Bado watanzania wengi hatujui kazi ya mbunge haswa mbunge wa upinzani, na ndio maana utakuta watu wanauliza maswali kama haya ya msanii Diamond. Sii kazi ya mbunge wa upinzani kujenga barabara, hospitali wala shule, kazi ya mbunge wa upinzani ni kuhakikisha anaisimamia serikali kutimiza ahadi zake ilizodiahidi kwa wananchi na kama serikali ikikataa kufanya hivyo, uchaguzi ujao ni mwepesi zaidi kwa wapinzani kwa sababu hoja kuu watakao ileta ni kwamba iondoeni serikali iliyopo madarakani kwa sababu imeshindwaa kutekeeza ahadi zake. Ahadi za wapinzani wakati wa uchaguzi ni ahadi za kama wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi watafanya waliyo ahidi, sasa kura hazikutosha hawana serikali tunawadai nini?