Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Huyo dogo shule inamsumbua kwani kazi ya mbunge ni kujenga barabara? Yeye si anasema ni bilionea akanunue nyumba masaki kazi tu kulea mimba za wanaume wenzake
 
hata yeye Diamond anaweza tu kujenga barabara,mwanaume mzima unamlalamikia mdada akujengee barabara?.. anaendaga w'house sana D, ashauri wamjengee (yeye diamond) barabara ya kwenda kwake- kama vipi ahamie pale obama raod- ataishi tu' maisha popote-aende madale koooote huko atafikaje haraka sasa magogoni na hizo foleni zenu za dar!
 
Halima Mdee ana kampuni ya ujenzi wa barabara?
Siku tukijua nani wa kumwajibisha nchi yeru itasonga mbele.
Kwa sasa adui ujinga bado anatutesa
kama hana mbona aliahidi atajenga?chadema kama ccm tu
 
Chadema ukweli unauma mbunge wenu alitoa Ahadi sasa kashifa za nini tulieni mnyolewe
 
Akili yako na huyo msanii wa jini mahaba zinafanana,wewe uliona lini mbunge anajenga barabara?tena wa kutoka upinzani?serikali ndio inatakiwa kuhakikisha huduma za jamii zinapatikana kwa kutumia kodi ya wananchi.mbunge ni kuimiza serikali kutoa hizo huduma na kuzisimamia.
Hayo ni mawazo ya watu wajinga wajinga kama ninyi maana hamuoni Mbowe hakusanyi kodi lakini jimboni kwake , tena shamba huko Hai, kunajengwa barabara ya kilometa 10.

Mkiwa wapinzani wengi wasio na akili kama ninyi basi faraja kwa chama tawala.
 
Hayo ni mawazo ya watu wajinga wajinga kama ninyi maana hamuoni Mbowe hakusanyi kodi lakini jimboni kwake , tena shamba huko Hai, kunajengwa barabara ya kilometa 10.

Mkiwa wapinzani wengi wasio na akili kama ninyi basi faraja kwa chama tawala.

Wewe kwa post yako hii ndio unajiona una akili?
 
Hapa ndio Watanzania tuapoonyesha uwezo mdogo wa kufikiri, kuamua na kutenda mambo...laiti mngejiuliza tu kama kweli Diamond anaweza kutamka hivyo na kwa sababu zipi ? Diamond hana upinzani wowote na Halima, Diamond sio mwanasiasa...ajabu ni kwamba mnachukua maneno ya mleta uzi na kuanza kushambulia tu bila uhakiki wowote.

Sasa sijui ni kwa vipi huwa mnashika vichwa pale Polisi wanapomtandika virungu mwanamama ambaye tayari ameshatii amri ya kupanda difenda...kwa akili hizi sijui ni tofauti gani ya uamuzi mnayoitegemea kutoka kwao ili hali nyote mnashirikiana vinasaba hivyo hivyo vya "utanzania"...vinasaba vya kukurupuka na kutenda bila hata kwanza kujiuliza/kutafakari mara mbili "hivi huyu ninayemshambulia kosa lake haswa ni lipi ? hata kama kuna aliyeamuru piga tuu.

.....SHAME ON YOU BONGO PEOPLE.
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.

Kwani Mdee ni Manispaa yenye kujenga barabara? Anapaswa kuishangaa Serikali ya Mkoa, Manispaa na Jiji. Hao ndiyo wenye mafungu ya ujenzi nk.
 
Mleta mada pamoja na Diamond wote ni mbumbumbu. Mbunge hajengi barabara ila anaiomba Serikali ijenge, Sekali inaangalia vipaumbele vyake na pesa iliyopo. Kabla ya Mdee Jimbo hilo lilikuwa chini ya CCM kwa miaka 40 mbona hawakuweka lami? Matako yenu.
 
amwambie promota wake afanye kazi waliomkabidhi watanzania na sio kuwa promota wa nasbu
 
Tumesha ona wabunge wakihaidi vitu na vikafanyika.Hivyo kama Mbunge kama yupo yupo tu nini faida ya kuwa naye katika jimbo, au kuhimiza posho zake tu.Maendeleo huimizwa,Na huyo anaezungumzia wakati wa zilipendwa ana fikra,Sababu mambo yamesha badirika sasa enzi za J.K.N sio sawa na kipindi hiki cha J.M.K. kama ndivyo basi turudishe NMC ,Moretiko, Kauru n.k tujadili hali harisi tuliyo nayo sasa.
 
Mkuu sina matatizo na IQ yangu na inawezekana haipo kabisa, hilo halinipi wasiwasi, napata usingizi kama kawaida.
IQ yako ipo chini sana na nakupa ushauri wa bure tu ndugu yangu rudi shule
 
Halima Mdee ana kampuni ya ujenzi wa barabara?
Siku tukijua nani wa kumwajibisha nchi yeru itasonga mbele.
Kwa sasa adui ujinga bado anatutesa

alivyoahidi alikuwa na kampuni ya ujenzi?

Alivyoahidi hamkumwuliza kama ana kampuni ya ujenzi...kwani mmekuwa kama wa watoto wadogo msiojua wajibu wa mbunge ni upi??

Mdee alipokuwa anatuomba tumpe ubunge alituahidi kushughulikia matatizo ya barabara..kwani hakujua yeye si kampuni ya ujenzi?Hongera Diamond kwa kuusema ukweli Halima Mdee ni mzigo kabisa..

Sasa mwulizeni ameshughuliakiaje matatizo ya barabara......akiwapa majibu then chukueni hatua stahiki

Kwa nini aliahidi kuwaletea wananchi wa madale barabara ya lami ikiwa anajua kuwa hana kampuni ya ujenzi?

Alipokuahidi hukuhoji atailetaje hiyo barabara ya lami??

lakini kama aliahidi kujenga hiyo barabara kuna kosa gani watu kuhoji hilo kwani halima Mdee wakati anaahidi hakujua kuwa hana kampuni ya ujenzi wa barabara?

Kwa hiyo unakubaliana kwamba hujui wajibu wa mbunge...kama aliahidi kukujengea barabara ilikuwa ni sababu tosha ya kutompa kura yako maana hajui kazi/wajibu wa mbuge.

Sasa alivyotoa hiyo ahadi alitegemea zitajijenga zenyewe au!????

CDM + CCM = Ukoo Wa Panya

Ungemwuliza 2010

Hili ni swali la ushabiki wa ajabu sana! Halima ni mbunge ni wajibu wake kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma muhimu kama barabara. Acheni ushabiki usiokuwa na maana! Diamond yuko sahihi kabisa!!

Kwani ukiwa shabiki wa jambo unakuwa huna ufahamu wa mambo??

Hawa majuha wanajitoa ufahamu eti Halima Mdee anakusanya kodi? Wengine ana kampuni ya ujenzi? Wakati anawaahidi wananchi wa jimbo la Kawe hakulijua hilo? Acheni ujinga.

Wajinga ni walioahidiwa kwamba mbunge atajenga barabara na hawakuhoji atajengaje
 
Back
Top Bottom