Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Afadhali hata wasanii wanaliona hilo.

Manispaa ya Kinondoni imekazana kuweka lami mitaa yote ya Oysterbay waliko wanene.

Huku kwetu Kawe hakuna kabisa barabara za kwenye mitaa.

Ndio maana niliwahi kusema heri Mtemvu kule Temeke anafanya mambo yanayoonekana kuliko huyu kipeperushi cha CHADEMA.

Lakini mbaya zaidi, kwa hasira za wananchi bado wataichagua CHADEMA kwa vile huku KAWE CCM haipo kusikiliza kero za wananchi na kuzishughulikia.

Akili yako na huyo msanii wa jini mahaba zinafanana,wewe uliona lini mbunge anajenga barabara?tena wa kutoka upinzani?serikali ndio inatakiwa kuhakikisha huduma za jamii zinapatikana kwa kutumia kodi ya wananchi.mbunge ni kuimiza serikali kutoa hizo huduma na kuzisimamia.
 
NIMEIKUTA SEHEMU NIKASEMA ISIKUPITE.... Hasa kwa wale wanaonunua magari kwa mara ya kwanza, na hawana uzoefu wa kuendesha gari, na pia wale wote ambao wanaweza wakawa wana uzoefu wa kuendesha gari mijini, lakini hawana uzoefu wa kuendesha gari kwenye bara bara kuu za kwenda mikoani.

Lakini ni vema kila mtu aliye dereva akasoma ninachoeleza hapa. Inaweza kuokoa maisha yako ya familia yako, na wengine wanaoendesha magari au kuwa abiria.

Ndugu zangu, ukiweza kuendasha gari hapa Dar, au hata mikoani mijini, haina maana utaweza kuendesha gari pasipo tatizo kwenye barabara kuu. Nimeshuhudia watu wengi sana waliokufa kwa sababu baada ya kununua gari walikuwa na mchecheto wa ku-drive kwenda kwao kijijini.


Kuendesha gari kwenye barabara kuu ni tofauti sana na kuendesha gari mijini. Kwenye barabara kuu challenge zake ni kubwa sana kwa sababu gari zinaenda kwa kasi, na pia kuna mambo mengi ya ghafla yanayoweza kujitokeza ambayo kama huna uamuzi wa haraka kama dereva utakufa tu kabla ya kufika mwisho wa safari yako. Ukifanya kosa hata dogo barabara kuu unaweza kufa, tofauti na mijini.

Kwa mfano, ku-overtake katika barabara kuu ni jambo linatakiwa lifanywe kwa makini sana. Na pia kila unapoingia kona kali au blind spot kwenye barabara kuu weka akilini kwamba unaweza kukutana na kitu upande wako, basi linaloenda kasi, lori au trekta liloharibika, mifugo, shimo kubwa, mawe yaliyoporomoka, ajali nk. Pia unaweza kukutana ghafla na dereva mzembe anae-overtake kwenye kona na yuko upande wako.

Usithubutu ku-overtake sehemu ambayo huoni mbali mbele, na usikaribie sana gari unayotaka ku-overtake kabla ya kui-overtake. Na unapo-overtake kama una gari manual gear, rudi gia za chini kwanza ili kujenga spidi ya ku-overtake. Kama una gari automatiki, ikibidi itoe gari kwenye overdrive (unabonyeza kiswitch cha Overdrive na kuna kataa katawaka kwenye dashboard kuonyesha Overdrive iko off), hasa kama ulilkuwa umepunguza mwendo. Mara nyingine toa gia kwenye "D" na rudi kwenye "2" ili kujenga spidi ya ku-overtake, na ukishamaliza rudi kwenye D na Overdrive. Hili ni muhimu sana kwa gari za ambazo ukikanyaga accerator gari inakawia kuchanganya. Overtake kwa haraka, sehemu ambayo iko salama, na ni vizuri gari unayoi-overtake dereva wake ajue unamu-overtake. Unaweza kumpigia honi kidogo ya kuibia kama kuomba - usipige kwa nguvu ukamuudhi. Epuka kuovertake sehemu ya barabara yenye mashimo, maana dereva wa mbele anaweza kurudi upande wako ili akwepe shimo wakati tayari unamu-overtake.

Siri moja ya ku-overtake salama ni uvumilivu - overtake nzuri haitaki haraka.

Na pia kosa linaloua watu wengi sana ni ku-overtake kwa kukisia kwamba hakutakuwa na gari inayokuja upande wa pili zile sehemu ambazo huoni vizuri mbele. Hata kama barabara haina magari mengi usithubutu kukisia kwamba hakutakuwa na gari (gambling overtake).

Na pia katika barabara kuu kuna suala la uchovu - fatigue. Hili ni jambo jingine linaua sana watu wasio na uzoefu wa kuwa katika barabara kuu. Ni mbaya hata zaidi ikiwa utakaposimama mahali kwa chakula ukanywa bia - hata moja tu, kwa sababu itakuletea sana usingizi. Epuka kula vyakula vizito kama ugali na maharage, au kula hadi ukashiba sana! Ukisikia usingizi simama upumpzike, toka ndani ya gari, tembea kidogo, kabla ya kuendelea na safari. Kama ikibidi tumia Redbull (sio zaidi ya mbili).

Na jambo jingine muhimu sana la kukumbuka ni kwamba ukiingia barabara kuu, ukaendesha kwa muda fulani, akili yako inazoea spidi kali kiasi kwamba huoni tena kama unaenda spidi kali. Unaweza ukawa unaenda 140km/h ukaona kama unaenda 80km/hr. Hili huwa mara nyingi linasababisha kuacha njia na kupinduka, au kuingia kona ukiwa na spidi kubwa na gari kupinduka. Nadhani umesikia sana ajali zinazosemwa zilitokea kwa sababu dereva alishindwa kumiliki gari - ni kwa sababu akilini dereva aliona haendi spidi.

Na pia jambo jingine muhimu sana kukumbuka ni kwamba, unapoenda safari yoyote ya mbali ambayo utaendesha gari mfululizo kwa zaidi ya masaa manne, au kwa spidi zaidi ya 100km/hr, hakikisha tairi zako hazina umri zaidi ya miaka mitano, la sivyo utapata basti hata kama tairi inaonekana bado mpya kwa kuitazama. Tairi ikizidi miaka mitano haifai kusafiria safari ya mbali, japo unaweza ukaendelea kuitumia kwa safari za mijini.

Nimeona niseme haya kwa sababu nawapenda ndugu zangu. Sitaki mufe barabarani, au mniue mie na familia yangu. Wapeni taarifa wengine ili tuzidi kuepuka vifo hivi vya barabarani ambavyo vingi vinazuilika.

Neno langu la mwisho, ili uendeleee kuwa salama barabarani ni kwa lugha ya kiingereza; BE PATIENT kwa lolote unalotaka kufanya ukiwa unaendesha gari. Zingaitia hilo, utakuwa salama.
 
Halima Mdee ana kampuni ya ujenzi wa barabara?Siku tukijua nani wa kumwajibisha nchi yeru itasonga mbele.Kwa sasa adui ujinga bado anatutesa
sasa kwanini alitoa ahadi......
 
Mbunge ana ushawishi mkubwa katika miradi ya maendeleo ndani ya halmashauri husika. Pia Mdee ni mjumbe wa baraza la madiwani, manispaa ya Kinondoni ni wajibu wake kulitolea majibu swala la ujenzi wa barabara ya Wazo Hill hadi Madale na Mivumoni
 
Kama wewe ni mbunge na katika jimbo lako kero hazitatuliwi, ujue tu hauna ushawishi.

Katika hali hiyo ya kukosa ushawishi, basi hufai kuwa mwakilishi wa wananchi husika. It's simple as that.

Halima, time to go!

Ushawishi wa aina gani unaousema hapa? Hebu tupe mfano
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.
Nimesikia kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuwa mh. dr. prof. Kikwete anajigamba kua ametekeleza ahadi zake kwa +90%. Nahisi swala la barabara husika lilikua kwenye ahadi zake! Pia nataka nimuulize huyo dayimondi kuwa je alikua kwenye huo mkutano wa kampeni ya Mdee aliyotoa ahadi ya kutengeneza hiyo barabara? Je alimpigia kura mpaka anakua na jeuri ya kumdai hiyo barabara (kama hiyo ahadi ni ya kweli).
 
Huyu diamond mjinga kweli, yaani kukosa barabara kwake ndo mbunge hafai. Akafie mbali. Big up Mdee
 
Halima Mdee ni mbunge wangu lakini bahati mbaya kawaangusha sana wapiga kura wake.

Katoa ahadi nyingi sana kujenga barabarani pale Msasani mandazi 'road' alisema anajenga soko la samaki pale Kunduchi mtongani.

Muda mwingi anautumia saloon kuliko jimboni kwake nadhani muda wake umefika mwisho.
 
Last edited by a moderator:
Halima Mdee ni mbunge wangu lakini bahati mbaya kawaangusha sana wapiga kura wake.

Katoa ahadi nyingi sana kujenga barabarani pale Msasani mandazi 'road' alisema anajenga soko la samaki pale Kunduchi mtongani.

Muda mwingi anautumia saloon kuliko jimboni kwake nadhani muda wake umefika mwisho.

Hahahahahahahah hivi Gerezani ipo Kawe?! au huko huwa unaenda kugonga gahawa tu?!
 
Halima Mdee ni mbunge wangu lakini bahati mbaya kawaangusha sana wapiga kura wake.

Katoa ahadi nyingi sana kujenga barabarani pale Msasani mandazi 'road' alisema anajenga soko la samaki pale Kunduchi mtongani.

Muda mwingi anautumia saloon kuliko jimboni kwake nadhani muda wake umefika mwisho.
Halima Mdee ni dini gani?
 
Last edited by a moderator:
Halima Mdee ni mbunge wangu lakini bahati mbaya kawaangusha sana wapiga kura wake.

Katoa ahadi nyingi sana kujenga barabarani pale Msasani mandazi 'road' alisema anajenga soko la samaki pale Kunduchi mtongani.

Muda mwingi anautumia saloon kuliko jimboni kwake nadhani muda wake umefika mwisho.

lini umehamia Kawe?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom