! Na frustration hizo ndio zitawapelekea kuongeza watoto maana wanajua jamii haiwataki!

Amandla...
 
Serikali ya Tanzania imetangaza kuwaruhusu wanafunzi waliokatiza masomo yao kwa kwasababu ya kupata mimba kurejea masomoni kupitia vyuo vya maendeleo ya wananchi
Akizungumza na wakuu wa vyuo vya maendeleo ya wananchi nchini humo, Katibu mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , Dk Leonard Akwilapo amewataka wakuu hao wa vyuo kuhakikisha kuwa wanafunzi wa kike walioshindwa kuendelea na masomo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo mimba wanarudi na kuendelea na masomo.

Amewataka wakuu hao wa vyuo kutekeleza agizo hilo la kudahili wanafunzi hao kupitia mpango wa elimu haina mwisho ifikapo mwaka 2022.
Pamoja na kutaka vyuo vyote vya maendeo ya wananachi viwe vimesajiliwa kama vituo vya kufanyia mitihani ya kidato cha pili na kidato cha nne, amesema hatua hiyo ya kurejesha wanafunzi wa kike waliokatiza masomo yao yanatokana na majadiliano ya muda mrefu ya wizara hiyo na benki ya dunia.
Elimu

Katibu mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , Dk Leonard Akwilapo

'Tulikuwa na mabishano mazungumzo marefu kwenye mpango wa kuimarisha na kuboresha elimu ya sekondari hapa nchini, moja ya makubaliano , ilikuwa ni kutoa fursa kwa wasichana ambao wamekatiza masomo kwa njia yoyote ile, wapate fursa ya kurudi na kuendelea na masomo, na tukasema tutatumia vyuo vya maendeleo ya wananchi, lazima tuanze hatuna uwanja, sio suala la kujadiliana, mambo mengine ya walimu mtatuachia sisi', alisema Dk. Akwilapo.
Kwa mujibu wa maelezo hayo, wanafunzi hao watarejea darasani katika vyuo 54 kuanzia mwakani, ikiwa ni utekelezaji wa makubaliano ya kuboresha elimu ya sekondari pamoja na kuwapa fursa wasichana waliokatiza masomo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo mimba kupata haki ya elimu.


Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli alipiga marufuku wanafunzi wanaopata mimba mashuleni kuendelea na masomo ya shule ya msingi na sekondari hali iliyozua mijadala na makelele kutoka kwa wanaharakati wa haki za binadamu nchini na nje ya nchi hiyo.
Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania Zitto Kabwe aliwahi kuiandikia Benki ya Dunia kusitisha kuikopesha Tanzania dola milioni 500 za elimu kabla ya mabadiliko ya kisera kufanyika.
Vyama vya upinzani nchini Tanzania na wanaharakati wa haki za binadamu nchini humo na wa kimataifa wamekuwa wakitishia shinikizo la kutotolewa kwa mkopo huo mpaka pale Tanzania itakaporuhusu wanafunzi wanaopata ujauzito waruhusiwe kuendelea na mfumo rasmi wa elimu.
Masikini MAGUFULI MAMBO YAKO YANAFUTIKA
 
Serikali ya Tanzania imetangaza kuwaruhusu wanafunzi waliokatiza masomo yao kwa kwasababu ya kupata mimba kurejea masomoni kupitia vyuo vya maendeleo ya wananchi.

Akizungumza na wakuu wa vyuo vya maendeleo ya wananchi nchini humo, Katibu mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , Dk Leonard Akwilapo amewataka wakuu hao wa vyuo kuhakikisha kuwa wanafunzi wa kike walioshindwa kuendelea na masomo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo mimba wanarudi na kuendelea na masomo. Amewataka wakuu hao wa vyuo kutekeleza agizo hilo la kudahili wanafunzi hao kupitia mpango wa elimu haina mwisho ifikapo mwaka 2022.

Pamoja na kutaka vyuo vyote vya maendeo ya wananachi viwe vimesajiliwa kama vituo vya kufanyia mitihani ya kidato cha pili na kidato cha nne, amesema hatua hiyo ya kurejesha wanafunzi wa kike waliokatiza masomo yao yanatokana na majadiliano ya muda mrefu ya wizara hiyo na benki ya dunia.

Elimu

Katibu mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , Dk Leonard Akwilapo

'Tulikuwa na mabishano mazungumzo marefu kwenye mpango wa kuimarisha na kuboresha elimu ya sekondari hapa nchini, moja ya makubaliano , ilikuwa ni kutoa fursa kwa wasichana ambao wamekatiza masomo kwa njia yoyote ile, wapate fursa ya kurudi na kuendelea na masomo, na tukasema tutatumia vyuo vya maendeleo ya wananchi, lazima tuanze hatuna uwanja, sio suala la kujadiliana, mambo mengine ya walimu mtatuachia sisi', alisema Dk. Akwilapo.

Kwa mujibu wa maelezo hayo, wanafunzi hao watarejea darasani katika vyuo 54 kuanzia mwakani, ikiwa ni utekelezaji wa makubaliano ya kuboresha elimu ya sekondari pamoja na kuwapa fursa wasichana waliokatiza masomo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo mimba kupata haki ya elimu.

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli alipiga marufuku wanafunzi wanaopata mimba mashuleni kuendelea na masomo ya shule ya msingi na sekondari hali iliyozua mijadala na makelele kutoka kwa wanaharakati wa haki za binadamu nchini na nje ya nchi hiyo.

Kiongozi wa chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania Zitto Kabwe aliwahi kuiandikia Benki ya Dunia kusitisha kuikopesha Tanzania dola milioni 500 za elimu kabla ya mabadiliko ya kisera kufanyika.

Vyama vya upinzani nchini Tanzania na wanaharakati wa haki za binadamu nchini humo na wa kimataifa wamekuwa wakitishia shinikizo la kutotolewa kwa mkopo huo mpaka pale Tanzania itakaporuhusu wanafunzi wanaopata ujauzito waruhusiwe kuendelea na mfumo rasmi wa elimu.
Mmh
 
Back
Top Bottom