Mmaka Sengahu
JF-Expert Member
- Jan 1, 2015
- 252
- 86
Msishangae october ikawa Zari(CCM) vs. Halima Mdee (CHADEMA)...................Brother kaanza kampeni mapeeeeema
Kwani Halima Mdee anakusanya kodi kutoka kwa wananchi au ameskia wapi kuwa mbunge ndio mwenye maamuzi ya barabara gani ijengwe? Acha Umbulula wewe
Tupo automatic kama upo manually kapime maleria!!mbona huduma hizo zikipelekwa mnawasifu wabunge? nakumbuka kuna threads nyingi tu humu zikiwasifu akina nyika dee na wengine kwa miundombinu iliyojengwa na serikali kwa nini pia wasilaumiwe kama haikujengwa? au mnamaana hata zile sifa mnazowapa wabunge wenu ni fake? double standard.
Hapo sasa kaka unatafuta kiki kwani halima mdee analalamika mara ngapi kuhusu ubovu wa miundo mbinu lakin kwakua ni upinzan hapewi nyenzo ulitaka ajenge na nn hiyo barabara mpe mshiko wako atajenga na hesabu utapewa siasa na unayofanya yametokea wapi?
level ya daimond ni wakina wema sepetu, kidoti na wengine wengene kama zari, kwa mdee kaingia chaka bovu yule ni taasisi..
Wana Ukumbi,
Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.
Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!
Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.
kwahiyo km hakukua na lami ndo na mdee kaona asiweke lami? Hebu jifungueni pingu za fikra mbn jambo jepesi hivi mnataka kuwafanya wananchi mbulula! Hata km unakipenda chama ila kikiharibu sema ukweli.
Mdee ni iron lady hilo sikatai ila kwa hili la barabara anapaswa kulaumiwa acheni siasa za maji taka! Ni bora umwambie ukweli aumie kuliko kumwambia uongo acheke! Km ndo huwa mnashauriana hivi mnampoteza mdee kwa kutanguliza uchama mbele na kujifunga macho kana kwamba hamuoni!
alivyoahidi alikuwa na kampuni ya ujenzi?